Mwige Yesu kwa Kusitawisha Sifa Zifuatazo:
HURUMA
Akiwa mwanadamu mkamilifu, Yesu hakupatwa na matatizo na mahangaiko mengi yaliyowapata wanadamu wengine. Hata hivyo, aliwahurumia sana watu. Alikuwa tayari kuchukua hatua ili kuwasaidia, alifanya mengi zaidi ya ilivyokuwa kawaida. Naam, alichochewa na huruma kuwasaidia wengine. Fikiria mifano iliyo katika Sura ya 32, 37, 57, na 99.
KUFIKIKA
KUSALI
Yesu alisali kwa Baba yake kwa ukawaida na kwa bidii, akiwa faraghani na alipokuwa na waabudu wa kweli. Alisali pindi nyingi, si wakati tu wa mlo. Alisali ili kumshukuru Baba yake, kumsifu, na kutafuta mwongozo wake kabla ya kufanya maamuzi muhimu. Chunguza mifano iliyo kwenye Sura ya 24, 34, 91, 122, na 123.
KUTOKUWA NA UBINAFSI
KUSAMEHE
BIDII
Ilitabiriwa kwamba Wayahudi wengi wangekataa kumkubali Masihi na kwamba maadui wake wangemuua. Kwa hiyo, ingekuwa rahisi kwa Yesu kutowatumikia watu kwa moyo wote. Badala yake, alikuwa na bidii katika ibada ya kweli. Aliwawekea wafuasi wake wote mfano wa kuwa na bidii wanapowahubiria watu wasiopendezwa na ujumbe wao au hata kuteswa. Soma Sura ya 16, 72, na 103.
UNYENYEKEVU
Yesu aliwazidi wanadamu wasio wakamilifu kwa njia nyingi, kwa mfano aliwazidi katika ujuzi na hekima. Alikuwa mkamilifu, basi alikuwa na uwezo wa kimwili na wa kiakili uliozidi uwezo wa watu wengine wote. Hata hivyo, aliwatumikia wengine kwa unyenyekevu. Utapata masomo kuhusu hilo katika Sura ya 10, 62, 66, 94, na 116.