Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 4

Yesu Kristo Ni Nani?

Yesu Kristo Ni Nani?

1, 2. (a) Kama unajua tu jina la mutu fulani mwenye kujulikana, ni kusema unamujua muzuri? Fasiria. (b) Watu wanasemaka nini juu ya Yesu?

KATIKA dunia, kuko watu wengi wenye kujulikana. Pengine unajua jina la mutu fulani mwenye kujulikana. Lakini, kujua tu jina lake haiko kusema kama unamujua muzuri. Haujue mambo yote juu ya maisha yake na haujue yeye ni mutu wa namna gani kabisa.

2 Pengine umekwisha kusikia habari juu ya Yesu Kristo, hata kama kumepita miaka 2 000 hivi tangu wakati aliishi mu dunia. Lakini watu wengi hawajue Yesu alikuwa nani kabisa. Watu fulani wanasema kama alikuwa mutu muzuri, wengine wanasema kama alikuwa nabii, na wengine wanaamini kama yeye ni Mungu. Wewe unawaza nini?​—Ona Mafasirio Ingine ya 12.

3. Juu ya nini ni jambo la maana ujue kweli juu ya Yehova Mungu na Yesu Kristo?

3 Ni jambo la maana ujue kweli juu ya Yesu. Juu ya nini? Biblia inasema hivi: “Uzima wa milele ndio huu, wafikie kukujua wewe Mungu wa pekee wa kweli, na ule mwenye ulituma, Yesu Kristo.” (Yohana 17:3) Kwa kweli, ikiwa unajua kweli juu ya Yehova na Yesu, unaweza kuishi milele mu dunia paradiso. (Yohana 14:6) Tena, kujua Yesu kutakusaidia hata leo kwa sababu Yesu alituonyesha namna tunapaswa kuishi, na namna tunapaswa kuwatendea wengine. (Yohana 13:34, 35) Mu Sura ya 1, tulijifunza kweli juu ya Mungu. Sasa tutajifunza mambo yenye Biblia inafundisha juu ya Yesu.

TUMEMUPATA MASIYA!

4. Majina “Masiya” na “Kristo” maana yake nini?

4 Miaka mingi mbele Yesu azaliwe, Yehova alisema kupitia Biblia kama angetuma Masiya, ao Kristo. Neno “Masiya” linatoka mu luga ya Kiebrania na neno “Kristo” linatoka mu luga ya Kigiriki. Majina hayo mbili maana yake, “mutiwa mafuta,” ni kusema, ule mwenye Mungu amechagua ili kumupatia cheo fulani cha pekee. Masiya atatimiza ahadi zote za Mungu. Yesu anaweza pia kukusaidia leo. Lakini, mbele Yesu azaliwe, watu wengi walijiuliza hivi: ‘Ni nani atakuwa Masiya?’

5. Wanafunzi wa Yesu waliamini kabisa kama alikuwa Masiya?

5 Wanafunzi wa Yesu waliamini kabisa kama Yesu alikuwa Masiya. (Yohana 1:41) Kwa mufano, Simoni Petro aliambia Yesu hivi: “Wewe ndiye Kristo.” (Matayo 16:16) Namna gani tunaweza kuamini kabisa kama Yesu ni Masiya?

6. Namna gani Yehova alisaidia watu waaminifu wamutambue Masiya?

6 Miaka mingi mbele Yesu azaliwe, manabii wa Mungu waliandika mambo mingi yenye yangesaidia watu wamutambue Masiya. Namna gani habari hizo zingewasaidia? Wazia mutu fulani anakuomba uende kwenye bisi zinasimamaka kwenye kuwa watu wengi sana ili kumupokea mutu fulani mwenye haujaonaka. Kama unapewa mafasirio ya muzuri juu ya mutu mwenye unaenda kutafuta, unaweza kumutambua. Vilevile, Yehova alitumia manabii ili waandike mambo yenye Masiya angefanya na mambo yenye yangemupata. Kutimia kwa unabii huo wote kunasaidia watu waaminifu wajue kama Yesu ni Masiya.

7. Ni unabii gani mbili wenye unaonyesha kabisa kama Yesu ni Masiya?

7 Tuzungumuzie unabii mbili juu ya Masiya. Kwanza, miaka 700 mbele Yesu azaliwe, Mika alitabiri kama Masiya angezaliwa mu muji mudogo wa Betlehemu. (Mika 5:2) Na Yesu alizaliwa mu muji huo! (Matayo 2:1, 3-9) Pili, Danieli alitabiri kama Masiya angetokea mu mwaka wa 29. (Danieli 9:25) Unabii huo mbili, na unabii mwingine unaonyesha kabisa kama Yesu ni Masiya mwenye aliahidiwa.​—Ona Mafasirio Ingine ya 13.

Wakati Yesu alibatizwa, akakuwa Masiya, ao Kristo

8, 9. Ni jambo gani lilitokea wakati Yesu alibatizwa? Na jambo hilo linaonyesha kabisa nini?

8 Yehova alionyesha waziwazi kama Yesu ni Masiya. Mungu alimupatia Yohana Mubatizaji ahadi (malako) kama angemupatia alama yenye ingemusaidia kutambua Masiya. Yohana aliona alama hiyo wakati Yesu alimuendea ili amubatize katika Mutoni Yordani mu mwaka wa 29. Biblia inatuambia jambo lenye lilitokea. Inasema hivi: “Kisha kubatizwa, Yesu akapanda mara moja kutoka katika maji; na angalia, mbingu zikafunguka, na Yohana akaona roho ya Mungu ikishuka kama njiwa, ikikuja juu ya Yesu. Angalia! Sauti ikatoka pia mbinguni, na kusema: ‘Huyu ni Mwana wangu, mupendwa, mwenye nimekubali.’” (Matayo 3:16, 17) Wakati Yohana aliona na kusikia alama hiyo, alijua kama Yesu alikuwa Masiya. (Yohana 1:32-34) Siku hiyo, wakati Yehova alishusha roho yake takatifu juu ya Yesu, Yesu akakuwa Masiya. Yeye njo Mungu alikuwa amechagua ili akuwe Kiongozi na Mufalme.​—Isaya 55:4.

9 Unabii wa Biblia, maneno ya Yehova mwenyewe, na alama yenye alitoa wakati Yesu alibatizwa, vinaonyesha kabisa kama Yesu ni Masiya. Lakini, Yesu alitoka wapi, na alikuwa mutu wa namna gani? Tuone mambo yenye Biblia inasema.

YESU ALITOKA WAPI?

10. Biblia inafundisha nini juu ya maisha ya Yesu mbele akuje mu dunia?

10 Biblia inafundisha kama Yesu aliishi mbinguni kwa muda murefu mbele akuje mu dunia. Mika alisema kama Masiya alikuwa “kuanzia nyakati za zamani.” (Mika 5:2) Yesu yeye mwenyewe alisema kama aliishi mbinguni mbele akuwe mwanadamu. (Soma Yohana 3:13; 6:38, 62; 17:4, 5.) Hata mbele akuje mu dunia, Yesu alikuwa na urafiki wa pekee pamoja na Yehova.

11. Juu ya nini Yehova anamupenda sana Yesu?

11 Yehova anamupenda sana Yesu. Juu ya nini? Juu yeye njo Yehova aliumba kwanza, mbele ya vitu vingine vyote. Njo maana Yesu anaitwa “muzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.” * (Wakolosai 1:15) Pia, Yehova anamupenda sana Yesu juu ni yeye tu njo Yehova aliumba moja kwa moja. Njo maana anaitwa “Mwana . . . muzaliwa-pekee.” (Yohana 3:16) Tena, ni Yesu tu njo Yehova alitumia ili kuumba vitu vingine vyote. (Wakolosai 1:16) Na Yesu tu njo anaitwa “Neno,” juu Yehova alimutumia ili kupatia malaika na wanadamu ujumbe na maagizo.​—Yohana 1:14.

12. Ni nini inaonyesha kama Yesu na Mungu hawako mutu mumoja?

12 Watu fulani wanaamini kama Yesu na Mungu ni mutu mumoja. Lakini, Biblia haifundishe vile. Biblia inasema kama Yesu aliumbwa, maana yake Yesu alikuwa na mwanzo. Lakini Yehova, mwenye aliumba vitu vyote, hana mwanzo. (Zaburi 90:2) Yesu, Mwana wa Mungu, hajapima hata siku moja kukamata nafasi ya Mungu. Biblia inafundisha waziwazi kama Baba ni mukubwa kuliko Mwana. (Soma Yohana 14:28; 1 Wakorinto 11:3.) Yehova tu njo “Mungu Mweza-Yote.” (Mwanzo 17:1) Yeye njo mutu mukubwa zaidi na mwenye nguvu zaidi mu ulimwengu.​—Ona Mafasirio Ingine ya 14.

13. Juu ya nini Biblia inasema kama Yesu ni “mufano wa Mungu mwenye haonekane”?

13 Yehova na Mwana wake Yesu, walitumika pamoja kwa miaka mingi sana mbele ya kuumbwa kwa mbingu na dunia. Kwa kweli, walipendana sana! (Yohana 3:35; 14:31) Yesu alionyesha kabisa sifa za Baba yake njo maana Biblia inamuita “mufano wa Mungu mwenye haonekane.”​—Wakolosai 1:15.

14. Namna gani Yesu alifikia kuwa mwanadamu?

14 Mwana mupendwa wa Yehova alikuwa tayari kuacha makao yake mbinguni na kuwa mwanadamu. Hilo liliwezekana namna gani? Yehova alifanya muujiza: alihamisha uzima wa Mwana wake kutoka mbinguni na akautia mu tumbo la uzazi la bikira mwenye aliitwa Maria. Kwa hiyo, Yesu hakukuwa na baba mwanadamu. Maria alizaa mutoto mukamilifu, na akamupatia jina Yesu.​—Luka 1:30-35.

YESU ALIKUWA MUTU WA NAMNA GANI?

15. Unaweza kufanya nini ili ufikie kumujua Yehova muzuri zaidi?

15 Unaweza kujifunza mambo mingi juu ya Yesu, maisha yake, na sifa zake kwa kusoma kitabu cha Matayo, Marko, Luka, na Yohana. Vitabu hivyo vya Biblia vinaitwa Injili. Juu Yesu iko na sifa kama za Baba yake, mambo yenye utasoma mu vitabu hivyo, yatakusaidia pia ufikie kumujua Yehova muzuri zaidi. Njo maana Yesu alisema hivi: “Kila mutu mwenye ameniona mimi amemuona Baba pia.”​—Yohana 14:9.

16. Yesu alifundisha nini? Mambo yenye Yesu alifundisha yalitoka wapi?

16 Watu wengi walimuita Yesu “Mwalimu.” (Yohana 1:38; 13:13) Jambo moja kati ya mambo ya maana zaidi yenye Yesu alifundisha ni “habari njema ya Ufalme.” Ufalme huo ni nini? Ni serikali ya Mungu yenye kuwa mbinguni. Serikali hiyo itatawala dunia yote na italetea baraka watu wenye kumutii ao kumusikia Mungu. (Matayo 4:23) Mambo yote yenye Yesu alifundisha yalitoka kwa Yehova. Yesu alisema hivi: “Mambo yenye ninafundisha haiko yangu, lakini ni ya ule mwenye alinituma.” (Yohana 7:16) Yesu alijua kama Yehova anapenda watu wasikie hii habari njema yenye kusema kama Ufalme wa Mungu utatawala dunia.

17. Yesu alifundisha wapi? Juu ya nini alijikaza sana kufundisha watu?

17 Yesu alifundisha wapi? Alifundisha kila mahali kwenye alikuta watu. Alifundisha mu vijiji, na mu miji, mu soko, mahali pa ibada, na mu nyumba za watu. Hakungojea watu wakuje kumutafuta. Mara nyingi yeye njo alienda kuwatafuta. (Marko 6:56; Luka 19:5, 6) Yesu alitumika sana na alitumia wakati murefu na nguvu mingi ili kufundisha watu. Juu ya nini? Juu alijua kama Mungu alipenda afanye vile na juu alimutii Baba yake sikuzote. (Yohana 8:28, 29) Pia, Yesu alihubiria watu juu alikuwa anawasikilia huruma. (Soma Matayo 9:35, 36.) Aliona namna wakubwa wa dini (religion) hawakukuwa wanafundisha watu kweli juu ya Mungu na Ufalme wake. Kwa hiyo, alipenda kusaidia watu wengi zaidi wasikie habari njema.

18. Ni sifa gani za Yesu zenye unapenda sana?

18 Yesu alipenda watu na aliwahangaikia. Alikuwa mwema na watu walijisikia huru kuzungumuza naye. Hata watoto walipenda kuwa pamoja naye. (Marko 10:13-16) Yesu alitenda kwa haki sikuzote. Alichukia mambo ya udanganyifu na ya ukosefu wa haki. (Matayo 21:12, 13) Aliishi wakati wenye wanamuke walikuwa wanazarauliwa na kuimwa haki fulani. Lakini sikuzote Yesu alitendea wanamuke muzuri na kwa heshima. (Yohana 4:9, 27) Tena, Yesu alikuwa munyenyekevu kabisa. Kwa mufano, mangaribi moja alinawisha mitume wake miguu; kwa kawaida mutumishi njo alikuwa anafanya kazi ya kunawisha watu miguu.​—Yohana 13:2-5, 12-17.

Yesu alihubiri kila mahali kwenye alikuta watu

19. Ni mifano gani yenye kuonyesha kama Yesu alijua mambo yenye watu walikuwa nayo lazima kabisa na kama alipenda kuwasaidia?

19 Yesu alijua mambo yenye watu walikuwa nayo lazima kabisa, na alipenda kuwasaidia. Jambo hilo lilionekana wazi wakati alitumia nguvu yenye Mungu alimupatia ili kuponyesha watu kwa njia ya muujiza. (Matayo 14:14) Kwa mufano, mwanaume mumoja mwenye alikuwa na ugonjwa wa ukoma alikuja kwa Yesu na kusema hivi: “Kama tu unataka, unaweza kunifanya nikuwe safi.” Wakati Yesu aliona maumivu na mateso ya mwanaume huyo, alimusikilia huruma na akapenda kumusaidia. Kwa hiyo, Yesu akanyoosha mukono wake, akagusa mwanaume huyo, na kumuambia hivi: “Ninataka! Kuwa safi.” Na mwanaume huyo mwenye alikuwa mugonjwa akapona! (Marko 1:40-42) Wazia namna mwanaume huyo alifurahi sana!

SIKUZOTE ALIKUWA MUAMINIFU KWA BABA YAKE

20, 21. Namna gani Yesu alionyesha mufano muzuri wa kumutii Mungu?

20 Yesu alionyesha mufano muzuri zaidi wa kumutii Mungu. Hata wakati hali ilikuwa ya nguvu ao wakati maadui wake walimutendea mubaya, alibakia muaminifu kwa Baba yake. Kwa mufano, Yesu hakufanya zambi wakati Shetani alimujaribu. (Matayo 4:1-11) Watu fulani wa familia yake mwenyewe hawakuamini kama alikuwa Masiya na walisema kama “amepoteza akili,” lakini Yesu aliendelea kufanya kazi ya Mungu. (Marko 3:21) Wakati maadui wake walikuwa wanamutesa, alibakia muaminifu kwa Mungu na hakupima hata kidogo kuwatendea mubaya.​—1 Petro 2:21-23.

21 Mbele Yesu akufe, aliteseka sana. Lakini alibakia muaminifu kwa Yehova. (Soma Wafilipi 2:8.) Wazia mambo yote yenye alivumilia siku yenye alikufa. Alikamatwa, mashahidi wa uongo walimusingizia kuwa alimutukana Mungu, waamuzi wenye hawana haki walimuhukumu, kikundi cha watu kilimuchekelea, na maaskari walimutesa na kumupigilia misumari ku muti. Wakati alikaribia kufa, alisema hivi kwa sauti kubwa: “Imetimizwa!” (Yohana 19:30) Siku tatu kisha Yesu kufa, Yehova alimufufua na kumupatia mwili wa roho. (1 Petro 3:18) Kisha majuma kidogo, Yesu alirudia mbinguni, ‘akakaa kwenye mukono wa kuume wa Mungu,’ na kungojea Mungu amufanye kuwa Mufalme.​—Waebrania 10:12, 13.

22. Tuko na nafasi gani leo kwa sababu Yesu alibakia muaminifu kwa Baba yake?

22 Kwa sababu Yesu alibakia muaminifu kwa Baba yake, leo tuko na nafasi ya kuishi milele mu dunia paradiso, kama vile tu Yehova alikusudia. Mu habari yenye kufuata, tutazungumuzia namna kifo cha Yesu kinafanya iwezekane tuishi milele.

^ fu. 11 Yehova anaitwa Baba juu yeye njo Muumbaji. (Isaya 64:8) Yesu anaitwa Mwana wa Mungu juu Yehova njo alimuumba. Malaika, na wanadamu wanaitwa pia wana wa Mungu.​—Yobu 1:6; Luka 3:38.