Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 14

Familia Yako Inaweza Kuwa na Furaha

Familia Yako Inaweza Kuwa na Furaha

1, 2. Yehova anataka familia zikuwe na maisha ya namna gani?

YEHOVA MUNGU njo alianzisha ndoa ya kwanza. Biblia inasema kama alimufanya mwanamuke wa kwanza na “akamuleta kwa ule mwanaume.” Adamu alifurahi sana, kwa hiyo, akasema hivi: “Mwishowe huyu ni mufupa wa mifupa yangu na nyama ya nyama yangu.” (Mwanzo 2:22, 23) Hilo linaonyesha kama Yehova anapenda bibi na bwana wakuwe na furaha.

2 Jambo la kuhuzunisha ni hili: watu wengi hawana furaha hata kidogo mu maisha ya familia. Lakini, Biblia iko na kanuni za mingi zenye zinaweza kusaidia watu wote wa familia waishi pamoja kwa furaha.​—Luka 11:28.

MUNGU ANAOMBA BWANA AFANYE NINI?

3, 4. (a) Namna gani bwana anapaswa kumutendea bibi yake? (b) Juu ya nini ni jambo la maana bibi na bwana wakuwe tayari kusameheana?

3 Biblia inasema kama bwana muzuri anapaswa kumutendea bibi yake kwa upendo na heshima. Unaweza kusoma Waefeso 5:25-29. Sikuzote, bwana anapaswa kumutendea bibi yake kwa upendo. Tena, anapaswa kumulinda, kumuhangaikia, na hapaswe kumutendea mubaya hata kidogo.

4 Lakini bwana anapaswa kufanya nini wakati bibi yake anafanya makosa? Biblia inaambia bwana hivi: “Muendelee kupenda bibi zenu na musiwakasirikie kwa uchungu.” (Wakolosai 3:19) Bwana, ukumbuke kama na wewe unafanyaka makosa. Na kama unapenda Mungu akusamehe, na wewe unapaswa kumusamehe bibi yako. (Matayo 6:12, 14, 15) Wakati bibi na bwana wako tayari kusameheana, hilo litawasaidia wakuwe na ndoa yenye furaha.

5. Juu ya nini bwana anapaswa kumuheshimia bibi yake?

5 Yehova anapenda bwana amuheshimie bibi yake. Bwana anapaswa kufikiria sana mambo yenye bibi yake iko nayo lazima. Ni jambo la maana sana kufanya vile. Kama bwana hamutendee bibi yake muzuri, Yehova anaweza kukataa kusikiliza sala zake. (1 Petro 3:7) Yehova anaona watu wote wenye kumupenda kuwa wa maana. Haone wanaume kuwa watu wa maana kupita wanamuke.

6. Bibi na bwana ni “mwili mumoja.” Maana yake nini?

6 Yesu alionyesha kama bibi na bwana “hawako wawili tena, lakini mwili mumoja.” (Matayo 19:6) Kila mumoja anapaswa kuwa muaminifu kwa mwenzake. (Mezali 5:15-21; Waebrania 13:4) Na kila mumoja anapaswa kuwa tayari kutimizia mwenzake mahitaji ya kitendo cha ndoa. (1 Wakorinto 7:3-5) Bwana anapaswa kukumbuka kama “hakuna mutu mwenye anachukia mwili wake; lakini anaukulisha na kuutunza kwa upendo.” Njo maana anapaswa kumupenda bibi yake na kumutunza. Na zaidi sana, bibi anataka bwana yake amutendee muzuri na kumupenda.​—Waefeso 5:29.

MUNGU ANAOMBA BIBI AFANYE NINI?

7. Juu ya nini familia iko na lazima ya kichwa?

7 Kila familia iko na lazima ya kichwa, ni kusema, mutu fulani mwenye kuongoza familia ili waishi muzuri pamoja. Mu 1 Wakorinto 11:3, Biblia inasema hivi: “Kichwa cha kila mwanaume ni Kristo; na kichwa cha mwanamuke ni mwanaume; na kichwa cha Kristo ni Mungu.”

8. Namna gani bibi anaweza kumuonyesha bwana yake heshima kubwa?

8 Kila bwana anafanyaka makosa. Lakini, wakati bibi anaitika maamuzi ya bwana yake na kumuunga mukono, familia yote inapata faida. (1 Petro 3:1-6) Biblia inasema hivi: “Bibi anapaswa kumuheshimia sana bwana yake.” (Waefeso 5:33) Tuseme nini ikiwa bwana hana imani moja na bibi yake? Anapaswa tu kumuheshimia sana. Biblia inasema hivi: “Ninyi bibi, mujitiishe kwa bwana zenu, ili kama kuko wale wenye hawatii lile neno, wavutwe bila neno kupitia mwenendo wa bibi zao, kwa sababu wameshuhudia kwa macho yao mwenendo wenu wenye kuwa safi pamoja na heshima kubwa.” (1 Petro 3:1, 2) Mufano muzuri wa bibi unaweza kusaidia bwana yake aelewe na kuheshimia imani yake.

9. (a) Bibi anapaswa kufanya nini kama haitike mawazo ya bwana yake? (b) Andiko la Tito 2:4, 5 linatolea bibi mashauri gani?

9 Bibi anapaswa kufanya nini kama haitike mawazo ya bwana yake? Anapaswa kueleza mawazo yake kwa heshima. Kwa mufano, Sara alisema jambo fulani lenye Abrahamu hakufurahia, lakini Yehova alimuambia hivi: “Umusikilize.” (Mwanzo 21:9-12) Bibi anapaswa kuunga mukono maamuzi yote ya bwana yake, kama hayapinge mambo yenye Biblia inasema. (Matendo 5:29; Waefeso 5:24) Bibi muzuri anahangaikia familia yake. (Soma Tito 2:4, 5.) Wakati bwana yake na watoto wake wanaona namna anatumika kwa bidii juu yao, watamupenda na kumuheshimia hata zaidi.​—Mezali 31:10, 28.

Juu ya nini Sara ni mufano muzuri wenye bibi wanapaswa kufuata?

10. Biblia inasema nini juu ya kutengana na kuvunja ndoa?

10 Wakati fulani bibi na bwana wanaamua haraka kutengana ao kuvunja ndoa yao. Lakini, Biblia inasema kama “bibi asitengane na bwana yake” na “bwana asimuache bibi yake.” (1 Wakorinto 7:10, 11) Kuko magumu fulani makubwa yenye yanaweza kufanya bibi na bwana watengane, lakini huo ni uamuzi muzito. Biblia inasema nini juu ya kuvunja ndoa? Inaonyesha kama kuko sababu moja tu yenye inaweza kufanya bibi na bwana wavunje ndoa. Bibi na bwana wanaweza kuvunja ndoa kama tu mumoja wao anafanya kitendo cha ndoa pamoja na mutu mwingine.​—Matayo 19:9.

MUNGU ANAOMBA WAZAZI WAFANYE NINI?

Yesu ni mufano muzuri wenye kila mutu mu familia anapaswa kufuata

11. Watoto wako na lazima ya jambo gani la maana zaidi?

11 Wazazi, mujikaze sana kupitisha wakati mingi pamoja na watoto wenu. Watoto wenu wako na lazima yenu, na zaidi sana wako na lazima muwafundishe juu ya Yehova.​—Kumbukumbu la Torati 6:4-9.

12. Wazazi wanapaswa kufanya nini ili walinde watoto wao?

12 Ulimwengu wa Shetani unaendelea kuharibika sana, na kuko watu fulani wenye wanaweza kupenda kuwafanyia watoto wetu mambo ya mubaya, hata kulala nao kinguvu. Wazazi fulani wanaona kama ni vigumu kuzungumuza na watoto wao juu ya jambo hilo. Lakini wazazi wanapaswa kushauria watoto wao juu ya watu kama hao na kuwafundisha namna ya kuwaepuka. Wazazi, munapaswa kulinda watoto wenu. *​—1 Petro 5:8.

13. Namna gani wazazi wanapaswa kufundisha watoto wao?

13 Wazazi wanapaswa kufundisha watoto wao tabia za muzuri. Namna gani unaweza kufundisha watoto wako? Watoto wako na lazima ya mazoezi, lakini wakati unawapatia malipizi, usifanye vile kwa ukali ao kwa kuwaumiza. (Yeremia 30:11) Kwa hiyo, usipatie watoto wako nizamu wakati unakasirika. Usitumie maneno makali yenye “yanatoboa kama upanga,” maneno hayo yanaweza kuwaumiza. (Mezali 12:18) Fundisha watoto wako waelewe ao wajue juu ya nini wanapaswa kuonyesha utii.​—Waefeso 6:4; Waebrania 12:9-11; ona Mafasirio Ingine ya 30.

MUNGU ANAOMBA WATOTO WAFANYE NINI?

14, 15. Juu ya nini watoto wanapaswa kutii wazazi wao?

14 Sikuzote, Yesu alimutii ao kumusikia Baba yake, hata wakati ilikuwa nguvu kufanya vile. (Luka 22:42; Yohana 8:28, 29) Yehova anaomba pia watoto watii wazazi wao.​—Waefeso 6:1-3.

15 Watoto, hata kama munaona kuwa ni nguvu kutii wazazi wenu, mukumbuke kama wakati munatii, Yehova anafurahi na wazazi wenu nao wanafurahi. *​—Mezali 1:8; 6:20; 23:22-25.

Ni nini itasaidia vijana wakuwe waaminifu kwa Mungu wakati wenzao wanawasukuma kufanya mambo ya mubaya?

16. (a) Namna gani Shetani anajaribu kuchochea vijana wafanye mambo ya mubaya? (b) Juu ya nini ni jambo la maana kuchagua marafiki wenye kumupenda Yehova?

16 Shetani anaweza kutumia marafiki wako na vijana wengine ili wakuchochee ao wakusukume kufanya mambo ya mubaya. Anajua kama inaweza kuwa nguvu kwako kuwapinga. Kwa mufano, Dina, binti ya Yakobo, alikuwa na marafiki wenye hawakumupenda Yehova. Hilo lilimuletea magumu yeye na familia yao. (Mwanzo 34:1, 2) Kama marafiki wako hawamupendi Yehova, wanaweza kukuchochea ufanye mambo yenye Yehova anachukia. Jambo hilo linaweza kukuletea huzuni wewe na familia yenu, na linaweza kuhuzunisha Mungu naye. (Mezali 17:21, 25) Kwa hiyo, ni jambo la maana sana utafute marafiki wenye kumupenda Yehova.​—1 Wakorinto 15:33.

FAMILIA YAKO INAWEZA KUWA NA FURAHA

17. Mu familia, kila mutu anapaswa kufanya nini?

17 Wakati watu wa familia wanafanya mambo yenye Mungu anawaomba wafanye, wanaepuka magumu mingi. Kwa hiyo, kama uko bwana, umupende bibi yako, na umutendee kwa upendo. Kama uko bibi, uheshimie bwana yako na ujitiishe kwake na ufuate mufano wa bibi mwenye kuzungumuziwa mu Mezali 31:10-31. Kama uko muzazi, ufundishe watoto wako kumupenda Mungu. (Mezali 22:6) Kama uko baba, uongoze familia yako “muzuri.” (1 Timoteo 3:4, 5; 5:8) Watoto, mutii wazazi wenu. (Wakolosai 3:20) Ukumbuke kama kila mutu mu familia anaweza kufanya makosa, kwa hiyo mukuwe wanyenyekevu na mukuwe tayari kuombana musamaha. Kwa kweli, Biblia inaonyesha mambo yenye Yehova anapenda kila mutu mu familia afanye.

^ fu. 12 Unaweza kupata habari zaidi juu ya namna ya kulinda watoto wako mu Sura ya 32 ya kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu, chenye kilichapishwa na Mashahidi wa Yehova.

^ fu. 15 Mutoto anaweza kukataa kutii wazazi wake kama wanamuomba afanye jambo fulani lenye linapingana na sheria ya Mungu.​—Matendo 5:29.