Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

ULIZO LA 6

Nifanye Nini Kama Wenzangu Wananikaza Kufanya Jambo Fulani?

Nifanye Nini Kama Wenzangu Wananikaza Kufanya Jambo Fulani?

SABABU GANI ULIZO HILO NI LA MAANA?

Kama unajitumainia, unaweza kuongoza maisha yako kuliko kuacha watu wengine wayaongoze.

UNGEFANYA NINI?

Wazia jambo hili: Brian anaogopa wakati anaona wanafunzi wenzake wanamukaribia. Wanafunzi hao wamejaribu kumupatia tumbako mara mbili katika juma hili. Sasa, hii ni mara ya tatu.

Mwanafunzi wa kwanza anasema hivi:

“Ah! Uko peke yako tena? Acha nikuonyeshe rafiki yangu.”

Anakazia neno “rafiki” wakati anatosha kitu fulani katika mufuko wake na kumupatia Brian kitu hicho.

Brian anaona tumbako katika mukono wa rafiki yake. Brian anaogopa tena zaidi.

Brian anamuambia hivi: “Unisamehe, nimekwisha kukuambia kama . . .”

Mwanafunzi wa pili anamukatiza na kusema: “Mutu haogopake vile!”

Brian anapata nguvu ya kusema hivi: “Siogope!”

Mwanafunzi huyo wa pili anatia mukono wake kwenye mabega ya Brian na anasema kwa sauti ya utulivu, “Ukamate tu!”

Mwanafunzi wa kwanza anamupatia Brian tumbako na anasema kwa sauti ya chini hivi: “Hatutaambia mutu. Hakuna mutu mwenye atajua.”

Kama ungekuwa Brian, ungefanya nini?

WAZA KIDOGO!

Marafiki wa Brian walifikiri juu ya mambo yenye walikuwa wanafanya? Waliamua kufanya hivyo wao wenyewe? Pengine hapana. Mara nyingi, walifuata mufano wa wengine. Walipenda watu wengine wawakubali ili wafuate mufano wao.

Ungekuwa katika hali kama hiyo, ungefanya nini ili kupambana na jambo lenye vijana wenzako wanakukaza ufanye?

  1. UJITAYARISHE

    Biblia inasema hivi: ‘Mutu mwerevu ni yule ambaye ameona musiba [ao, hatari] na kujificha, lakini wasio na uzoefu wameendelea mbele nao lazima waumie.’—Methali 22:3.

    Mara nyingi, unaweza kuona hatari mbele ya wakati. Kwa mufano, wazia unaona kikundi cha wanafunzi wenzako wenye wanakuja mbele yako, na wako wanavuta. Kama unajitayarisha mbele ya wakati, unaweza kujua namna ya kupambana na hali hiyo.

  2. UFIKIRI

    Biblia inasema hivi: ‘Mukuwe na zamiri njema.’—1 Petro 3:16.

    Ujiulize, ‘Nitajisikia namna gani wakati wenye kuja kama ninafuata watu wengine?’ Kwa kweli, unaweza kufurahisha wanafunzi wenzako kwa muda kidogo. Lakini, utajisikia namna gani wakati wenye kuja? Uko tayari kuharibisha sifa yako ili kufurahisha wanafunzi wenzako tu?—Kutoka 23:2.

  3. UAMUE

    Biblia inasema hivi: “Mwenye hekima ni mwangalifu.”—Methali 14:16, Biblia Habari Njema kwa Wote

    Lakini, siku moja tunapaswa kukamata maamuzi fulani na kupata matokeo ya maamuzi hayo. Biblia inazungumuzia wanaume fulani wenye walikamata maamuzi ya muzuri kama vile Yosefu, Ayubu, na Yesu. Inazungumuzia pia wengine wenye walikamata maamuzi ya mubaya kama vile Kaini, Esau, na Yuda. Utakamata uamuzi gani?

Biblia inasema hivi: “Utende kwa uaminifu.” (Zaburi 37:3) Kama umekwisha kufikiri juu ya matokeo ya jambo lenye unataka kufanya na kukamata uamuzi wako, inaweza kuwa mwepesi kuonyesha musimamo wako, na unaweza kupata matokeo ya muzuri kuliko namna uliwazia.

Hapana kuogopa. Haiko lazima kuambia marafiki wako maneno mengi. Kusema HAPANA bila kufanya muzaha kunaweza kutosha. Ao ili kuonyesha waziwazi uamuzi wako, unaweza kusema:

  • “Muniache!”

  • “Sifanyake mambo kama hayo!”

  • “Ninaona kwamba hamunijue muzuri kabisa!”

Siri ni kujibu haraka na kwa njia yenye kuonyesha kama uko hakika na uamuzi wako. Kama unafanya hivyo, unaweza kushangaa kuona namna marafiki wako wanaweza kukuacha bila kukawia!

Unaweza Kufanya Nini Wakati Wengine Wanakucheka?

Kama unakubali kuongozwa na vijana wenzako, unakuwa kama robot yenye wanaongoza

Unaweza kufanya nini kama vijana wenzako wanakuzarau? Utafanya nini kama wanasema, “Ni nini, unasikia woga sana?” Ujue kwamba vijana wenzako wanapenda tu kukucheka. Unaweza kufanya nini? Uko na mambo mbili yenye unaweza kufanya.

  • Unaweza kukubali wakuzarau. (“Ni kweli, ninaogopa!” Kisha uwaelezee kwa kifupi sababu gani unaogopa.)

  • Unaweza kuamua kusema jambo fulani. Uwaambie waziwazi sababu gani unakataa kufanya jambo lenye wanakuomba ufanye, na uwaambie kwamba wanapaswa kufikiri muzuri. (“Mutu mwenye kuwa na akili ya muzuri hawezi kuvuta tumbako!”)

Kama vijana wenzako wanaendelea kukukaza ufanye jambo la mubaya, ondoka! Ukumbuke kwamba kama unabakia nao muda murefu, mukazo huo utaendelea kuwa mukubwa zaidi. Wakati unaondoka, unaonyesha kwamba haukubali watu wengine wabadilishe mambo yenye unaamini kabisa.

Kwa kweli, hauwezi kuepuka kabisa mukazo wa vijana wenzako. Lakini unaweza kuamua mambo yenye unataka kufanya, kuwajulisha wengine mambo yenye unaamini, na kukataa wengine wakuongoze. Kwa kweli, uamuzi ni wako!—Yoshua 24:15.