Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ulizo LA 4

Nifanye Nini Kama Ninafanya Makosa?

Nifanye Nini Kama Ninafanya Makosa?

SABABU GANI ULIZO HILO NI LA MAANA

Kukubali makosa yako kutakufanya ukuwe mutu mwenye kukamata mambo kwa uzito na mwenye kutumainika.

UNGEFANYA NINI?

Wazia jambo hili: Wakati Tim anacheza na marafiki wake, kabumbu yenye anapiga inavunja kioo cha motokari ya jirani wao.

Kama ungekuwa Tim, ungefanya nini?

WAZA KIDOGO!

KUNA MAMBO TATU YENYE UNAWEZA KUFANYA:

  1. Kukimbia.

  2. Kusema kama ni kosa la mutu mwengine.

  3. Kuambia jirani huyo jambo lenye limetokea na kumuambia kama uko tayari kutengeneza kioo hicho.

Pengine unaweza kujaribu kuchagua Jambo la A. Lakini, kuna sababu ya muzuri ya kukubali makosa yako, ikuwe ni kioo chenye uliharibisha ao jambo lingine.

SABABU TATU ZA KUKUBALI MAKOSA YAKO

  1. Ni muzuri kufanya hivyo.

    Biblia inasema hivi: “Tunataka kujiendesha kwa unyoofu [ao, uaminifu] katika mambo yote.”—Waebrania 13:18.

  2. Watu wanasamehe zaidi wale wenye wanakubali makosa yao.

    Biblia inasema hivi: “Anayefunika makosa yake hatafanikiwa, lakini yeye anayeyaungama na kuyaacha ataonyeshwa rehema.”—Methali 28:13.

  3. Jambo la maana zaidi ni kwamba, kukubali makosa kunamufurahisha Mungu.

    Biblia inasema hivi: ‘Mutu mwenye hila [ao, tabia ya kudanganya] ni chukizo kwa Yehova, lakini urafiki Wake uko pamoja na watu wanyoofu.’—Methali 3:32.

Karina, mwenye kuwa na miaka 20, alijaribu kumuficha baba yake karatasi ya amande yenye alilipa kwa sababu ya kutembeza motokari mbio sana. Lakini, hangeweza kuendelea kuficha jambo hilo. Karina anasema hivi: “Kisha mwaka moja, baba yangu alivumbua karatasi ya amande yenye kuwa na jina langu. Nilihangaika sana!”

Jambo hilo lilimufundisha nini Karina? Anasema hivi: “Kuficha makosa, kunafanya hali ikuwe mubaya zaidi. Hata kama unayaficha, utayalipa tu!”

MAKOSA YAKO YANAWEZA KUKUFUNDISHA NINI?

Biblia inasema hivi: “Sisi sote hujikwaa [ao, tunafanya makosa] mara nyingi.” (Yakobo 3:2) Na kama vile tuliona, kukubali makosa yako kisha tu kuyafanya ni alama yenye kuonyesha kama uko munyenyekevu na mwenye kukomaa.

Jambo lingine ni mambo yenye makosa yako yanakufundisha. Mwanamuke mwenye kuitwa Vera anasema hivi: “Ninajikaza kuona makosa yangu kuwa njia ya kupata fundisho lenye litanisaidia kuwa mutu muzuri zaidi na kujua jambo la kufanya wakati nitafanya tena makosa.” Acha tuone namna unaweza kufanya hivyo.

Unabeba kinga ya baba yako na kisha unaiharibisha. Utafanya nini?

  • Kunyamaza na kuwaza kama baba yako hatajua.

  • Kumuambia baba yako jambo lenye ulifanya.

  • Kumuambia baba yako jambo lenye lilitokea na kusema kama ni kosa la mutu mwengine.

Unashindwa examen fulani kwa sababu haukujifunza. Utafanya nini?

  • Utasema ni kosa la examen.

  • Utaitika kwamba ni kwa sababu haukujifunza.

  • Utasema kwamba mwalimu wako hakupendake.

Kukaza akili yako juu ya makosa yenye ulifanya zamani ni kama vile kuendelea kujiangalia katika kioo cha motokari wakati unatembeza

Sasa, fikiria mambo yenye tumetoka kuzungumuzia. Jaribu kujitia pa nafasi ya (1) baba yako na (2) mwalimu wako. Baba yako na mwalimu wako watawaza nini kama uko tayari kukubali makosa yako? Watawaza nini kama unaficha makosa yako?

Sasa, kumbuka kosa fulani lenye ulifanya mwaka jana na ujibu maulizo yenye kufuata.

Ulifanya kosa gani? Kisha, ulifanya nini?

  • Nilificha kosa hilo.

  • Nilisema kama ni kosa la mutu mwengine.

  • Nilikubali mara moja kosa hilo.

Kama haukukubali kosa lako, ulijisikia namna gani?

  • Muzuri, haikunifanya kitu!

  • Mubaya, nilipaswa tu kusema kweli.

Namna gani ungemaliza hali hiyo katika njia yenye kuwa muzuri zaidi?

Umejifunza nini kupitia makosa yenye ulifanya?

UNAWAZA NAMNA GANI?

Sababu gani watu fulani hawakubali makosa yao?

Kama unazoea kuficha makosa yako, watu wengine watakuona namna gani? Lakini kama unakubali makosa yenye unafanya, watu wengine watakuona namna gani?—Luka 16:10.