Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Hii Njo Maisha Yenye Mungu Anapenda Tukuwe Nayo?

Hii Njo Maisha Yenye Mungu Anapenda Tukuwe Nayo?

WAKATI unasoma gazeti, unaangalia televizyo, ao kusikiliza radio, unaona na kusikia habari za mingi juu ya kuvunja sheria, vita, na ugaidi (terrorisme). Pengine wewe pia uko unateseka juu ya ugonjwa ao juu mutu fulani mwenye unapenda amekufa.

Ujiulize hivi:

  • Hii njo maisha yenye Mungu anapenda nikuwe nayo mimi na familia yangu?

  • Ninaweza kupata wapi musaada wa kupiganisha magumu yangu?

  • Kuko siku kutakuwa amani mu dunia?

Biblia inajibu maulizo hayo kwa njia yenye kusadikisha.

BIBLIA INAFUNDISHA KAMA MUNGU ATAFANYA MAMBO YA MUZURI SANA KU DUNIA.

  • Watu hawatateseka tena, hawatazeeka tena, na hawatakufa tena.​—Ufunuo 21:4

  • “Kilema wa miguu ataruka-ruka kama paa.”​—Isaya 35:6

  • “Macho ya vipofu yatafunguliwa.”​—Isaya 35:5

  • Watu wenye wamekufa watafufuliwa.​—Yohana 5:28, 29

  • Hakuna mutu mwenye atagonjwa.​—Isaya 33:24

  • Kila mutu ku dunia atakuwa na chakula mingi.​—Zaburi 72:16

MAMBO YENYE BIBLIA INAFUNDISHA YANAWEZA KUKULETEA FAIDA

Unaweza kuwaza kama mambo yenye umesoma ku ukurasa wa 4 na wa 5 wa kitabu hiki ni ndoto tu. Lakini Mungu ametupatia ahadi (malako) ya kufanya mambo hayo ku dunia hivi karibuni, na Biblia inafasiria namna atafanya vile.

Lakini Biblia inafundisha mambo ingine ya mingi. Inatuambia mambo yenye tunapaswa kujua ili tupate furaha ya kweli na kufurahia maisha kuanzia leo. Waza kidogo juu ya mambo yenye kukuletea mahangaiko. Pengine ni mambo kama vile kukosa feza ao magumu mu familia, magonjwa, ao kifo cha mutu fulani mwenye unapenda. Biblia inaweza kukusaidia kupiganisha magumu hayo, na inaweza kukutuliza kwa kujibu maulizo kama haya:

Juu unasoma kitabu hiki, unaonyesha kama unapenda kujua mambo yenye Biblia inafundisha. Kitabu hiki kitakusaidia. Kuko maulizo ya mafungu, yenye yatakusaidia kuelewa muzuri Biblia. Watu wengi sana wamefurahia kuzungumuza juu ya Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Tunatumainia kama na wewe utafurahia jambo hilo. Mungu akubariki wakati unaendelea kujikaza ili kujua mambo yenye Biblia inafundisha!