Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 17

Sala Ni Zawadi Kutoka kwa Mungu

Sala Ni Zawadi Kutoka kwa Mungu

“Mutengenezaji wa mbingu na dunia” anapenda kusikiliza sala zetu.​—Zaburi 115:15

1, 2. (a) Juu ya nini unawaza kama sala ni zawadi ya maana sana? (b) Juu ya nini tunapaswa kujua mambo yenye Biblia inasema juu ya sala?

DUNIA ni ya kidogo sana wakati inalinganishwa na ulimwengu wote muzima. Wakati Yehova anaangalia dunia, anaona watu wa mataifa yote kama vile tone ya maji mu mbegeti. (Zaburi 115:15; Isaya 40:15) Hata kama tuko wadogo sana wakati tunalinganishwa na ulimwengu wote, Zaburi 145:18, 19 inasema hivi: “Yehova iko karibu na wale wote wenye kumuitia; wote wenye kumuitia katika ukweli. Anatimiza tamaa ya wale wenye kumuogopa; anasikia kilio chao cha kuomba musaada, na anawaokoa.” Hiyo ni heshima kubwa sana! Yehova, Muumbaji mweza-yote, anapenda kuwa karibu na sisi, na anapenda kusikiliza sala zetu. Kwa kweli, sala ni zawadi ya maana sana, zawadi ya pekee, yenye Yehova amepatia kila mumoja wetu.

2 Lakini, Yehova atasikiliza sala zetu kama tu tunazungumuza naye kwa njia yenye anaitika. Namna gani tunaweza kufanya vile? Tuone basi mambo yenye Biblia inasema juu ya sala.

JUU YA NINI TUNAPASWA KUSALI KWA YEHOVA?

3. Juu ya nini unapaswa kusali kwa Yehova?

3 Yehova anapenda usali kwake, ao uzungumuze naye. Namna gani tunajua jambo hilo? Unaweza kusoma Wafilipi 4:6, 7. Fikiria maneno ya andiko hilo. Muumbaji wa ulimwengu anakuhangaikia sana na anapenda umuambie magumu yako na namna unajisikia.

4. Kusali kwa Yehova kila mara kunaweza kukusaidia ukuwe na urafiki wenye nguvu pamoja naye. Namna gani?

4 Sala inatusaidia kuwa na urafiki wa sana pamoja na Yehova. Wakati marafiki wanaambiana kila mara mawazo yao, mahangaiko yao, na namna wanajisikia, urafiki wao unakuwa wenye nguvu zaidi. Ni vile pia wakati tunasali kwa Yehova. Kupitia Biblia, amekujulisha mawazo yake na namna anajisikia, na mambo yenye atafanya wakati wenye kuja. Unaweza kumuambia namna unajisikia kabisa mu moyo wako kwa kuzungumuza naye kila mara. Wakati unafanya vile, urafiki wako pamoja na Yehova utakuwa wenye nguvu zaidi.​—Yakobo 4:8.

TUNAPASWA KUFANYA NINI ILI MUNGU ASIKILIZE SALA ZETU?

5. Ni nini inaonyesha kama Yehova hasikilize sala zote?

5 Yehova anasikiliza sala zote? Hapana. Wakati wa nabii Isaya, Yehova aliambia Waisraeli hivi: “Hata kama munatoa sala nyingi, sisikilize; mikono yenu imejaa damu.” (Isaya 1:15) Kwa hiyo, kama hatuko waangalifu, tunaweza kufanya mambo yenye yanaweza kutufanya tumuache Yehova, na kufanya asisikilize sala zetu.

6. Juu ya nini imani ni ya maana sana? Namna gani unaweza kuonyesha kama uko na imani?

6 Kama tunapenda Yehova asikilize sala zetu, tunapaswa kuwa na imani kwake. (Marko 11:24) Mutume Paulo alisema hivi: “Bila imani haiwezekane kumupendeza Mungu, kwa maana mutu yeyote mwenye anamukaribia Mungu lazima aamini kwamba yeye iko na kwamba yeye anakuwa mwenye kuwapatia zawabu [ao, malipo] wale wenye wanamutafuta kwa bidii.” (Waebrania 11:6) Lakini, zaidi ya kusema tu kama tuko na imani, tunapaswa kufanya jambo lingine. Tunapaswa kuonyesha imani yetu waziwazi kwa kumutii Yehova kila siku.​—Soma Yakobo 2:26.

7. (a) Juu ya nini tunapaswa kuwa wanyenyekevu na kuonyesha heshima wakati tunasali kwa Yehova? (b) Wakati tunasali, namna gani tunaweza kuonyesha kama mambo yenye tunasema yanatoka mu moyo wetu?

7 Tunapaswa kuwa wanyenyekevu na kuonyesha heshima wakati tunasali kwa Yehova. Juu ya nini? Kama tunapenda kuzungumuza na mufalme ao raisi (kiongozi wa inchi), tutafanya vile kwa heshima. Yehova ni Mungu Mweza-Yote, kwa hiyo tunapaswa kuonyesha heshima kubwa na kuwa wanyenyekevu sana wakati tunazungumuza naye. (Mwanzo 17:1; Zaburi 138:6) Wakati tunasali, tunapaswa pia kusema mambo yenye kutoka mu moyo wetu, hatupaswe tu kurudilia-rudilia maneno ileile tena na tena.​—Matayo 6:7, 8.

8. Wakati tunasali juu ya jambo fulani, tunapaswa kufanya jambo gani lingine?

8 Tena, wakati tunasali juu ya jambo fulani, tunapaswa kufanya yetu yote ili tutende kupatana na sala zetu. Kwa mufano, kama tunasali kwa Yehova ili atusaidie kupata mambo yenye tuko nayo lazima kila siku hatupaswe kuwa wavivu. Hatupaswe kuwaza kama atatupatia kila kitu, hata kama hatufanye kazi. Tunapaswa kutumika sana na kuitika kila kazi yenye tunaweza kufanya. (Matayo 6:11; 2 Watesalonike 3:10) Ao kama tunamuomba Yehova atusaidie ili tuache kufanya jambo fulani la mubaya, tunapaswa kuepuka kila hali yenye inaweza kutuchochea ao kutusukuma kufanya jambo hilo. (Wakolosai 3:5) Sasa tuzungumuzie maulizo fulani yenye watu wanaulizaka sana juu ya sala.

MAULIZO YENYE WATU WANAULIZAKA SANA JUU YA SALA

9. Tunapaswa kusali kwa nani? Andiko la Yohana 14:6 linatufundisha nini juu ya sala?

9 Tunapaswa kusali kwa nani? Yesu alifundisha wanafunzi wake wasali kwa “Baba yetu mwenye kuwa mbinguni.” (Matayo 6:9) Tena alisema hivi: “Mimi ndiye njia na kweli na uzima. Hakuna mwenye anakuja kwa Baba isipokuwa kupitia mimi.” (Yohana 14:6) Kwa hiyo, tunapaswa kusali kwa Yehova tu kupitia jina la Yesu. Kusali kupitia jina la Yesu maana yake nini? Ili Yehova asikilize sala zetu, tunapaswa kuonyesha kama tunaheshimia daraka la pekee lenye Yehova alimupatia Yesu. Kama vile tumekwisha kujifunza, Yesu alikuja mu dunia ili atuokoe kutoka katika zambi na kifo. (Yohana 3:16; Waroma 5:12) Tena, Yehova amemufanya Yesu kuwa Kuhani Mukubwa na Muamuzi.​—Yohana 5:22; Waebrania 6:20.

Unaweza kusali kila wakati

10. Tunapaswa kusimama, kukaa, kupiga magoti, ao kuwa mu hali ingine fulani wakati tunasali? Fasiria.

10 Tunapaswa kusimama, kukaa, kupiga magoti, ao kuwa mu hali ingine fulani wakati tunasali? Hapana, Yehova hatuombe tupige magoti, tukae, ao tusimame wakati tunasali. Biblia inatufundisha kama tunaweza kuzungumuza na Yehova mu kila hali yenye kuonyesha heshima. (1 Mambo ya Nyakati 17:16; Nehemia 8:6; Danieli 6:10; Marko 11:25) Jambo lenye Yehova anaona kuwa la maana sana, haiko hali yetu wakati tunasali, lakini ni kuzungumuza naye kwa heshima na kusema mambo yenye kutoka mu moyo. Tunaweza kusali kwa sauti ao kimya-kimya kila mahali kwenye tuko na kila wakati, muchana ao usiku. Wakati tunasali kwa Yehova, tunaweza kutumainia kama atatusikiliza hata kama hakuna mutu mwingine mwenye anatusikia.​—Nehemia 2:1-6.

11. Tunaweza kusali kwa Yehova juu ya mambo gani fulani?

11 Tunaweza kusali juu ya mambo gani? Tunaweza kusali juu ya kila jambo lenye kupatana na mapenzi ya Yehova. Biblia inasema hivi: “Hata kama tunaomba nini kulingana na mapenzi yake, yeye anatusikia.” (1 Yohana 5:14) Tunaweza kusali juu ya mambo yetu wenyewe? Ndiyo. Kusali kwa Yehova ni sawa na kuzungumuza na rafiki yetu wa sana. Tunaweza kumuambia Yehova mambo yote yenye kuwa mu akili na mu moyo wetu. (Zaburi 62:8) Tunaweza kumuomba atupatie roho yake takatifu yenye nguvu ili itusaidie kufanya mambo ya muzuri. (Luka 11:13) Tena, tunaweza kumuomba Yehova atupatie hekima ya kukamata maamuzi ya muzuri, na tunaweza kumuomba atupatie nguvu ya kupiganisha magumu. (Yakobo 1:5) Tunapaswa kumuomba Yehova atusamehe zambi zetu. (Waefeso 1:3, 7) Na, tunapaswa kusali kwa ajili ya wengine, kwa mufano, tunapaswa kusali kwa ajili ya watu wa familia yetu na ndugu na dada zetu katika kutaniko.​—Matendo 12:5; Wakolosai 4:12.

12. Tunapaswa kutanguliza mambo gani mu sala zetu?

12 Tunapaswa kutanguliza mambo gani mu sala zetu? Mambo yenye kumuhusu Yehova na mapenzi yake. Tunapaswa kumushukuru kwa moyo wote juu ya mambo yote yenye ametufanyia. (1 Mambo ya Nyakati 29:10-13) Tunajua jambo hilo juu wakati Yesu alikuwa mu dunia, alifundisha wanafunzi wake namna ya kusali. (Soma Matayo 6:9-13.) Alisema kama walipaswa kwanza kuomba jina la Mungu litakaswe, ni kusema, lionwe kuwa takatifu. Kisha, Yesu alionyesha kama tunapaswa kuomba Ufalme wa Mungu ukuje na mapenzi yake yafanyike mu dunia yote. Yesu alionyesha kama tunaweza kusali juu ya mambo yenye tuko nayo lazima kisha kusali juu ya mambo hayo ya maana sana. Wakati tunatanguliza Yehova na mapenzi yake mu sala zetu, tunaonyesha ni mambo gani yenye tunaona kuwa ya maana zaidi.

13. Sala zetu zinapaswa kuwa na urefu gani?

13 Sala zetu zinapaswa kuwa na urefu gani? Biblia haiseme. Sala zetu zinaweza kuwa za mufupi ao za murefu, kupatana na hali. Kwa mufano tunaweza kutoa sala ya mufupi mbele ya kula, lakini tunaweza kutoa sala ya murefu wakati tunamushukuru Yehova ao wakati tunamuelezea magumu yetu. (1 Samweli 1:12, 15) Hatupaswe kutoa sala za murefu ili tu kujionyesha kwa wengine, kama vile watu fulani walikuwa wanafanya wakati wa Yesu. (Luka 20:46, 47) Yehova hapendezwe na sala za namna hiyo. Kusema mambo yenye kutoka mu moyo wetu njo jambo lenye Yehova anaona kuwa la maana.

14. Tunapaswa kusali mara ngapi, na hilo linatufundisha nini juu ya Yehova?

14 Tunapaswa kusali mara ngapi? Yehova anatuomba tuzungumuze naye kila mara. Biblia inasema kama tunapaswa “kusali bila kuacha,” na ‘kudumu katika sala,’ ao kuendelea kusali. (Matayo 26:41; Waroma 12:12; 1 Watesalonike 5:17) Sikuzote, Yehova iko tayari kutusikiliza. Tunaweza kumushukuru kila siku juu anatupenda na anatupatia mambo mingi. Tunaweza pia kumuomba atuongoze, atupatie nguvu, na kutufariji. Kama tunaona sala kuwa zawadi ya maana sana kutoka kwa Yehova, tutasali kila mara wakati tunapata nafasi ya kufanya vile.

15. Juu ya nini tunapaswa kusema “amina” ku mwisho wa sala?

15 Juu ya nini tunapaswa kusema “amina” ku mwisho wa sala? Neno “amina” maana yake “hakika” ao “ikuwe vile.” Kusema amina kunaonyesha kama tunaitika mambo yenye tumesema mu sala, ni kusema, yanatoka mu moyo wetu. (Zaburi 41:13) Biblia inatufundisha kama ni muzuri kusema “amina” kimya-kimya ao kwa sauti ku mwisho wa sala yenye kutolewa kwa ajili ya watu wengi. Kufanya vile kunaonyesha kama tunaitika mambo yenye yamesemwa mu sala.​—1 Mambo ya Nyakati 16:36; 1 Wakorinto 14:16.

NAMNA GANI MUNGU ANAJIBU SALA ZETU?

16. Je, Yehova anajibiaka kabisa sala zetu? Fasiria.

16 Je, Yehova anajibiaka kabisa sala zetu? Ndiyo. Biblia inamuita “Musikiaji wa sala.” (Zaburi 65:2) Yehova anasikiaka na kujibu sala za mamilioni ya watu wenye mioyo ya muzuri, na anafanya vile kwa njia mbalimbali.

17. Namna gani Yehova anatumia malaika na watumishi wake wenye kuwa mu dunia juu ya kujibu sala zetu?

17 Yehova anatumia malaika na watumishi wake wenye kuwa mu dunia juu ya kujibu sala zetu. (Waebrania 1:13, 14) Kuko mifano mingi ya watu wenye walisali kwa Mungu ili awasaidie kuelewa Biblia na kisha wakati mufupi Mashahidi wa Yehova waliwatembelea. Biblia inaonyesha kama malaika wanasaidia kutangaza “habari njema” mu dunia yote. (Soma Ufunuo 14:6.) Na pengine tumekwisha kusali kwa Yehova juu ya magumu fulani ao juu ya jambo fulani lenye tulikuwa nalo lazima na kisha ndugu ao dada yetu Mukristo akatusaidia.​—Mezali 12:25; Yakobo 2:16.

Yehova anaweza kujibu sala zetu kwa kuchochea Wakristo wenzetu watusaidie

18. Namna gani Yehova anatumia roho yake takatifu na Biblia juu ya kujibu sala zetu?

18 Yehova anatumia roho yake takatifu ili kujibu sala zetu. Wakati tunamuomba Mungu atusaidie kupiganisha magumu fulani, anaweza kutumia roho yake takatifu ili kutupatia muongozo na nguvu. (2 Wakorinto 4:7) Tena, Yehova anatumia Biblia ili kujibu sala zetu na kutusaidia kukamata maamuzi ya muzuri. Wakati tunasoma Biblia, tunaweza kupata maandiko yenye yatatusaidia. Tena, Yehova anaweza kuchochea mutu fulani mwenye anatoa maelezo kwenye mikutano ili aseme jambo fulani lenye tuko na lazima ya kusikia. Na anaweza kuchochea muzee wa kutaniko azungumuzie wazo fulani la Biblia pamoja na sisi.​—Wagalatia 6:1.

19. Juu ya nini tunaweza kuona kuwa Yehova hajibu sala zetu?

19 Lakini wakati fulani, tunaweza kujiuliza hivi: ‘Juu ya nini Yehova hajajibu sala zangu?’ Ukumbuke kama anajua wakati na namna ya kujibu sala zetu. Anajua mambo yenye tuko nayo lazima. Wakati fulani, tunapaswa kuendelea kusali ili tuonyeshe kama tuko na lazima kabisa ya mambo yenye tuko tunaomba na kumuonyesha kama tuko na imani kabisa kwake. (Luka 11:5-10) Wakati fulani Yehova anajibu sala zetu mu njia zenye hatukuwazia. Kwa mufano, tunaweza kusali juu ya magumu fulani, lakini kuliko kutosha magumu hayo, anaweza kutupatia nguvu ya kuvumilia.​—Soma Wafilipi 4:13.

20. Juu ya nini tunapaswa kusali kwa Yehova kila mara?

20 Sala ni zawadi ya maana sana yenye Yehova ametupatia! Tunaweza kuamini kabisa kama atatusikiliza. (Zaburi 145:18) Na kama tunamuambia Yehova kila mara mambo yenye kuwa mu moyo wetu, urafiki wetu pamoja naye utakuwa wenye nguvu zaidi.