Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 15

Njia ya Muzuri ya Kumuabudu Mungu

Njia ya Muzuri ya Kumuabudu Mungu

1. Ni nani njo anapaswa kutuambia njia ya muzuri ya kumuabudu Mungu?

DINI (religion) za mingi zinasemaka kama zinafundisha kweli juu ya Mungu. Lakini, hiyo haiko kweli, juu kila dini inafundisha mambo yake kabisa juu ya Mungu na juu ya namna tunapaswa kumuabudu. Namna gani tunaweza kujua njia ya muzuri ya kumuabudu Mungu? Yehova tu njo anaweza kutuambia namna tunapaswa kumuabudu.

2. Ni nini inaweza kukusaidia ujue njia ya muzuri ya kumuabudu Mungu?

2 Yehova ametupatia Biblia ili tujifunze njia ya muzuri ya kumuabudu. Kwa hiyo, ujifunze Biblia, na Yehova atakusaidia ili mafundisho yake yakuletee faida juu anakupenda sana.​—Isaya 48:17.

3. Mungu anapenda tufanye nini?

3 Watu fulani wanasema kama Mungu anaitika dini zote, lakini Yesu hakufundisha vile. Alisema hivi: “Haiko kila mutu mwenye kuniambia, ‘Bwana, Bwana,’ ndiye ataingia katika Ufalme wenye kuwa mbinguni, lakini ni ule tu mwenye kufanya mapenzi ya Baba yangu.” Kwa hiyo, ni jambo la lazima tujifunze mapenzi ya Mungu ni nini na kisha tufanye mapenzi hayo. Ni jambo la maana sana kufanya vile juu Yesu alifananisha watu wenye hawamutii Mungu na watu waovu “wenye matendo ya kuvunja sheria.”​—Matayo 7:21-23.

4. Yesu alisema nini juu ya kufanya mapenzi ya Mungu?

4 Yesu alituonyesha kama haitakuwa mwepesi sikuzote kufanya mapenzi ya Mungu. Alisema hivi: “Muingie kupitia mulango mwembamba, kwa sababu mulango ni mukubwa, na barabara yenye kuongoza kwenye uharibifu ni kubwa, na watu wengi wanaingia kupitia mulango huo; lakini mulango ni mwembamba na barabara yenye kuongoza kwenye uzima ni ya kidogo, na ni watu kidogo ndio wanaipata.” (Matayo 7:13, 14) Barabara ya kidogo, ao njia ya muzuri ya kumuabudu Mungu, inaongoza watu kwenye uzima wa milele. Barabara kubwa, ao njia ya mubaya ya kumuabudu Mungu, inaongoza watu kwenye kifo. Lakini Yehova hapendi mutu yeyote akufe. Anapatia kila mutu nafasi ya kujifunza juu yake.​—2 Petro 3:9.

NJIA YA MUZURI YA KUMUABUDU MUNGU

5. Namna gani unaweza kujua wale wenye kumuabudu Mungu mu njia ya muzuri?

5 Yesu alisema kama tunaweza kutambua ao kujua wale wenye kumuabudu Mungu mu njia ya muzuri. Tunaweza kuwajua kwa kuchunguza mambo yenye wanaamini na mambo yenye wanafanya. Alisema hivi: “Mutawatambua kwa matunda yao.” Na aliongeza hivi: “Kila muti muzuri unazaa matunda ya muzuri.” (Matayo 7:16, 17) Haiko kusema kama wale wenye kumuabudu Mungu mu njia ya muzuri ni wakamilifu. Lakini watumishi wa Mungu wanajikaza sikuzote kufanya mambo yenye kuwa sawa. Tuone basi mambo yenye yatatusaidia kujua wale wenye kumuabudu Mungu mu njia ya muzuri.

6, 7. Juu ya nini mafundisho ya wale wenye kumuabudu Mungu mu njia ya muzuri yanapaswa kutoka mu Biblia? Mufano wa Yesu unatufundisha nini?

6 Mafundisho yetu yanapaswa kutoka mu Biblia. Biblia inasema hivi: “Kila Andiko limeongozwa na roho ya Mungu na liko na faida kwa kufundisha, kwa kukaripia, kwa kunyoosha mambo, kwa kutia nizamu katika haki, ili mutu wa Mungu akuwe na uwezo kamili, akiwa na vifaa kamili kwa ajili ya kila kazi njema.” (2 Timoteo 3:16, 17) Mutume Paulo aliandikia Wakristo hivi: “Wakati mulipokea neno la Mungu, lenye mulisikia kutoka kwetu, hamukulikubali [ao, hamukuliitika] kama neno la wanadamu, lakini mulilikubali kama vile liko kwa kweli, kama neno la Mungu.” (1 Watesalonike 2:13) Mafundisho ya wale wenye kumuabudu Mungu mu njia ya muzuri yanatoka tu mu Biblia, Neno la Mungu. Hayatoke mu mawazo ya watu, mu desturi, ao jambo lingine lolote.

7 Mambo yote yenye Yesu alifundisha yalitoka mu Neno la Mungu. (Soma Yohana 17:17.) Mara nyingi alitaja maneno yenye kuwa mu Maandiko. (Matayo 4:4, 7, 10) Watumishi wa kweli wa Mungu wanafuata mufano wa Yesu na mambo yote yenye wanafundisha yanatoka mu Biblia.

8. Yesu alitufundisha nini juu ya kumuabudu Yehova?

8 Tunapaswa kumuabudu Yehova tu. Zaburi 83:18 inasema hivi: “Wewe, mwenye jina lako ni Yehova, wewe peke yako ndiye Mwenye Kuwa Juu Zaidi, juu ya dunia yote.” Yesu alipenda watu wajue kabisa Mungu wa kweli ni nani, na alifundisha watu jina la Mungu. (Soma Yohana 17:6.) Yesu alisema hivi: “Yehova Mungu wako ndiye unapaswa kuabudu, na yeye peke yake ndiye unapaswa kutolea utumishi mutakatifu.” (Matayo 4:10) Kwa hiyo, sisi watumishi wa Mungu, tunafuata mufano wa Yesu. Tunamuabudu Yehova tu. Tunatumia jina lake, na tunafundisha wengine jina hilo, na mambo yenye atatufanyia.

9, 10. Namna gani tunaonyesha kama tunapendana?

9 Tunapaswa kupendana kabisa. Yesu alifundisha wanafunzi wake wapendane. (Soma Yohana 13:35.) Tunapaswa kupendana, hata kama tunatoka wapi, ao tuko wa desturi gani, ao hata kama tuko maskini ao matajiri. Upendo wetu unapaswa kutuunganisha; tunapaswa kuwa kama ndugu na dada. (Wakolosai 3:14) Njo maana hatupiganake vita ao kuua watu. Biblia inasema hivi: “Watoto wa Mungu na watoto wa Ibilisi wanaonekana kupitia jambo hili: Mutu yeyote mwenye hazoee kutenda haki hatokane na Mungu, na pia ule mwenye hamupendi ndugu yake.” Na inaongeza hivi: “Tunapaswa kupendana; hapana kama Kaini, mwenye alitokana na ule muovu na akamuua ndugu yake.”​—1 Yohana 3:10-12; 4:20, 21.

10 Tunatumia wakati wetu, nguvu zetu, na vitu vyetu vya kimwili ili kusaidiana na kutiana moyo. (Waebrania 10:24, 25) ‘Tunatendea watu wote mambo ya muzuri.’​—Wagalatia 6:10.

11. Juu ya nini tunapaswa kuamini kama tunaweza kuokolewa kupitia Yesu tu?

11 Tunapaswa kumutii Yesu juu tunaweza kuokolewa kupitia yeye tu. Biblia inasema hivi: “Hakuna wokovu katika mutu mwingine yeyote, kwa maana hakuna jina lingine chini ya mbingu lenye wanadamu walipewa, lenye kupitia hilo tunapaswa kuokolewa.” (Matendo 4:12) Mu Sura ya 5 ya kitabu hiki, tulijifunza kama Yehova alimutuma Yesu ili atoe uzima wake kuwa bei ya ukombozi kwa ajili ya wanadamu wenye kutii. (Matayo 20:28) Yehova amemuchagua Yesu ili akuwe Mufalme juu ya dunia. Njo maana Biblia inatuambia kama tunapaswa kumutii Yesu kama tunapenda kuishi milele.​—Soma Yohana 3:36.

12. Juu ya nini hatujiingize mu mambo ya politike?

12 Hatupaswe kujiingiza mu mambo ya politike. Yesu hakujiingiza mu mambo ya politike. Wakati alikuwa anasambishwa, alimuambia Pilato, mutawala Muroma, hivi: “Ufalme wangu hauko sehemu ya ulimwengu huu.” (Soma Yohana 18:36.) Kama Yesu, na sisi tuko washikamanifu kwa Ufalme wa Mungu wenye kuwa mbinguni, njo maana, hata kama tunaishi wapi, hatujiingize mu mambo ya politike. Lakini, Biblia inatuamuru tutii “mamlaka zenye kuwa kubwa,” ni kusema, serikali. (Waroma 13:1) Tunafuata sheria za inchi yetu. Lakini, wakati sheria fulani inapinga sheria za Mungu, tunapaswa kufuata mufano wa mitume wenye walisema hivi: “Tunapaswa kumutii Mungu kuwa mutawala kuliko wanadamu.”​—Matendo 5:29; Marko 12:17.

13. Tunahubiria watu nini juu ya Ufalme wa Mungu?

13 Tunaamini kama Ufalme wa Mungu tu njo utamaliza magumu yenye kuwa mu dunia. Yesu alisema kama “habari njema ya Ufalme” itahubiriwa mu dunia yote. (Soma Matayo 24:14.) Hakuna serikali ya wanadamu yenye inaweza kufanya mambo yenye Ufalme wa Mungu utatufanyia. (Zaburi 146:3) Yesu alitufundisha tusali juu ya Ufalme wa Mungu. Alisema hivi: “Ufalme wako ukuje. Mapenzi yako yafanyike duniani kama mbinguni.” (Matayo 6:10) Biblia inatuambia kama Ufalme wa Mungu utaharibu serikali zote za wanadamu na kama “ufalme huo peke yake utasimama milele.”​—Danieli 2:44.

14. Unawaza ni nani wenye kumuabudu Mungu mu njia ya muzuri?

14 Kisha kujifunza mambo hayo, ujiulize hivi: ‘Ni nani wenye wanafundishaka mambo yenye kutoka mu Biblia? Ni nani wanaambiaka wengine juu ya jina la Mungu? Ni nani wanapendanaka kabisa na wanaamini kama Mungu alimutuma Yesu ili atuokoe? Ni nani hawajiingizake mu mambo ya politike? Ni nani wanahubiriaka watu kama Ufalme wa Mungu tu njo unaweza kumaliza magumu yetu?’ Ni Mashahidi wa Yehova tu.​—Isaya 43:10-12.

UTAFANYA NINI?

15. Tunapaswa kufanya nini kama tunapenda Mungu aitike ibada yetu?

15 Zaidi ya kuamini kama Mungu iko, tunapaswa kufanya jambo lingine. Hata pepo wachafu wanaamini kama Mungu iko, lakini hawamutii. (Yakobo 2:19) Kama tunapenda Mungu aitike ibada yetu, hatupaswe tu kuamini kama iko, lakini tunapaswa pia kufanya mambo yenye anasema.

16. Juu ya nini tunapaswa kuachana na dini za uongo?

16 Ili Mungu aitike ibada yetu, tunapaswa kuachana na dini za uongo. Nabii Isaya aliandika hivi: “Mutoke katikati yake, mujilinde mukiwa safi.” (Isaya 52:11; 2 Wakorinto 6:17) Njo maana tunapaswa kuachana na kila kitu chenye kuwa na upatano na dini za uongo.

17, 18. “Babiloni Mukubwa” ni nini? Juu ya nini tunapaswa kutoka haraka mu dini za uongo?

17 Dini za uongo ni nini? Ni dini zote zenye zinafundisha watu kumuabudu Mungu mu njia yenye haipatane na Neno lake. Biblia inaita dini zote za uongo “Babiloni Mukubwa.” (Ufunuo 17:5) Juu ya nini? Kisha Garika ya siku za Noa, mafundisho mingi ya dini za uongo yalianzia mu muji wa Babiloni. Mafundisho hayo ya uongo yalienea mu dunia yote. Kwa mufano, watu wenye walikuwa wanaishi Babiloni waliabudu vikundi vya miungu tatu-tatu. Na leo, dini nyingi zinafundisha kama Mungu ni Utatu. Lakini Biblia inafundisha waziwazi kama kuko Mungu mumoja wa kweli, ni kusema, Yehova, na kama Yesu ni Mwana wake. (Yohana 17:3) Tena, watu wenye walikuwa wanaishi Babiloni waliamini kama sehemu fulani ya mutu inaendelea kuishi kisha mwili kufa na kama inaweza kuteseka mu moto wa mateso. Lakini hiyo haiko kweli.​—Ona Mafasirio Ingine ya 14, 17, na 18.

18 Mungu ametabiri kama karibuni dini zote za uongo zitaharibiwa. (Ufunuo 18:8) Unaona ni juu ya nini unapaswa kutoka haraka sana mu dini ya uongo? Yehova Mungu anapenda ufanye vile bila kuchelewa.​—Ufunuo 18:4.

Wakati unamutumikia Yehova pamoja na watu wake, utakuwa mu familia ya ndugu na dada wa mu dunia yote

19. Wakati unaamua kumutumikia Yehova, atakuhangaikia namna gani?

19 Wakati unaamua kutoka mu dini ya uongo ili umutumikie Yehova, pengine marafiki wako fulani ao watu fulani wa familia hawataelewa uamuzi wako na wanaweza hata kukupinga. Lakini Yehova hatakuacha. Utakuwa mu familia kubwa ya mamilioni ya watu wenye kupendana kabisa, na utakuwa na tumaini la kuishi milele mu dunia mupya ya Mungu. (Marko 10:28-30) Pengine marafiki wako fulani ao watu fulani wa familia, wenye wanapinga uamuzi wako wa kumutumikia Yehova, wanaweza kufikia kuamua kujifunza Biblia.

20. Juu ya nini ni jambo la maana kumuabudu Mungu mu njia ya muzuri?

20 Hivi karibuni, Mungu atatosha mambo yote ya mubaya na Ufalme wake utatawala dunia yote. (2 Petro 3:9, 13) Huo utakuwa wakati wa muzuri sana! Watu wote watamuabudu Yehova mu njia yenye anapenda. Kwa hiyo, ni jambo la maana ukamate uamuzi sasa wa kumuabudu Mungu mu njia ya muzuri.