Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 5

Bei ya Ukombozi: Zawadi Kubwa Zaidi Kutoka kwa Mungu

Bei ya Ukombozi: Zawadi Kubwa Zaidi Kutoka kwa Mungu

1, 2. (a) Ni nini inafanya zawadi fulani ikuwe ya maana kwako? (b) Juu ya nini bei ya ukombozi njo zawadi kubwa zaidi kutoka kwa Mungu?

NI ZAWADI gani ya muzuri zaidi yenye umekwisha kupata? Ili zawadi ikuwe ya maana kwako, haiko lazima ikuwe ya bei sana. Unafurahia zawadi wakati inakuletea furaha ao wakati zawadi hiyo ni kitu fulani chenye ulikuwa nacho lazima kabisa.

2 Mungu ametupatia zawadi nyingi. Lakini kati ya zawadi hizo kuko moja yenye tuko nayo lazima sana. Njo zawadi kubwa zaidi yenye Mungu amepatia wanadamu. Mu sura hii, tutajifunza kama Yehova alimutuma Mwana wake, Yesu Kristo, ili tupate uzima wa milele. (Soma Matayo 20:28.) Wakati alimutuma Yesu mu dunia ili akuwe bei ya ukombozi, Yehova alionyesha kama anatupenda kabisa.

BEI YA UKOMBOZI NI NINI?

3. Juu ya nini watu wanakufaka?

3 Bei ya ukombozi ni njia yenye Yehova alitumia ili kukomboa wanadamu kutoka katika zambi na kifo. (Waefeso 1:7) Ili kuelewa juu ya nini bei ya ukombozi ilikuwa ya lazima, tunapaswa kujua mambo yenye yalitokea mu bustani ao shamba la Edeni miaka mingi yenye imepita. Wazazi wetu wa kwanza, Adamu na Eva, walifanya zambi. Kwa hiyo, walikufa kwa sababu walifanya zambi. Sisi pia tunakufaka juu tuliriti zambi kutoka kwa Adamu na Eva.​—Ona Mafasirio Ingine ya 9.

4. Adamu alikuwa nani, na Yehova alimupatia nini?

4 Wakati Yehova alimuumba Adamu, mwanaume wa kwanza, alimupatia kitu fulani cha maana sana. Alimupatia Adamu uzima mukamilifu. Alikuwa na akili kamilifu na mwili mukamilifu. Hangegonjwa hata kidogo, hangezeeka, na hangekufa. Kwa sababu Yehova njo alimuumba Adamu, alikuwa kama baba yake. (Luka 3:38) Yehova alizungumuza naye mara kwa mara. Alimuambia Adamu waziwazi mambo yenye alitaka afanye na alimupatia kazi yenye kufurahisha.​—Mwanzo 1:28-30; 2:16, 17.

5. Biblia inasema kama Adamu aliumbwa “kwa mufano wa Mungu.” Maana yake nini?

5 Adamu aliumbwa “kwa mufano wa Mungu.” (Mwanzo 1:27) Wakati Yehova alimuumba alimupatia sifa kama zake; sifa kama vile upendo, hekima, haki, na nguvu. Alimupatia Adamu uhuru wa kuchagua. Adamu hakukuwa kama mashine. Mungu alimuumba na uhuru wa kuchagua kufanya mambo ya muzuri ao mambo ya mubaya. Adamu angechagua kumutii ao kumusikia Mungu, angeishi milele mu Paradiso.

6. Wakati Adamu alikosa kumutii Mungu, alipoteza nini? (b) Kukosa kutii kwa Adamu kunatuletea matokeo gani?

6 Wakati Adamu alifanya zambi alipewa hukumu ya kifo. Kwa hiyo, alipoteza mambo mingi. Alipoteza urafiki wake wa pekee pamoja na Yehova, uzima wake mukamilifu, na Paradiso kwenye alikuwa anaishi. (Mwanzo 3:17-19) Adamu na Eva walichagua kukosa kumutii Mungu, kwa hiyo, walipoteza tumaini lao. Juu ya jambo lenye Adamu alifanya, “zambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia zambi, na ni vile kifo kilienea kwa watu wote kwa sababu wote walikuwa wamefanya zambi.” (Waroma 5:12) Wakati Adamu alifanya zambi, ‘alijiuzisha’ yeye mwenyewe na ‘kutuuzisha’ sisi pia katika utumwa wa zambi na kifo. (Waroma 7:14) Kuko tumaini fulani kwa ajili yetu? Ndiyo. Yehova alitutolea bei ya ukombozi.

7, 8. Bei ya ukombozi ni nini?

7 Bei ya ukombozi ni nini? Bei ya ukombozi iko na maana mbili. Kwanza, bei ya ukombozi ni bei yenye inalipwa ili kuachilia mutu fulani ao ili kukomboa kitu fulani. Pili, bei ya ukombozi ni bei yenye kufunika ao kulipia garama ya kitu fulani.

8 Hakuna mwanadamu mwenye angeweza kulipia mambo yenye Adamu alipoteza wakati alifanya zambi na kutuletea kifo. Lakini, Yehova alifanya mupango wa kutukomboa kutoka katika zambi na kifo. Tuzungumuzie basi namna bei ya ukombozi ilitolewa na faida zenye inatuletea.

NAMNA GANI YEHOVA ALITOA BEI YA UKOMBOZI?

9. Bei ya ukombozi ingelipwa namna gani?

9 Hakuna mwanadamu mwenye angeweza kulipia bei ya ukombozi kwa ajili ya uzima mukamilifu wenye Adamu alipoteza. Juu ya nini? Juu sisi wote hatukamilike. (Zaburi 49:7, 8) Bei ya ukombozi yenye ilipaswa kulipwa ilikuwa uzima mwingine mukamilifu wa kibinadamu. Njo maana inaitwa “bei ya ukombozi yenye kulingana.” (1 Timoteo 2:6) Bei ya ukombozi ilipaswa kuwa yenye kulingana na uzima mukamilifu wenye Adamu alipoteza.

10. Namna gani Yehova alitoa bei ya ukombozi?

10 Namna gani Yehova alitoa bei ya ukombozi? Yehova alituma mu dunia Mwana wake mwenye anapenda sana. Mwana ule, njo kiumbe chake cha kwanza. (1 Yohana 4:9, 10) Yesu alikuwa tayari kuacha Baba yake na kuacha makao yake ya mbinguni. (Wafilipi 2:7) Yehova alitosha uzima wa Yesu mbinguni, na kuuhamishia mu dunia. Wakati Yesu alizaliwa, alikuwa mwanadamu mukamilifu, hakukuwa na zambi.​—Luka 1:35.

Yehova alitoa mwana wake mwenye anapenda sana ili akuwe bei ya ukombozi kwa ajili yetu

11. Namna gani mutu mumoja angelipia wanadamu wote bei ya ukombozi?

11 Adamu, mutu wa kwanza, alipoteza uzima mukamilifu kwa ajili ya wanadamu wote, wakati alikosa kumutii Mungu. Je, mutu mwingine angeweza kutoshea wanadamu wote kifo? Ndiyo. (Soma Waroma 5:19.) Yesu, mwenye hakufanya zambi hata kidogo, alitoa uzima wake mukamilifu kuwa bei ya ukombozi. (1 Wakorinto 15:45) Uzima wake mukamilifu ungetumiwa ili kutoshea wanadamu wote kifo.​—1 Wakorinto 15:21, 22.

12. Juu ya nini iliomba Yesu ateseke sana?

12 Biblia inaeleza namna Yesu aliteseka sana mbele akufe. Alipigwa bila huruma, akapigiliwa misumari kwenye muti wa mateso, na alivumilia kifo cha polepole na chenye maumivu makali. (Yohana 19:1, 16-18, 30) Juu ya nini iliomba Yesu ateseke sana? Juu Shetani alisema kama hakuna mutu mwenye anaweza kubakia mushikamanifu kwa Mungu kama anajaribiwa sana. Yesu alionyesha kama mutu mukamilifu anaweza kuwa mushikamanifu kwa Mungu hata kama anateseka sana. Wazia namna Yehova alijivunia uaminifu wa Yesu!​—Mezali 27:11; ona Mafasirio Ingine ya 15.

13. Bei ya ukombozi ililipwa namna gani?

13 Bei ya ukombozi ililipwa namna gani? Yesu alipatia Baba yake bei ya uzima wake. Mu mwaka wa 33, tarehe 14 Mwezi wa Nisani wa kalenda ya Wayahudi, Yehova aliruhusu maadui wa Yesu wamuue. (Waebrania 10:10) Kisha siku tatu, Yehova alimufufua Yesu akiwa kiumbe wa roho, hakukuwa tena mwanadamu. Kisha, wakati Yesu alirudia mbinguni kwa Baba yake, alimutolea bei ya uzima wake mukamilifu wa kibinadamu kuwa bei ya ukombozi. (Waebrania 9:24) Sasa, juu bei ya ukombozi imelipwa, tunaweza kukombolewa kutoka katika zambi na kifo.​—Soma Waroma 3:23, 24.

FAIDA ZENYE BEI YA UKOMBOZI INAWEZA KUKULETEA

14, 15. Tunapaswa kufanya nini ili zambi zetu zisamehewe?

14 Zawadi kubwa zaidi ya Mungu inatuletea faida. Tuone basi faida zenye inatuletea leo na faida zenye itatuletea wakati wenye kuja.

15 Zambi zetu zinasamehewa. Haiko mwepesi kufanya mambo ya muzuri kila wakati. Tunafanyaka makosa, na wakati fulani tunasemaka jambo fulani la mubaya. (Wakolosai 1:13, 14) Tunapaswa kufanya nini kusudi tusamehewe? Tunapaswa kuhuzunika sana juu ya makosa yenye tumefanya. Na tunapaswa kuwa wanyenyekevu na kumuomba Yehova musamaha. Kama tunafanya vile, tunaweza kuwa hakika kama zambi zetu zitasamehewa.​—1 Yohana 1:8, 9.

16. Tunapaswa kufanya nini ili tukuwe na zamiri ya muzuri?

16 Tunaweza kuwa na zamiri ya muzuri. Kama zamiri yetu inatuambia kuwa tumefanya jambo fulani la mubaya, tunajihukumu, na pengine tunajisikia kuwa hatuna tumaini na tuko watu wa bure. Lakini hatupaswe kuvunjika moyo. Kama tunamulilia Yehova atusamehe, tunaweza kuwa hakika kama atatusikiliza na kutusamehe. (Waebrania 9:13, 14) Yehova anapenda tumuambie magumu yetu yote na uzaifu wetu wote. (Waebrania 4:14-16) Kama tunafanya vile, tunaweza kuwa na amani pamoja na Mungu.

17. Tunaweza kupata baraka gani juu Yesu alikufa kwa ajili yetu?

17 Tuko na tumaini la kuishi milele. “Mushahara wenye zambi inalipa ni kifo, lakini zawadi yenye Mungu anatoa ni uzima wa milele kupitia Kristo Yesu Bwana wetu.” (Waroma 6:23) Juu Yesu alikufa kwa ajili yetu, tunaweza kuishi milele na kuwa na afya kamilifu. (Ufunuo 21:3, 4) Lakini tunapaswa kufanya nini ili tupate baraka hizo?

UNAONA BEI YA UKOMBOZI KUWA YA MAANA?

18. Ni nini inaonyesha kama Yehova anatupenda?

18 Wazia namna unafurahi sana wakati mutu anakupatia zawadi fulani ya muzuri. Bei ya ukombozi njo zawadi ya maana zaidi kuliko zote, na tunapaswa kuwa wenye shukrani sana kwa Yehova kwa ajili ya zawadi hiyo. Andiko la Yohana 3:16 linatuambia kama “Mungu alipenda ulimwengu sana na hivyo akamutoa Mwana wake muzaliwa-pekee.” Kwa kweli, Yehova anatupenda sana njo maana alitutolea Yesu, Mwana wake mwenye anapenda sana. Na tunajua kama Yesu pia anatupenda, juu aliitika kufa kwa ajili yetu. (Yohana 15:13) Zawadi ya bei ya ukombozi inapaswa kukuhakikishia kama Yehova na Yesu wanakupenda kabisa.​—Wagalatia 2:20.

Wakati tunaendelea kujifunza juu ya Yehova, tutakuwa marafiki wake na tutamupenda zaidi

19, 20. (a) Unaweza kufanya nini ili ukuwe rafiki ya Yehova? (b) Namna gani unaweza kuonyesha kama unaamini bei ya ukombozi?

19 Sasa kwa sababu umejifunza juu ya upendo mukubwa zaidi wa Mungu, namna gani unaweza kuwa rafiki yake? Haiko mwepesi kupenda mutu mwenye haujue. Andiko la Yohana 17:3 linasema kama tunaweza kufikia kumujua Yehova. Wakati unaendelea kujifunza juu ya Yehova, utamupenda zaidi, utapenda kumufurahisha, na utakuwa rafiki yake. Kwa hiyo, uendelee kujifunza Biblia ili umujue Yehova muzuri.​—1 Yohana 5:3.

20 Ona bei ya ukombozi ya Yesu kuwa ya maana. Biblia inasema kama “ule mwenye anamuamini Mwana iko na uzima wa milele.” (Yohana 3:36) Kuamini Yesu maana yake nini? Maana yake ni kufanya mambo yenye Yesu alitufundisha. (Yohana 13:15) Tunapaswa kufanya jambo lingine zaidi ya kusema kama tunamuamini Yesu. Tunapaswa kuonyesha kupitia matendo yetu kama tunamuamini. Andiko la Yakobo 2:26 linasema hivi: “Imani bila matendo imekufa.”

21, 22. (a) Juu ya nini tunapaswa kuja ku Ukumbusho wa kifo cha Kristo kila mwaka? (b) Tutazungumuzia nini mu Sura ya 6 na ya 7?

21 Ukuje ku Ukumbusho wa kifo cha Kristo. Mangaribi mbele Yesu akufe, alitufundisha kama tunapaswa kukumbuka kifo chake. Tunafanya vile kila mwaka, na tukio hilo linaitwa Ukumbusho ao “Chakula cha Mangaribi cha Bwana.” (1 Wakorinto 11:20; Matayo 26:26-28) Yesu anapenda tukumbuke kama alitoa uzima wake mukamilifu kuwa bei ya ukombozi kwa ajili yetu. Alisema hivi: “Muendelee kufanya hivi kwa kunikumbuka mimi.” (Soma Luka 22:19.) Wakati unakuja kwenye Ukumbusho, unaonyesha kama unakumbuka bei ya ukombozi na unakumbuka kama Yehova na Yesu wanatupenda sana.​—Ona Mafasirio Ingine ya 16.

22 Bei ya ukombozi njo zawadi kubwa zaidi yenye tunaweza kupata. (2 Wakorinto 9:14, 15) Zawadi hiyo ya maana sana italetea faida hata mamilioni ya watu wenye wamekwisha kufa. Mu Sura ya 6 na ya 7, tutazungumuzia namna jambo hilo linawezekana.