Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SEHEMU YA 5

Huduma ya Yesu ya Baadaye Upande wa Mashariki wa Yordani

‘Watu Wengi Wamwamini’​—Yohana 10:42

Huduma ya Yesu ya Baadaye Upande wa Mashariki wa Yordani

KATIKA SEHEMU HII

SURA YA 82

Huduma ya Yesu Huko Perea

Yesu anawaeleza wasikilizaji wake jambo wanalohitaji kufanya ili kuokolewa. Ushauri wake ulikuwa muhimu wakati huo. Namna gani leo?

SURA YA 83

Kualikwa Kwenye Mlo​—Mungu Anawaalika Nani?

Akiwa kwenye mlo katika nyumba ya Farisayo, Yesu anatoa mfano kuhusu mlo mkubwa wa jioni. Anafundisha somo muhimu kwa watu wote wa Mungu. Ni somo gani hilo?

SURA YA 84

Kuwa Mwanafunzi​—Kwa Nini Ni Jambo Zito?

Kuwa mwanafunzi wa Yesu ni wajibu mzito. Yesu anaonyesha kwamba mengi yanahusika. Wengine wanashangazwa na mambo anayosema.

SURA YA 85

Kushangilia Mtenda Dhambi Anapotubu

Mafarisayo na waandishi wanamshutumu Yesu kwa kushirikiana na watu wa kawaida. Ili kuwajibu, Yesu anatumia mifano kuonyesha jinsi Mungu anavyowaona watenda dhambi.

SURA YA 86

Mwana Aliyepotea Arudi

Tunaweza kujifunza masomo gani kutokana na mfano wa Yesu wa mwana mpotevu?

SURA YA 87

Panga Mapema​—Tumia Hekima Inayotumika

Yesu anatumia mfano wa msimamizi wa nyumba mjanja na aliye fisadi kufundisha ukweli unaoshangaza.

SURA YA 88

Mabadiliko Katika Hali ya Tajiri na Lazaro

Siri ya kuuelewa mfano wa Yesu ni kuwatambua watu wanaowakilishwa na wahusika wawili wakuu.

SURA YA 89

Afundisha Huko Perea Akiwa Njiani Kwenda Yudea

Anakazia sifa inayoweza kutusaidia kuwasamehe hata wale wanaotukosea tena na tena.

SURA YA 90

“Ufufuo na Uzima”

Yesu alimaanisha nini aliposema kwamba wale wanaomwamini ‘hawatakufa kamwe’?

SURA YA 91

Lazaro Afufuliwa

Mambo mawili muhimu katika tukio hili yanafanya isiwezekane kwa wapinzani wa Yesu kupinga muujiza huo.

SURA YA 92

Watu Kumi Wenye Ukoma Waponywa​—Mmoja Ashukuru

Mtu huyo aliyeponywa anamshukuru Yesu na pia Mungu.

SURA YA 93

Mwana wa Binadamu Atafunuliwa

Kuwapo kwa Kristo kutakuwa kama radi jinsi gani?

SURA YA 94

Mambo Mawili Muhimu Sana​—Sala na Unyenyekevu

Katika mfano wa mwamuzi mwovu na mjane, Yesu anakazia thamani ya sifa fulani.

SURA YA 95

Afundisha Kuhusu Talaka na Kuwapenda Watoto

Maoni ya Yesu kuhusu watoto wadogo ni tofauti sana na maoni ya wanafunzi wake. Kwa nini?

SURA YA 96

Yesu Amjibu Mtawala Kijana Aliye Tajiri

Ni nini kinachomchochea Yesu kusema kwamba ni rahisi kwa ngamia kupitia katika tundu la sindano kuliko tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu?

SURA YA 97

Mfano wa Wafanyakazi Katika Shamba la Mizabibu

Wa kwanza wanakuwaje wa mwisho na wa mwisho wanakuwaje wa kwanza?

SURA YA 98

Mitume Wabishana Tena Kuhusu Umashuhuri

Yakobo na Yohana wanaomba kupewa vyeo vya pekee katika Ufalme, lakini wengine pia wana tamaa kama hiyo.

SURA YA 99

Yesu Awaponya Wanaume Vipofu, Kisha Amsaidia Zakayo

Inaonekana masimulizi ya Biblia kuhusu jinsi Yesu alivyomponya mwanamume kipofu karibu na Yeriko yanapingana, lakini yanawezaje kupatanishwa?

SURA YA 100

Mfano wa Mina Kumi

Yesu alimaanisha nini aliposema: “Kila mtu aliye na kitu, ataongezewa, lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa”?