Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 9

Mwisho wa Dunia Uko Karibu?

Mwisho wa Dunia Uko Karibu?

1. Ni nani mwenye anaweza kutusaidia kujua mambo ya wakati wenye kuja?

UMESIKILIZA habari siku moja na kujiuliza hivi: ‘Juu ya nini mambo yanaendelea kuharibika zaidi?’ Kuko mambo mingi sana ya mubaya na mateso mingi sana, kwa hiyo watu fulani wanaamini kama mwisho wa dunia uko karibu. Ni kweli? Inawezekana kujua mambo yenye yatatokea wakati wenye kuja? Ndiyo. Watu hawawezi kujua mbele ya wakati mambo yenye yatatokea wakati wenye kuja, lakini Yehova anaweza kujua. Kupitia Biblia anatuambia juu ya wakati wetu wenye kuja na juu ya wakati wenye kuja wa dunia.​—Isaya 46:10; Yakobo 4:14.

2, 3. Wanafunzi wa Yesu walipenda kujua nini? Yesu aliwajibu namna gani?

2 Wakati Biblia inazungumuzia mwisho wa dunia, haiko kuharibiwa kwa dunia hii, lakini mwisho wa mambo ya mubaya. Yesu alifundisha watu kama Ufalme wa Mungu utatawala dunia. (Luka 4:43) Wanafunzi wake walipenda kujua ni wakati gani Ufalme wa Mungu ungekuja, kwa hiyo walimuuliza ulizo hili: “Mambo haya yatakuwa wakati gani, na ni nini itakuwa alama ya kuwapo kwako na ya umalizio wa mupangilio wa mambo?” (Matayo 24:3) Yesu hakuwapatia tarehe yenye mwisho wa dunia ungekuja, lakini aliwaambia mambo yenye yangetokea mbele mwisho wa dunia ufike. Na mambo hayo yenye Yesu alisema yanatokea leo.

3 Mu sura hii tutazungumuzia mambo yenye kuonyesha kabisa kama tunaishi mu siku za mwisho. Kwanza, tunapaswa kujifunza juu ya vita fulani yenye ilitokea mbinguni ili tuelewe juu ya nini hali iko mubaya sana mu dunia.

VITA MBINGUNI

4, 5. (a) Kisha tu Yesu kuwa Mufalme, ni nini ilitokea mbinguni? (b) Andiko la Ufunuo 12:12 linasema ni mambo gani yangetokea kisha Shetani kutupwa ku dunia?

4 Mu Sura ya 8 tulijifunza kama Yesu alifanywa kuwa Mufalme mu mwaka wa 1914. (Danieli 7:13, 14) Kitabu cha Ufunuo kinatuambia mambo yenye yalitokea. Kinasema hivi: “Vita ikatokea mbinguni: Mikaeli [ni kusema, Yesu] na malaika wake wakapigana na ule nyoka mukubwa [Shetani], na ule nyoka mukubwa na malaika wake wakapigana.” * Shetani na pepo wake wachafu walishindwa katika vita hiyo na wakatupwa chini ku dunia. Wazia furaha yenye malaika walikuwa nayo! Lakini ni mambo gani yenye yangepata wanadamu mu dunia? Biblia inasema kama huo ungekuwa wakati wa magumu kwa wanadamu. Juu ya nini? Juu Ibilisi iko na kasirani sana, “akijua kwamba iko na kipindi kifupi cha wakati.”​—Ufunuo 12:7, 9, 12.

5 Ibilisi anajikaza sana kuleta mateso mingi mu dunia. Iko na kasirani sana juu anajua kama anabakia na wakati mufupi mbele Mungu amuharibu. Tuzungumuzie basi mambo yenye Yesu alisema kama yangetokea mu siku za mwisho.​—Ona Mafasirio Ingine ya 24.

SIKU ZA MWISHO

6, 7. Ni nini inaonyesha kama mambo yenye Yesu alisema juu ya vita na njaa yanatimia leo?

6 Vita. Yesu alisema hivi: “Taifa litasimama kupigana na taifa na ufalme kupigana na ufalme.” (Matayo 24:7) Watu wengi wameuawa katika vita wakati wetu kuliko wakati mwingine wote mu historia. Ripoti moja kutoka kwenye shirika fulani lenye kutafuta habari (Worldwatch Institute) inaonyesha kama kuanzia mwaka wa 1914, vita imeua watu zaidi ya milioni 100. Hesabu ya watu wenye wamekufa mu miaka 100 yenye imepita, ni kusema kati ya mwaka wa 1900 na 2000, inapita mara tatu hesabu ya watu wenye walikufa mu vita katika miaka 1 900 mbele ya pale. Mamilioni ya watu wameteseka sana juu ya vita!

7 Njaa. Yesu alisema hivi: “Kutakuwa upungufu wa chakula.” (Matayo 24:7) Hata kama leo wanadamu wanakomalisha chakula mingi kuliko zamani, watu wengi hawapate chakula cha kutosha ao cha kuenea. Juu ya nini? Juu hawana feza za kutosha za kuuza chakula ao hawana mashamba kwenye wanaweza kukomalisha chakula. Watu zaidi ya miliare moja wako maskini sana. Shirika la Afya Ulimwenguni linasema kama mamilioni ya watoto wanagonjwa na kufa kila mwaka juu wanakosa chakula cha kutosha.

8, 9. Ni nini inaonyesha kama mambo yenye Yesu alisema juu ya matetemeko ya inchi na magonjwa yanatimia leo?

8 Matetemeko ya Inchi. Yesu alitabiri hivi: “Kutakuwa matetemeko makubwa ya inchi.” (Luka 21:11) Kila mwaka kunatokea matetemeko makubwa ya inchi. Kuanzia mwaka wa 1900, watu zaidi ya milioni mbili wamekufa juu ya matetemeko ya inchi. Na hata kama teknolojia imesaidia watu kujua mbele ya wakati kama matetemeko yatatokea, watu wengi wanaendelea kufa juu ya matetemeko hayo.

9 Magonjwa. Yesu alitabiri kama kutakuwa “magonjwa ya kuambukiza.” Magonjwa hatari yangeenea haraka sana na kuua watu wengi. (Luka 21:11) Hata kama wanganga wamejifunza namna ya kutunza magonjwa mingi, kuko magonjwa fulani yenye haina dawa. Ripoti moja inasema kama kila mwaka, mamilioni ya watu wanakufa juu ya magonjwa kama vile kifua kikuu (tuberculose), malaria, na kolera. Zaidi ya hilo, wanganga wamevumbua magonjwa ingine ya mupya 30, na magonjwa fulani kati ya magonjwa hayo haina dawa.

TABIA ZA WATU WA SIKU ZA MWISHO

10. Namna gani andiko la 2 Timoteo 3:1-5 linatimia leo?

10 Mu andiko la 2 Timoteo 3:1-5, Biblia inasema hivi: “Katika siku za mwisho kutakuwa nyakati za hatari zenye kuwa ngumu kuvumilia.” Mutume Paulo alionyesha tabia zenye watu wangekuwa nazo mu siku za mwisho. Alisema kama watu wangekuwa

  • wenye kujipenda wenyewe

  • wenye kupenda feza

  • wenye hawatii ao kusikia wazazi wao

  • wenye hawana ushikamanifu

  • wenye hawapendi watu wa familia yao

  • wenye hawajizuie

  • wenye jeuri na wakali

  • wenye kupenda raha kuliko Mungu

  • wenye kwa inje wanaonekana kuwa wanamupenda Mungu lakini wanakataa kumutii

11. Andiko la Zaburi 92:7, linasema kama watu wabaya watapatwa na nini?

11 Watu wengi wako na tabia hizo mahali kwenye unaishi? Mu dunia yote, watu wengi wako na tabia hizo. Lakini karibuni Mungu atafanya jambo fulani. Anatoa ahadi (malako) hii: “Wakati waovu wanachipuka kama magugu na wakati wakosaji wote wanasitawi, ni ili waharibiwe milele.”​—Zaburi 92:7.

HABARI NJEMA MU SIKU ZA MWISHO

12, 13. Mu siku za mwisho, Yehova ametusaidia kuelewa mafundisho gani?

12 Biblia ilitabiri kama mu siku za mwisho, mambo mingi yenye kuleta huzuni na mateso yangejaa mu dunia. Lakini Biblia inasema pia kama mambo ya muzuri yangetokea.

“Hii habari njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia yote yenye kuikaliwa na watu.”​—Matayo 24:14

13 Kuelewa muzuri mafundisho ya Biblia. Nabii Danieli aliandika juu ya siku za mwisho. Alisema hivi: “Ujuzi wa kweli utakuwa mwingi.” (Danieli 12:4) Mungu angesaidia watu wake kuelewa muzuri zaidi mafundisho ya Biblia kupita zamani. Yehova amefanya vile zaidi sana kuanzia mwaka wa 1914. Kwa mufano, ametusaidia kuelewa kama jina lake ni la maana sana, kuelewa kusudi lake juu ya dunia, na pia kweli juu ya bei ya ukombozi, juu ya hali ya watu wenye wamekufa, na ufufuo. Tumejifunza kama Ufalme wa Mungu njo tu unaweza kumaliza mateso yetu yote. Tena, tumejifunza namna tunaweza kuwa na furaha na namna ya kuishi maisha yenye kumupendeza Mungu. Lakini, namna gani watumishi wa Mungu wanatumikisha mambo yenye wamejifunza? Unabii mwingine unatupatia jibu.​—Ona Mafasirio Ingine ya 21 na ya 25.

14. Habari njema ya Ufalme inahubiriwa wapi? Na ni nani wanahubiri habari hiyo?

14 Kazi ya kuhubiri mu dunia yote. Yesu alisema hivi juu ya kazi ya kuhubiri mu siku za mwisho: “Hii habari njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia yote yenye kuikaliwa na watu.” (Matayo 24:3, 14) Habari njema juu ya ufalme inahubiriwa mu inchi 240 na mu luga zaidi ya 900. Mu dunia yote, Mashahidi wa Yehova kutoka katika “mataifa yote na makabila” wanasaidia watu kuelewa Ufalme wa Mungu ni nini na mambo yenye Ufalme huo utafanyia watu. (Ufunuo 7:9) Na wanafanya vile bila kulipisha watu feza. Hata kama watu wengi wanawachukia na kuwatesa, hakuna kitu chenye kinaweza kuzuia kazi ya kuhubiri, kama vile tu Yesu alitabiri.​—Luka 21:17.

UTAFANYA NINI?

15. (a) Unaamini kama tunaishi mu siku za mwisho? Juu ya nini? (b) Wale wenye kumutii Yehova wataona nini? Wale wenye hawamutii Yehova watapatwa na nini?

15 Unaamini kama tunaishi mu siku za mwisho? Mambo mingi yenye Biblia ilitabiri juu ya siku za mwisho yanatimia. Karibuni Yehova atasimamisha kazi ya kuhubiri habari njema na “ule mwisho” utakuja. (Matayo 24:14) Ule mwisho ni nini? Mwisho ni vita ya Armagedoni, wakati Mungu ataharibu watu wabaya. Yehova atatumia Yesu na malaika wake wenye nguvu ili kuharibu kila mutu mwenye anakataa kumutii yeye na Mwana wake. (2 Watesalonike 1:6-9) Kisha pale, Shetani na pepo wake wachafu hawatadanganya tena watu. Na wale wote wenye wanapenda kumutii Mungu na kukubali Ufalme wake wataona namna ahadi zake zote zitatimia.​—Ufunuo 20:1-3; 21:3-5.

16. Kwa sababu ule mwisho uko karibu sana, unapaswa kufanya nini?

16 Mwisho wa ulimwengu huu wenye kutawaliwa na Shetani unakaribia. Kwa hiyo, ni jambo la maana sana tujiulize hivi: ‘Ninapaswa kufanya nini?’ Yehova anataka ujifunze mambo mingi katika Biblia. Unapaswa kujifunza Biblia kwa bidii. (Yohana 17:3) Mashahidi wa Yehova wanafanya mikutano kila juma ili wasaidie watu kuelewa Biblia. Ujikaze kuenda ku mikutano hiyo kila mara. (Soma Waebrania 10:24, 25.) Ukijifunza kama unapaswa kufanya mabadiliko, usiogope. Ufanye mabadiliko hayo na urafiki wako pamoja na Yehova utakuwa wenye nguvu zaidi.​—Yakobo 4:8.

17. Juu ya nini watu wengi watashituka wakati mwisho utakuja?

17 Mutume Paulo alifasiria kama uharibifu wa watu wabaya utakuja wakati wenye watu wengi hawawazie, kama “vile mwizi anakuja usiku.” (1 Watesalonike 5:2) Yesu alitabiri kama watu wengi watakataa kuona mambo yenye kuonyesha kabisa kama tunaishi mu siku za mwisho. Alisema hivi: “Kama vile siku za Noa zilikuwa, ni vile kuwapo kwa Mwana wa binadamu [ao, siku za mwisho] kutakuwa. Kwa maana kama vile walikuwa katika siku hizo mbele ya Garika, walikuwa wanakula na kunywa, wanaume walikuwa wanaoa na wanamuke walikuwa wanaolewa, mupaka siku ile Noa aliingia ndani ya safina, na hawakuhangaika mupaka Garika ikakuja na kuwaharibu wote, ni vile kuwapo kwa Mwana wa binadamu kutakuwa.”​—Matayo 24:37-39.

18. Yesu alitupatia angalisho gani?

18 Yesu alitupatia onyo ao angalisho kama hatupaswe kukengeushwa “na kula kupita kiasi na kunywa sana na mahangaiko ya maisha.” Alisema kama mwisho utakuja kwa kushitukia, “kama mutego.” Tena, alisema kama ‘utakuja juu ya wale wote wenye kuishi juu ya uso wa dunia yote.’ Kisha aliongeza hivi: “Muendelee kukesha, mukimulilia Mungu [ao kusali kwa moyo wote] kila wakati ili muweze kuponyoka mambo haya yote yenye yanapaswa kutokea na kusimama mbele ya Mwana wa binadamu.” (Luka 21:34-36) Juu ya nini ni jambo la maana kutii onyo la Yesu? Juu hivi karibuni ulimwengu mubaya wa Shetani utaharibiwa. Wale tu wenye kukubaliwa na Yehova na Yesu njo wataokoka mwisho wa dunia na kuishi milele mu dunia mupya.​—Yohana 3:16; 2 Petro 3:13.

^ fu. 4 Mikaeli ni jina lingine la Yesu Kristo. Ili kupata habari zaidi, ona Mafasirio Ingine ya 23.