Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mwige Yesu kwa Kusitawisha Sifa Zifuatazo:

Mwige Yesu kwa Kusitawisha Sifa Zifuatazo:

HURUMA

Akiwa mwanadamu mkamilifu, Yesu hakupatwa na matatizo na mahangaiko mengi yaliyowapata wanadamu wengine. Hata hivyo, aliwahurumia sana watu. Alikuwa tayari kuchukua hatua ili kuwasaidia, alifanya mengi zaidi ya ilivyokuwa kawaida. Naam, alichochewa na huruma kuwasaidia wengine. Fikiria mifano iliyo katika Sura ya 32, 37, 57, na 99.

KUFIKIKA

Watu wa kilaumri—vijana kwa wazee—walihisi kwamba wanaweza kumfikia Yesu kwa sababu hakujitenga na watu au kujiona kuwa mtu wa maana sana. Kwa kuwa watu walihisi kwamba alipendezwa nao kibinafsi, walistarehe walipokuwa pamoja naye. Ili uone jambo hilo, soma Sura ya 25, 27, na 95.

KUSALI

Yesu alisali kwa Baba yake kwa ukawaida na kwa bidii, akiwa faraghani na alipokuwa na waabudu wa kweli. Alisali pindi nyingi, si wakati tu wa mlo. Alisali ili kumshukuru Baba yake, kumsifu, na kutafuta mwongozo wake kabla ya kufanya maamuzi muhimu. Chunguza mifano iliyo kwenye Sura ya 24, 34, 91, 122, na 123.

KUTOKUWA NA UBINAFSI

Katika pindi fulani, ingawa alihitaji kupumzika au kustarehe, bado Yesu alijitolea kuwasaidia watu. Hakuwa na mtazamo wa kujitanguliza. Kwa njia hiyo pia, alituwekea kielelezo ambacho tunapaswa kufuata kwa ukaribu. Jifunze jinsi kielelezo hicho kinavyoonyeshwa kwenye Sura ya 19, 41, na 52.

KUSAMEHE

Zaidi ya kufundisha kuhusu umuhimu wa kusamehe, Yesu alionyesha sifa ya kusamehe aliposhughulika na wanafunzi wake na watu wengine. Tafakari kuhusu mifano iliyo kwenye Sura ya 26, 40, 64, 85, na 131.

BIDII

Ilitabiriwa kwamba Wayahudi wengi wangekataa kumkubali Masihi na kwamba maadui wake wangemuua. Kwa hiyo, ingekuwa rahisi kwa Yesu kutowatumikia watu kwa moyo wote. Badala yake, alikuwa na bidii katika ibada ya kweli. Aliwawekea wafuasi wake wote mfano wa kuwa na bidii wanapowahubiria watu wasiopendezwa na ujumbe wao au hata kuteswa. Soma Sura ya 16, 72, na 103.

UNYENYEKEVU

Yesu aliwazidi wanadamu wasio wakamilifu kwa njia nyingi, kwa mfano aliwazidi katika ujuzi na hekima. Alikuwa mkamilifu, basi alikuwa na uwezo wa kimwili na wa kiakili uliozidi uwezo wa watu wengine wote. Hata hivyo, aliwatumikia wengine kwa unyenyekevu. Utapata masomo kuhusu hilo katika Sura ya 10, 62, 66, 94, na 116.

SUBIRA

Pindi zote Yesu aliwaonyesha subira wanafunzi wake na watu wengine waliposhindwa kuiga mfano wake au kufuata mambo aliyofundisha. Kwa subira, alirudia masomo waliyohitaji ili wamkaribie zaidi Yehova. Fikiria mifano ya jinsi Yesu alivyoonyesha subira katika Sura ya 74, 98, 118, na 135.