Mungu Alituumba kwa Kusudi Gani?
UNAPOSOMA magazeti, kutazama televisheni, au kusikiliza redio unapata habari nyingi kuhusu uhalifu, vita, na ugaidi. Huenda wewe pia unateseka kwa sababu ya ugonjwa au umefiwa na mpendwa wako.
Hebu jiulize:
-
Je, Mungu alikusudia maisha yangu na ya familia yangu yawe hivi?
-
Ninaweza kupata wapi msaada wa kukabiliana na matatizo yangu?
-
Je, inawezekana kuwa na amani duniani?
Biblia inajibu maswali hayo kwa njia yenye kuridhisha.
BIBLIA INAFUNDISHA KWAMBA MUNGU ATAFANYA MAMBO MAZURI DUNIANI.
-
Hakutakuwa na maumivu, kuzeeka, au kifo.—Ufunuo 21: 4
-
“Kilema ataruka kama paa.” —Isaya 35:6
-
“Macho ya vipofu yatafunguliwa.”—Isaya 35:5
- Wafu watafufuliwa.—
-
Hakuna atakayekuwa mgonjwa. —Isaya 33:24
-
Dunia itakuwa na chakula tele. —Zaburi 72:16
FAIDIKA NA MAFUNDISHO YA BIBLIA
Usidhani kwamba mambo uliyosoma kwenye kurasa zilizotangulia ni ndoto tu. Mungu ameahidi kutimiza mambo hayo hivi karibuni, na Biblia inaeleza jinsi atakavyofanya.
Biblia inafundisha mambo mengine mengi zaidi ya hayo. Inatueleza mambo ya kufanya ili tuwe na maisha yenye furaha sasa. Hebu fikiria mambo yanayokufanya uwe na wasiwasi. Labda ni kuhusu pesa, matatizo ya familia, afya, au kifo cha mpendwa wako. Biblia inaweza kukusaidia kukabiliana na matatizo hayo, na inaweza kukufariji kwa kujibu maswali yafuatayo:
Kusoma kitabu hiki kunaonyesha kwamba unataka kujua yale ambayo Biblia inafundisha. Kitabu hiki kitakusaidia. Chini ya kurasa kuna maswali ambayo yatakusaidia kuielewa vizuri Biblia. Mamilioni ya watu wamefurahia kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Tunatumaini wewe pia utafurahia. Mungu na akubariki unapojitahidi kujifunza yale ambayo Biblia inafundisha!