Hamia kwenye habari

Ufalme wa Mungu Ni nini?

Ufalme wa Mungu Ni nini?

Unafikiri ni . . .

  • kitu kilicho moyoni?

  • kitu kisicho halisi au mfano?

  • serikali iliyo mbinguni?

BIBLIA HUSEMA HIVI

“Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaharibiwa kamwe.”—Danieli 2:44, Tafsiri ya Ulimwengu Mpya.

“Kuna mwana ambaye tumepewa; na utawala wa ukuu utakuwa juu ya bega lake.”—Isaya 9:6.

FAIDA ZA KUAMINI JAMBO HILO

  • Serikali yenye uadilifu inayoweza kukufaidi kibinafsi.​—Isaya 48:17, 18.

  • Kuishi katika ulimwengu mpya unaokuja, ukiwa na afya kamili na furaha.​—Ufunuo 21:3, 4.

JE, KWELI TUNAWEZA KUAMINI KILE AMBACHO BIBLIA HUSEMA?

Ndiyo, kwa sababu mbili:

  • Yesu alionyesha mambo ambayo Ufalme wa Mungu utatimiza. Yesu aliwafundisha wafuasi wake wasali ili Ufalme wa Mungu uje na mapenzi ya Mungu yatendeke duniani. (Mathayo 6:9, 10) Yesu alionyesha jinsi sala hiyo itakavyojibiwa.

    Alipokuwa duniani, Yesu alilisha wenye njaa, aliponya wagonjwa, na akafufua wafu! (Mathayo 15:29-38; Yohana 11:38-44) Wakati huo, Yesu alionyesha mambo ambayo Ufalme huo utawafanyia raia wake atakapotawala akiwa Mfalme.—Ufunuo 11:15.

  • Hali zilizo ulimwenguni zinaonyesha kwamba Ufalme wa Mungu utakuja hivi karibuni. Yesu alitabiri kwamba kabla Ufalme wa Mungu haujaleta amani duniani, ulimwengu ungekumbwa na vita, njaa, na matetemeko ya ardhi.—Mathayo 24:3, 7.

    Tunashuhudia mambo hayo leo. Basi, tunaweza kuwa na hakika kwamba hivi karibuni Ufalme wa Mungu utakomesha matatizo hayo yote.

JAMBO LA KUFIKIRIA

Maisha yatakuwaje chini ya Ufalme wa Mungu?

Biblia inajibu swali hilo kwenye ZABURI 37:29 na ISAYA 65:21-23.