Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ulizo LA 5

Nifanye Nini Kama Ninachokozwa Kwenye Masomo?

Nifanye Nini Kama Ninachokozwa Kwenye Masomo?

SABABU GANI ULIZO HILO NI LA MAANA?

Namna utajiendesha wakati unachokozwa inaweza kufanya mambo yakuwe muzuri zaidi ao mubaya zaidi.

UNGEFANYA NINI?

Wazia jambo hili: Thomas hapendi kuenda kwenye masomo leo, wala kesho, wala siku ingine. Mambo yote yalianzia kwenye masomo kumepita miezi tatu. Wakati huo wanafunzi wenzake walieneza habari za mubaya juu yake. Kisha walianza kumupatia majina mengi ya kumukasirisha. Wakati fulani mwanafunzi mwenzake anaweza kuangusha mabuku (cahiers) zenye kuwa katika mikono ya Thomas na kufanya kama vile ilikuwa aksida, ao mumoja kati ya wanafunzi wenye kuwa katika kikundi anaweza kumusukuma, na wakati Thomas anageuka ili kuangalia mutu mwenye alimusukuma, hatambue kama ni nani. Na jambo la mubaya zaidi ni kwamba, jana Thomas alipata barua kupitia Internete yenye kumuambia afanye angalisho . . .

Kama ungekuwa Thomas, ungefanya nini?

WAZA KIDOGO!

Haiko kusema kwamba hauna nguvu kabisa! Kwa kweli, unaweza kumushinda mutu mwenye anakuchokoza bila kumupiga. Namna gani?

  • UKUWE MWENYE KUTULIA. Biblia inasema hivi: ‘Mutu mujinga anaiachilia roho yake yote, lakini mwenye hekima anaituliza mupaka mwisho. (Methali 29:11) Kama unajikaza kuonyesha kwamba unatulia kabisa, inawezekana wale wenye kukuchokoza hawatafurahia tena kuendelea kukuchokoza.

  • USIRUDISHE UBAYA KWA UBAYA. Biblia inasema hivi: ‘Musimulipe yeyote uovu kwa uovu.’ (Waroma 12:17) Kama unatafuta kurudisha ubaya kwa ubaya, mambo yatakuwa mubaya zaidi.

  • USIJIINGIZE KATIKA MAGUMU. Biblia inasema hivi: ‘Mutu mwerevu ni yule ambaye ameona musiba [ao, hatari] na kujificha.’ (Methali 22:3) Ujikaze kabisa kuepuka watu wenye wanaweza kukuchokoza ao hali zenye zinaweza kufanya watu wakuchokoze.

  • UWAJIBIE KWA NJIA YENYE HAWAWAZIE. Biblia inasema hivi: ‘Jibu, linapokuwa la upole, linageuza gazabu [ao, hasira].’ (Methali 15:1) Unaweza hata kuchekesha kidogo. Kwa mufano, kama mutu mwenye anakuchokoza anasema kwamba unanenepa sana, unaweza kumujibia, “Ninaona kuwa ni muzuri kupunguza kilo fulani!”

  • UNYAMAZE. Nora mwenye kuwa na miaka 19 anasema hivi: “Kunyamaza kunaonyesha kwamba uko mutu mwenye kukomaa na kwamba uko na nguvu kuliko mutu mwenye anakuchokoza. Kufanya hivyo, kunaonyesha kwamba unajua kujizuia. Lakini, mutu mwenye anakuchokoza hajue kufanya jambo hilo.”—2 Timotheo 2:24.

  • UFANYE NGUVU ILI KUONYESHA KWAMBA UNAJITUMAINIA. Mara nyingi, watu wenye kuchokoza wengine wanaweza kutambua watu wenye hawajitumainie na wenye hawana nguvu ya kupigana kama wanachokozwa. Lakini, watu wengi wenye wanachokoza wengine hawatakuchokoza kama wanaona kwamba hauwapatie nafasi ya kufanya hivyo.

  • UMUAMBIE MUTU MWENGINE. Mutu mumoja mwenye alikuwa mwalimu wa masomo anasema hivi: “Ningeshauri mutu mwenye anachokozwa amuambie mutu mwengine jambo hilo. Hilo ni jambo la muzuri la kufanya ili kuzuia mutu mwengine asichokozwe.”

    Kujitumania kutakupatia nguvu yenye mutu mwenye anakuchokoza hana

Kujitumania kutakupatia nguvu yenye mutu mwenye anakuchokoza hana