Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 2

Biblia: Kitabu Kutoka kwa Mungu

Biblia: Kitabu Kutoka kwa Mungu

1, 2. Juu ya nini Biblia ni zawadi ya muzuri sana kutoka kwa Mungu?

UNAJISIKIA namna gani wakati rafiki yako anakupatia zawadi? Unafurahi kwa sababu rafiki yako anakukumbuka na uko na hamu sana ya kuifungua. Na unamuambia aksanti juu ya zawadi hiyo.

2 Biblia ni zawadi kutoka kwa Mungu. Inatuambia habari zenye hatuwezi kupata nafasi ingine yoyote. Kwa mufano, inatuambia kama Mungu aliumba mbingu, dunia, na mwanaume na mwanamuke wa kwanza. Inatupatia mashauri ya kutusaidia wakati tuko na magumu. Inatuambia pia kama Mungu iko na kusudi la kufanya dunia kuwa paradiso. Kwa kweli, Biblia ni zawadi ya muzuri sana!

3. Utajua nini wakati utaendelea kujifunza Biblia?

3 Wakati utaendelea kujifunza Biblia, utajua kama Mungu anapenda ukuwe rafiki yake. Kama unaendelea kujifunza mambo mingi juu yake, urafiki wako pamoja naye utaendelea kuwa wenye nguvu zaidi.

4. Ni jambo gani lenye linakushangaza sana juu ya Biblia?

4 Biblia imetafsiriwa mu luga zaidi ya 2 800, na mamiliare ya Biblia zimechapishwa. Karibu watu wote (ao, watu 9 juu ya watu 10) mu dunia wanaweza kusoma Biblia mu luga yao. Na kila juma, watu zaidi ya milioni moja wanapata Biblia! Kwa kweli, hakuna kitabu kingine chenye kuwa kama Biblia.

5. Juu ya nini tunasema kama Biblia ‘imeongozwa na roho ya Mungu’?

5 Biblia ‘imeongozwa na roho ya Mungu.’ (Soma 2 Timoteo 3:16.) Lakini watu fulani wanaweza kusema hivi: ‘Wanadamu njo waliandika Biblia. Sasa, juu ya nini tunasema kama ilitoka kwa Mungu?’ Biblia inajibu hivi: “Wanadamu walisema yenye yalitoka kwa Mungu wakiongozwa na roho takatifu.” (2 Petro 1:21) Ni kama vile tate (nkambo) anaambia mujukuu (munkana) wake amuandikie barua. Barua hiyo ni ya nani? Ni ya tate huyo, haiko ya mujukuu wake. Vilevile mawazo yenye kuwa mu Biblia ni ya Mungu, haiko ya wanadamu wenye alitumia ili kuiandika. Mungu aliwaongoza ili waandike mawazo yake. Kwa kweli, Biblia ni “neno la Mungu.”​—1 Watesalonike 2:13; ona Mafasirio Ingine ya 2.

Biblia​—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya inapatikana mu luga za mingi

BIBLIA INASEMA KWELI

6, 7. Juu ya nini tunasema kama Biblia inapatana?

6 Biblia iliandikwa kwa miaka zaidi ya 1 600. Watu wenye waliandika Biblia hawakuishi wakati mumoja. Wamoja walikuwa watu wenye kusoma sana, na wengine hawakusoma sana. Kwa mufano, mumoja alikuwa munganga. Wengine walikuwa walimaji, wengine walikuwa wanavua ao kuloa samaki, wengine walikuwa wachungaji wa wanyama, manabii, waamuzi, na wafalme. Hata kama watu mbalimbali njo waliandika Biblia, sehemu zote za Biblia zinapatana. Habari zote zenye kuwa mu Biblia zinapatana. *

7 Kitabu cha kwanza cha Biblia kinazungumuzia namna magumu yalianza mu dunia, na kitabu cha mwisho kinazungumuzia namna Mungu atatosha magumu hayo kwa kufanya dunia kuwa paradiso. Biblia inazungumuzia historia ya wanadamu tangu zamani na inaonyesha kama kusudi la Mungu linatimia sikuzote.

8. Biblia inasema kweli wakati inazungumuzia mambo ya sayansi? Leta mifano.

8 Biblia haikuandikwa juu ya kufundisha watu mambo ya sayansi. Lakini sikuzote inasema kweli juu ya mambo ya sayansi. Na hilo halishangaze kwa sababu ni kitabu kutoka kwa Mungu. Kwa mufano, kitabu cha Mambo ya Walawi kiko na sheria zenye Mungu alipatia Waisraeli juu ya namna ya kuzuia magonjwa yasiambukie watu wengine. Sheria hizo ziliandikwa muda murefu mbele watu wajue namna mikrobe na virusi vinaleta magonjwa. Biblia inafundisha pia kama hakuna kitu chenye kinakamata dunia. (Yobu 26:7) Na wakati watu wengi waliamini kama dunia iko tambarare (plat), Biblia ilisema kama dunia iko muviringo.​—Isaya 40:22.

9. Watu wenye waliandika Biblia walisema mambo ya kweli. Hilo linaonyesha nini?

9 Wakati Biblia inazungumuzia mambo ya historia, inasema kweli sikuzote. Lakini, vitabu mingi vya historia viko na makosa kwa sababu watu wenye waliviandika hawakusema mambo ya kweli sikuzote. Kwa mufano, wakati fulani hawakuandika namna inchi zao zilishindwa ku vita. Lakini watu wenye waliandika Biblia walisema kweli hata wakati Waisraeli walishindwa ku vita. Tena waliandika juu ya makosa yao. Kwa mufano, mu kitabu cha Hesabu, Musa anaonyesha namna alifanya kosa kubwa na Mungu alimupatia nizamu ao malipizi juu ya kosa hilo. (Hesabu 20:2-12) Kwa sababu watu wenye waliandika Biblia waliandika mambo ya kweli, hilo linaonyesha kama Biblia inatoka kwa Mungu. Maana yake, tunaweza kutumainia Biblia.

KITABU CHENYE KUWA NA MASHAURI MINGI YA MUZURI

10. Sababu gani mashauri ya Biblia yanaweza kutusaidia leo?

10 Biblia ‘imeongozwa na roho ya Mungu na iko na faida kwa kufundisha, kwa kukaripia, kwa kunyoosha mambo.’ (2 Timoteo 3:16) Kwa kweli, mashauri ya Biblia yanaweza kutusaidia leo. Ni Yehova alituumba; kwa hiyo, anaelewa namna yetu ya kuwaza na namna tunajisikia. Anatujua muzuri zaidi kuliko namna tunajijua, na anapenda tukuwe na furaha. Anajua mambo yenye kuwa ya muzuri kwetu na yenye kuwa ya mubaya kwetu.

11, 12. (a) Yesu alitoa mashauri gani ya muzuri mu Matayo sura ya 5 mupaka sura ya 7? (b) Ni kanuni gani zenye faida zenye kuwa mu Biblia?

11 Mu Matayo sura ya 5 mupaka sura ya 7, Yesu alitutolea mashauri ya muzuri. Kwa mufano, alituonyesha namna ya kupata furaha, namna ya kusikilizana na wengine, namna ya kusali, na namna ya kuwa na mawazo ya muzuri juu ya feza. Hata kama kumepita miaka 2 000 tangu wakati alitoa mashauri hayo, yangali ya maana sana na yenye faida leo.

12 Mu Biblia, Yehova anatupatia pia kanuni. Kanuni hizo zinatusaidia kuwa na maisha ya familia yenye furaha, kuwa wafanyakazi wazuri, na kuishi kwa amani pamoja na wengine. Kanuni za Biblia zinaweza kutusaidia sikuzote, hata kama tuko watu wa namna gani, tunaishi wapi, ao tuko na magumu ya namna gani.​—Soma Isaya 48:17; ona Mafasirio Ingine ya 3.

UNAWEZA KUAMINI UNABII WENYE KUWA MU BIBLIA

Isaya, muandikaji mumoja wa Biblia, alitabiri kama Babiloni ingeharibiwa

13. Isaya alitabiri nini juu ya muji wa Babiloni?

13 Unabii mbalimbali wenye kuwa mu Biblia umekwisha kutimia. Kwa mufano, Isaya alitabiri kama muji wa Babiloni ungeharibiwa. (Isaya 13:19) Alionyesha waziwazi namna muji huo ungeharibiwa. Muji huo ulilindwa na milango mikubwa-mikubwa na mutoni. Lakini, Isaya alitabiri kama mutoni ungekaushwa na milango ingeachwa wazi. Maaskari wangekamata muji huo bila kupigana vita. Isaya alitabiri pia kama mwanaume mwenye kuitwa Koreshi njo angeharibu Babiloni.​—Soma Isaya 44:27–45:2; ona Mafasirio Ingine ya 4.

14, 15. Namna gani unabii wa Isaya ulitimia?

14 Miaka 200 kisha unabii huo kuandikwa, maaskari walikuja kushambulia muji wa Babiloni. Ni nani alikuwa kiongozi wa maaskari hao? Alikuwa Koreshi, mufalme wa Uajemi, kama vile tu unabii ulikuwa umesema. Lakini maaskari wa Koreshi waliingia mu Babiloni kama vile unabii ulikuwa umetabiri?

15 Usiku wenye walishambulia muji huo, Wababiloni walikuwa wanafanya karamu. Waliwaza kama walikuwa salama kwa sababu walikuwa wanalindwa na kuta kubwa na mutoni. Inje ya muji, Koreshi na maaskari wake walikuwa wanachimba mufereji ili kugeuza njia ya maji na kufanya maji ya mutoni yapunguke. Maji yalipunguka kabisa na maaskari wa Uajemi waliweza kutembea ndani ya mutoni. Lakini namna gani maaskari wa Koreshi wangeingia mu muji wa Babiloni wenye ulikuwa na kuta kubwa? Kama vile tu unabii ulisema, milango ya muji iliachwa wazi; kwa hiyo, maaskari walikamata muji bila kupigana vita.

16. (a) Isaya alitabiri nini juu ya muji wa Babiloni? (b) Ni nini inaonyesha kama unabii wa Isaya ulitimia?

16 Isaya alitabiri kama hakuna mutu mwenye angeishi tena mu muji wa Babiloni. Aliandika hivi: “Haitaikaliwa na watu hata siku moja, wala haitakuwa mahali pa kuishi kwa vizazi vyote.” (Isaya 13:20) Unabii huo ulitimia? Ndiyo, mahali kwenye muji huo ulikuwa zamani mu inchi ya Iraki, ni kusema, kwenye kilometre 80 hivi kusini mwa muji wa Baghdad, ni mabomoko tu njo yamebakia pale. Hata leo hakuna mutu mwenye anaishi pale. Yehova alifagia muji wa Babiloni “kwa ufagio wa uharibifu.”​—Isaya 14:22, 23. *

Mabomoko ya Babiloni

17. Juu ya nini tunaweza kuamini ahadi zote za Mungu?

17 Unabii mbalimbali wa Biblia umekwisha kutimia. Kwa hiyo, tunaweza kuamini mambo yenye Biblia inasema juu ya wakati wenye kuja. Tunaweza kuwa hakika kama Yehova atatimiza ahadi (malako) yake ya kufanya dunia ikuwe paradiso. (Soma Hesabu 23:19.) Kwa kweli, tuko na tumaini la “uzima wa milele wenye Mungu, mwenye hawezi kusema uongo, aliahidi zamani sana.”​—Tito 1:2. *

BIBLIA INAWEZA KUGEUZA MAISHA YAKO

18. Paulo alisema nini juu ya “neno la Mungu”?

18 Tumejifunza kama hakuna kitabu kingine chenye kuwa sawa na Biblia. Inapatana, na wakati inazungumuzia mambo ya sayansi ao ya historia, inasema kweli sikuzote. Inatutolea pia mashauri mingi ya muzuri na iko na unabii mingi wenye umekwisha kutimia. Lakini kuko sababu ingine yenye kufanya Biblia ikuwe kitabu cha ajabu. Mutume Paulo aliandika hivi: “Neno la Mungu liko na uzima na liko na nguvu.” Maana yake nini?​—Soma Waebrania 4:12.

19, 20. (a) Namna gani Biblia inaweza kukusaidia kujichunguza? (b) Namna gani unaweza kuonyesha kama unaona zawadi ya Biblia kuwa ya maana?

19 Biblia inaweza kugeuza maisha yako. Inaweza kukusaidia kujichunguza ao kujiangalia sana. Inaweza kutusaidia kuelewa mambo yenye kuwa ndani kabisa ya akili yetu na moyo wetu. Kwa mufano, tunaweza kuwaza kama tunapenda Mungu. Lakini, ili tuonyeshe kama tunamupenda, tunapaswa kutumikisha mambo yenye Biblia inasema.

20 Kwa kweli Biblia ni kitabu kutoka kwa Mungu. Anapenda usome Biblia, ujifunze Biblia, na kuipenda. Uonyeshe kama unaona zawadi hiyo kuwa ya maana kwa kuendelea kujifunza. Kisha utaelewa kusudi la Mungu juu ya wanadamu. Mu habari yenye kufuata, tutajifunza mambo mingi zaidi juu ya kusudi hilo.

^ fu. 6 Watu fulani wanasema kama Biblia haipatane, lakini ile haiko kweli. Ona sura ya 7 ya kitabu Biblia​—Neno la Mungu au la Binadamu? chenye kilichapishwa na Mashahidi wa Yehova.

^ fu. 16 Kama unapenda kujua mambo ingine juu ya unabii wa Biblia, unaweza kusoma ukurasa wa 27-29 wa broshua Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, yenye ilichapishwa na Mashahidi wa Yehova.

^ fu. 17 Unabii juu ya kuharibiwa kwa muji wa Babiloni ni moja tu kati ya unabii mbalimbali wa Biblia wenye umekwisha kutimia. Unaweza kupata habari juu ya unabii wenye kuhusu Yesu Kristo mu Mafasirio Ingine ya 5.