Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SEHEMU YA 5

Yesu Anafanya Utumishi Wake Mashariki Mwa Yordani

“Watu Wengi Wakamuamini.”​—Yohana 10:42

Yesu Anafanya Utumishi Wake Mashariki Mwa Yordani

KATIKA SEHEMU HII

SURA YA 82

Utumishi wa Yesu Katika Perea

Yesu anaambia wasikilizaji wake kile wanapaswa kufanya ili kuokolewa. Shauri lake lilikuwa la maana zamani. Halafu leo?

SURA YA 83

Mialiko Kwenye Chakula

Wakati iko anakula kwenye nyumba ya Mufarisayo mumoja, Yesu anatoa mufano kuhusu chakula kikubwa cha mangaribi. Anatolea watu wote wa Mungu somo la maana. Ni somo gani hilo?

SURA YA 84

Kuwa Mwanafunzi wa Yesu Ni Daraka Nzito

Kuwa mwanafunzi wa Kristo ni daraka nzito. Yesu anaonyesha waziwazi mambo yenye yanaombwa ili kuwa mwanafunzi wake. Pengine maneno yake yanakwaza watu fulani wenye wangekuwa wafuasi wake.

SURA YA 85

Wanafurahi Wakati Mutenda-Zambi Anatubu

Waandishi na Wafarisayo wanamulaumu Yesu kwa sababu anasaidia watu wa kawaida. Ili kuwajibu, Yesu anatumia mifano ili kuonyesha namna Mungu anaona watenda-zambi.

SURA YA 86

Mutoto Mwenye Alipotea Anarudia

Mufano wa Yesu wa mutoto mupotevu unaweza kutufundisha nini?

SURA YA 87

Tumia Hekima Yenye Kutenda kwa Kupanga Mambo Mbele ya Wakati

Yesu anatumia mufano wa musimamizi-nyumba mujanja, na mwenye haiko mwaminifu ili kufundisha kweli yenye kushangaza.

SURA YA 88

Kubadilika kwa Hali ya Tajiri na Hali ya Lazaro

Ili kuelewa mufano wa Yesu ni lazima kutambua watu wawili wenye kuzungumuziwa sana wanafananisha nani.

SURA YA 89

Anafundisha Katika Perea Wakati Iko Anaenda Yudea

Anazungumuzia sifa yenye inaweza kutusaidia tusamehe wengine hata wale wenye wametukosea mara nyingi.

SURA YA 90

“Ufufuo na Uzima”

Yesu anamaanisha nini wakati alisema kwamba wale wenye wanamuamini “hawatakufa hata kidogo”?

SURA YA 91

Lazaro Anafufuliwa

Hali mbili za maana katika tukio hili, zinafanya isiwezekane kabisa kwa wapinzani wa Yesu kukataa muujiza.

SURA YA 92

Watu Kumi Wenye Ukoma Wanaponyeshwa ​—Mumoja Anaonyesha Shukrani

Mutu mwenye ameponyeshwa anaonyesha shukrani yake, hapana kwa Yesu tu lakini pia kwa mutu mwengine.

SURA YA 93

Mwana wa Binadamu Atafunuliwa

Namna gani kuwapo kwa Kristo kutafanana na mwangaza wa radi?

SURA YA 94

Mambo Mbili ya Lazima Sana​—Sala na Unyenyekevu

Katika mufano wake wa mwamuzi muovu na mujane, Yesu anakazia samani ya sifa fulani ya pekee.

SURA YA 95

Anafundisha Kuhusu Kuvunja Ndoa na Somo Kuhusu Watoto

Namna Yesu anaona watoto iko tofauti sana na namna wanafunzi wake wanawaona. Sababu gani?

SURA YA 96

Yesu Anamujibu Mutawala Kijana Mwenye Kuwa Tajiri

Ni nini ilimuchochea Yesu kusema kama ni vyepesi zaidi kwa ngamia kupita katika tundu la shindano ya kushonea kuliko tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu?

SURA YA 97

Mufano wa Wafanyakazi Katika Shamba la Mizabibu

Namna gani wa kwanza wanakuwa wa mwisho na wa mwisho wanakuwa wa kwanza?

SURA YA 98

Mitume Wanabishana Tena ili Kutafuta Ukubwa

Yakobo na Yohana wanaomba fasi ya pekee katika Ufalme, lakini haiko wao wenyewe tu.

SURA YA 99

Yesu Anaponyesha Vipofu Wanaume na Anasaidia Zakayo

Namna gani tunaweza kupatanisha maelezo ya Biblia yenye kuonekana kuwa tofauti, yenye kuzungumuzia Yesu akiponyesha kipofu mwanaume karibu na Yeriko?

SURA YA 100

Mufano Wake wa Mina Kumi

Yesu alimaanisha nini wakati alisema: “Kila mutu mwenye kuwa na kitu, ataongezewa, lakini ule mwenye hana, hata kile chenye iko nacho kitachukuliwa”?