Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 7

Kutakuwa Ufufuo!

Kutakuwa Ufufuo!

1-3. Sisi wote tuko wafungwa wa nini? Namna gani Yehova atatukomboa?

WAZIA unahukumiwa kufungwa mu gereza maisha yako yote juu ya kosa lenye haukufanya. Hauna hata tumaini la kufunguliwa. Hauna tena tumaini juu ya wakati wako wenye kuja, na hauwezi kufanya jambo lolote juu ya hali hiyo. Lakini, wakati umepoteza kabisa tumaini, unapata habari kama kuko mutu fulani mwenye kuwa na uwezo wa kukufungua na amesema kama atakusaidia! Utajisikia namna gani?

2 Sisi wote ni wafungwa wa kifo. Hata tufanye nini, hatuwezi kuponyoka kifo. Lakini, Yehova iko na uwezo wa kutukomboa kutoka katika kifo. Na amesema kama “adui wa mwisho mwenye ataharibiwa ni kifo.”​—1 Wakorinto 15:26.

3 Wazia namna utajisikia wakati watu hawatakufa tena! Lakini, zaidi ya kutosha kifo, Yehova atafanya jambo lingine. Atarudishia uzima wale wenye wamekufa. Wazia faida zenye jambo hilo litakuletea. Amesema kama wale wenye “hawana uwezo katika kifo” wataishi tena. (Isaya 26:19) Biblia inaita tukio hilo ufufuo.

WAKATI MUTU MWENYE TUNAPENDA ANAKUFA

4. (a) Ni nini inaweza kutufariji wakati mutu wa familia ao rafiki yetu anakufa? (b) Taja majina fulani ya marafiki wa sana wa Yesu.

4 Wakati mutu wa familia yetu, ao rafiki yetu wa sana anakufa, tunasikia huzuni sana na tunavunjika moyo kabisa. Hakuna kitu chenye tunaweza kufanya ili kurudishia mutu huyo uzima. Lakini, Biblia inatupatia faraja ao kitulizo cha kweli. (Soma 2 Wakorinto 1:3, 4.) Tuzungumuzie mufano wenye kuonyesha kama Yehova na Yesu wanapenda kabisa kufufua watu wenye tunapenda wenye wamekufa. Wakati Yesu alikuwa mu dunia, mara nyingi alitembelea Lazaro na dada zake Marta na Maria. Wote tatu walikuwa marafiki wa sana wa Yesu. Biblia inasema hivi: “Yesu alimupenda Marta na dada yake, na Lazaro.” Kisha, siku moja Lazaro akakufa.​—Yohana 11:3-5.

5, 6. (a) Yesu alifanya nini wakati aliona huzuni ya watu wa familia ya Lazaro na marafiki wake? (b) Juu ya nini inafariji kujua kama Yesu alisikia huzuni wakati Lazaro alikufa?

5 Yesu alienda kufariji Marta na Maria. Wakati Marta alisikia kama Yesu alikuwa anakuja, alienda inje ya muji ili kukutana naye. Alifurahi kumuona Yesu, lakini alimuambia hivi: “Kama ungekuwa hapa, ndugu yangu hangekufa.” Marta aliwaza kama Yesu amechelewa. Kisha pale, Yesu alimuona Maria, dada ya Marta, iko analia. Wakati aliona huzuni yao, alihuzunika sana na akalia. (Yohana 11:21, 33, 35) Alisikia maumivu ya mingi sana yenye tunasikiaka wakati mutu mwenye tunapenda anakufa.

6 Inafariji kujua kama Yesu alihuzunika sana. Hilo linaonyesha kama anachukia kifo. Na Yesu iko na sifa kama za Baba yake. (Yohana 14:9) Yehova iko na uwezo wa kutosha kifo milele na atafanya vile hivi karibuni.

“LAZARO, KUJA HUKU INJE!”

7, 8. Juu ya nini Marta hakupenda watoshe jiwe ku kaburi la Lazaro? Lakini Yesu alifanya nini?

7 Wakati Yesu alifika ku kaburi kwenye mwili wa Lazaro ulikuwa umewekwa, kaburi lilikuwa limefunikwa na jiwe kubwa. Yesu alisema hivi: “Mutoshe lile jiwe.” Lakini Marta hakupenda watoshe jiwe hilo. Mwili wa Lazaro ulikuwa umefanya siku ine mu kaburi. (Yohana 11:39) Hakujua jambo lenye Yesu alikuwa karibu kufanya ili kusaidia ndugu yake.

Wazia furaha yenye watu wa familia ya Lazaro na marafiki wake walikuwa nayo wakati alifufuliwa!​—Yohana 11:38-44

8 Yesu aliambia Lazaro hivi: “Kuja huku inje!” Jambo lenye Marta na Maria waliona kisha pale lilikuwa la kushangaza sana. “Mutu huyo mwenye alikuwa amekufa akatoka inje, miguu na mikono yake ilikuwa imefungwa kwa vitambaa.” (Yohana 11:43, 44) Yesu alikuwa amemurudishia Lazaro uzima! Alijiunga tena na watu wa familia yake na marafiki wake. Wangeweza kumukumbatia, kumugusa, na kuzungumuza naye. Huo ulikuwa muujiza wa ajabu! Yesu alikuwa amemufufua Lazaro.

“MUTOTO MWANAMUKE, NINAKUAMBIA, SIMAMA!”

9, 10. (a) Ni nani mwenye alipatia Yesu nguvu ya kufufua watu? (b) Juu ya nini habari zenye kuzungumuzia ufufuo ni za maana sana kwetu?

9 Yesu alifufua watu kwa nguvu yake mwenyewe? Hapana. Mbele amufufue Lazaro, Yesu alisali kwa Yehova, na Yehova alimupatia nguvu ya kumufufua Lazaro. (Soma Yohana 11:41, 42.) Haiko Lazaro tu njo alifufuliwa. Biblia inazungumuzia mutoto mwanamuke wa miaka 12 mwenye alikuwa mugonjwa sana. Yairo, baba yake, alikuwa amepoteza tumaini, na alimuomba sana Yesu aponyeshe mutoto wake. Alikuwa na ule mutoto mumoja tu. Wakati alikuwa anazungumuza na Yesu, wanaume fulani walikuja kwenye alikuwa na kumuambia hivi: “Binti yako amekufa! Sababu gani uendelee kumusumbua [kumuuzi] Mwalimu?” Lakini Yesu akamuambia hivi: “Usiogope, ukuwe tu na imani, na ataokolewa.” Kisha Yesu akaenda kwa Yairo pamoja naye. Wakati walikaribia ku nyumba ya Yairo, Yesu aliona na kusikia watu wako wanalia. Yesu aliwaambia hivi: “Muache kulia, kwa maana hakukufa lakini analala usingizi.” Pengine baba na mama yake walijiuliza ikiwa Yesu alipenda kusema nini. Yesu aliomba kila mutu atoke inje, kisha akaingia pamoja na baba na mama yake mu chumba kwenye mutoto huyo alikuwa amewekwa. Yesu akakamata mukono wake na kumuambia hivi: “Mutoto mwanamuke, ninakuambia, simama!” Wazia furaha yenye wazazi wake walikuwa nayo wakati aliamuka mara moja na kuanza kutembea. Yesu alikuwa amemufufua mutoto wao mwanamuke. (Marko 5:22-24, 35-42; Luka 8:49-56) Kuanzia siku hiyo, wakati walikuwa wanaona mutoto wao mwanamuke, walikuwa wanakumbuka mambo yenye Yehova alikuwa amewafanyia kupitia Yesu. *

10 Wale wenye Yesu alifufua walifikia kufa tena. Lakini mambo yenye tunajifunza juu ya watu hao ni ya maana, yanatupatia tumaini la kweli. Yehova anapenda kufufua watu na atafanya vile.

HABARI JUU YA UFUFUO ZINATUFUNDISHA NINI?

Mutume Petro alimufufua mwanamuke Mukristo Dorkasi.​—Matendo 9:36-42

Eliya alimufufua mutoto mwanaume wa mujane.​—1 Wafalme 17:17-24

11. Andiko la Muhubiri 9:5 linatufundisha nini juu ya Lazaro?

11 Biblia inasema waziwazi kama “wafu hawajue kitu chochote.” Habari juu ya ufufuo wa Lazaro inaonyesha kama jambo hilo ni kweli. (Muhubiri 9:5) Kama vile tu Yesu alisema, ilikuwa kama vile Lazaro alikuwa analala usingizi. (Yohana 11:11) Wakati Lazaro alikuwa mu kaburi, hakujua “kitu chochote.”

12. Ni nini inaonyesha kama Lazaro alifufuliwa kabisa?

12 Wakati Yesu alimufufua Lazaro, watu wengi waliona. Hata maadui wa Yesu walijua kama alikuwa amefanya muujiza huo. Lazaro alikuwa muzima, na hilo lilionyesha kama ufufuo ulifanyika kabisa. (Yohana 11:47) Tena, watu wengi walienda kumuona Lazaro. Kwa hiyo, wakaanza kuamini kama Yesu alikuwa ametumwa na Mungu. Maadui wa Yesu hawakufurahia jambo hilo, kwa hiyo walipanga kumuua Yesu na Lazaro.​—Yohana 11:53; 12:9-11.

13. Juu ya nini tunaamini kabisa kama Yehova atafufua watu wenye wamekufa?

13 Yesu alisema kama “wale wote wenye kuwa katika makaburi ya ukumbusho” watafufuliwa. (Yohana 5:28) Maana yake wale wote wenye Yehova anakumbuka wataishi tena. Lakini ili Yehova afufue mutu fulani, anapaswa kukumbuka kila kitu juu ya mutu huyo. Anaweza kabisa kukumbuka? Kuko mamiliare ya nyota mu ulimwengu. Biblia inasema kama Yehova anajua jina la kila nyota. (Soma Isaya 40:26.) Kama anaweza kukumbuka jina la kila nyota, kwa kweli ni mwepesi kwake kukumbuka kila kitu juu ya wale wenye atarudishia uzima. Na jambo la maana zaidi ni hili: Yehova njo aliumba kila kitu; kwa hiyo tunajua kama iko na nguvu ya kufufua watu.

14, 15. Maneno ya Yobu yanatufundisha nini juu ya ufufuo?

14 Yobu, mwanaume muaminifu, aliamini kama kutakuwa ufufuo. Aliuliza hivi: “Kama mutu anakufa, je, anaweza kuishi tena?” Kisha akamuambia Yehova hivi: “Utaita, na mimi nitakujibu. Utatamani sana kazi ya mikono yako.” Ndiyo, Yobu alijua kama Yehova anangojea kwa hamu wakati wenye atafufua watu wenye wamekufa.​—Yobu 14:13-15.

15 Unajisikia namna gani wakati unawaza juu ya tumaini la ufufuo? Pengine unajiuliza hivi: ‘Watu wa familia yangu na marafiki wangu wenye wamekufa, nao pia watafufuliwa?’ Kujua kama Yehova anapenda kabisa kufufua watu wenye wamekufa, kunatufariji. Tuone sasa mambo yenye Biblia inasema juu ya mahali kwenye wataishi na ni nani watafufuliwa.

“WATASIKIA SAUTI YAKE NA WATATOKA”

16. Wale wenye watafufuliwa ili kuishi mu dunia watakuwa na maisha ya namna gani?

16 Zamani, wale wenye walifufuliwa waliungana tena na watu wa familia zao na marafiki wao hapa ku dunia. Ni vile mambo yatakuwa pia wakati wenye kuja, lakini mambo yatakuwa muzuri zaidi. Juu ya nini? Juu wale wenye watafufuliwa mu dunia watakuwa na tumaini la kuishi milele na hawatakufaka tena. Na wataishi mu dunia yenye kuwa tofauti kabisa na dunia yenye tunaishi ndani leo. Hakutakuwa tena vita, magonjwa, na kuumizana ao kuuana.

17. Ni nani watafufuliwa?

17 Ni nani watafufuliwa? Yesu alisema kama “wale wote wenye kuwa katika makaburi ya ukumbusho watasikia sauti yake na watatoka.” (Yohana 5:28, 29) Na andiko la Ufunuo 20:13 linasema hivi: “Bahari ikatoa wafu wenye walikuwa ndani yake, na kifo na Kaburi vikatoa wafu wenye walikuwa ndani yavyo.” Ndiyo, watu wengi sana wataishi tena. Mutume Paulo alisema pia kama “wenye haki na wenye hawako wenye haki” watafufuliwa. (Soma Matendo 24:15.) Maana yake nini?

Mu Paradiso, watu wenye wamekufa watafufuliwa na kuwa tena pamoja na wapendwa wao

18. “Wenye haki” wenye watafufuliwa ni nani?

18 Kati ya “wenye haki” kuko watumishi wa Yehova waaminifu wenye waliishi mbele Yesu akuje mu dunia. Watu kama vile, Noa, Abrahamu, Sara, Musa, Rutu, na Esta watafufuliwa ili waishi hapa ku dunia. Unaweza kusoma habari juu ya wamoja kati ya wanaume na wanamuke hao mu sura ya 11 ya kitabu cha Waebrania. Watumishi wa Yehova waaminifu wenye wanakufa leo, nao watafufuliwa? Ndiyo, nao ni “wenye haki,” kwa hiyo watafufuliwa.

19. “Wenye hawako wenye haki” ni nani? Yehova atawapatia nafasi gani?

19 Kati ya “wenye hawako wenye haki” kuko watu wengi sana wenye hawakupata nafasi ya kumujua Yehova. Hata kama walikufa, Yehova angali anawakumbuka. Atawafufua, na kuwapatia nafasi ya kujifunza juu yake na kumutumikia.

20. Ni nani wenye hawatafufuliwa?

20 Ni kusema kama kila mutu mwenye amekufa atafufuliwa? Hapana. Yesu alisema kama watu fulani hawatafufuliwa. (Luka 12:5) Ni nani mwenye ataamua kama mutu fulani atafufuliwa ao hapana? Yehova njo Muamuzi mukubwa zaidi, lakini amemupatia pia Yesu mamlaka ya “kuwa muamuzi wa wazima na wafu.” (Matendo 10:42) Kila mutu mwenye Yehova atahukumu kuwa muovu na hapendi kubadilika hatafufuliwa.​—Ona Mafasirio Ingine ya 19.

UFUFUO WA WATU WENYE WATAISHI MBINGUNI

21, 22. (a) Wale wenye wanafufuliwa ili waende mbinguni wanapewa mwili wa namna gani? (b) Ni nani alikuwa mutu wa kwanza kufufuliwa ili aende kuishi mbinguni?

21 Tena, Biblia inatuambia kama watu fulani watafufuliwa ili waende kuishi mbinguni. Wakati mutu anafufuliwa ili kuenda mbinguni, hafufuliwe katika mwili wa mwanadamu. Anafufuliwa na mwili wa roho, ni kusema, mwili kama wa malaika.

22 Yesu njo alikuwa mutu wa kwanza kufufuliwa ili kuishi mbinguni. (Yohana 3:13) Siku tatu kisha Yesu kuuawa, Yehova alimufufua. (Zaburi 16:10; Matendo 13:34, 35) Wakati Yesu alifufuliwa, hakukuwa na mwili wa mwanadamu. Mutume Petro alisema kama Yesu “aliuawa katika mwili lakini akafanywa kuwa muzima katika roho.” (1 Petro 3:18) Kwa hiyo, Yesu alifufuliwa na kuwa malaika mwenye nguvu! (1 Wakorinto 15:3-6) Lakini Biblia inasema kama kuko watu wengine wenye wangefufuliwa ili waishi mbinguni.

23, 24. (a) Ni nani wenye kuwa katika “kundi ndogo” lenye Yesu alizungumuzia? (b) Ni watu ngapi?

23 Mbele Yesu akufe, aliambia wanafunzi wake waaminifu hivi: “Ninaenda kuwatayarishia ninyi nafasi.” (Yohana 14:2) Hilo linaonyesha kama wanafunzi wake fulani wangefufuliwa ili waishi pamoja naye mbinguni. Wangekuwa wangapi? Yesu alisema kama wangekuwa watu kidogo, ni kusema, “kundi ndogo.” (Luka 12:32) Mutume Yohana alionyesha hesabu ya watu hao: aliona Yesu “amesimama juu ya Mulima Sayuni [mbinguni], na pamoja naye watu elfu mia moja makumi ine na ine (144 000).”​—Ufunuo 14:1.

24 Wale Wakristo 144 000 wangefufuliwa wakati gani? Biblia inatuambia kama wangeanza kufufuliwa kisha Kristo kuanza kutawala mbinguni. (1 Wakorinto 15:23) Tunaishi wakati huo, na wengi kati ya wale 144 000 wamekwisha kufufuliwa na kuenda mbinguni. Wale wenye wangali mu dunia na wenye wanakufa wakati wetu, wanafufuliwa mara moja na kuenda mbinguni. Lakini watu wengi zaidi watafufuliwa wakati wenye kuja ili waishi mu dunia Paradiso.

25. Tutajifunza nini mu habari yenye kufuata?

25 Hivi karibuni, Yehova atakomboa wanadamu kutoka katika kifo, na kifo hakitakuwa tena hata kidogo! (Soma Isaya 25:8.) Lakini wale wenye wanaenda mbinguni watafanya nini kule? Biblia inasema kama watatawala pamoja na Yesu mu Ufalme. Tutajifunza mambo mengi zaidi juu ya Ufalme huo mu habari yenye kufuata.

^ fu. 9 Mu Biblia, kuko habari zingine zenye kuzungumuzia ufufuo wa vijana na watu wazima, wanaume na wanamuke, Waisraeli na wenye hawako Waisraeli. Unaweza kusoma juu ya habari hizo mu 1 Wafalme 17:17-24; 2 Wafalme 4:32-37; 13:20, 21; Matayo 28:5-7; Luka 7:11-17; 8:40-56; Matendo 9:36-42; 20:7-12.