Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

ULIZO LA 8

Ninapaswa Kujua Nini Kuhusu Kulalwa Kinguvu?

Ninapaswa Kujua Nini Kuhusu Kulalwa Kinguvu?

SABABU GANI ULIZO HILO NI LA MAANA?

Kila mwaka mamilioni ya watu wanabakwa ao kulalwa kinguvu, na zaidi vijana ndio wanatendewa mubaya.

UNGEFANYA NINI?

Mutu fulani alimutupa Annette chini mbele atambue mambo yenye kutokea. Annette anasema hivi: “Nilifanya yangu yote ili kumuzuia asinitendee mubaya. Nilijikaza kulalamika, lakini wapi. Nilimusukuma, nilimupiga kwa muguu na mukono, na kumukwaruza. Na hilo lilifanya anichome kisu. Nilisikia nguvu yote inaisha kabisa.”

Kama ungekuwa Annette, ungefanya nini?

WAZA KIDOGO!

Hata kama uko tayari, pengine wakati unatembea usiku, mambo ya mubaya yanaweza kukufikia. Biblia inasema hivi: “Si wenye mbio wanaoshinda katika mbio, . . . wala wenye ujuzi wanaopata kibali; kwa sababu wakati na tukio lisilotazamiwa huwapata wote.”—Mhubiri 9:11.

Vijana fulani, kama vile Annette, wanalalwa kinguvu na mutu mwenye hawajue. Wengine wanatendewa hivyo na mutu mwenye wanajua ao hata mutu fulani wa familia. Wakati alikuwa na miaka kumi tu, Natalie alilalwa kinguvu na kijana mwenye alikuwa anaishi karibu nao. Anasema hivi: “Niliogopa na kusikia haya sana, na mwanzoni sikuambia hata mutu yeyote.”

HAIKO KOSA LAKO

Annette anaendelea kujisikia kama mambo yenye yalimupata ni kosa lake. Anasema hivi: “Ninaendelea kukumbuka sana mambo yenye yalinipata siku hiyo. Ninawaza kama nilipaswa kuongeza nguvu zaidi ili kumuzuia asinitendee mubaya. Kusema kweli, kisha kunichoma kisu, niliogopa sana. Singeweza kufanya jambo lingine, lakini ninawaza kama nilipaswa kufanya jambo fulani.”

Natalie pia anaendelea kujisikia kama ni kosa lake. Anasema hivi: “Sikupaswa kujitumainia sana. Wazazi wangu walisema kwamba tulipaswa kuwa pamoja na dada yangu wakati tunachezea inje, lakini sikutii. Kwa hiyo, ninajisikia kama nilimupatia jirani yetu nafasi ya kunitendea mubaya. Watu wa familia yangu walihuzunika sana kwa sababu ya jambo lenye lilinipata, na ninaona kama ni mimi nilifanya wajisikie hivyo. Ninaendelea kuhangaishwa na jambo hilo sana.”

Ikiwa unajisikia kama vile Annette ao Natalie, kumbuka kwamba mutu mwenye alilalwa kinguvu haiko yeye alipenda kutendewa hivyo. Watu fulani wanafanya jambo hilo lionekane kuwa haliko la mubaya kabisa, na wanasema kama ni jambo la kawaida kwa wanaume kutenda hivyo ao kwamba watu wenye walitendewa hivyo ndio walipenda jambo hilo liwafikie. Lakini, hakuna mutu mwenye anapaswa kulalwa kinguvu. Kama ulitendewa ubaya huo, haiko kosa lako!

Kwa kweli, ni mwepesi kusoma maneno “haiko kosa lako”; lakini inaweza kuwa nguvu kuamini maneno hayo. Watu fulani wanaficha namna wanajisikia kuhusu mambo yenye yaliwafikia na wanawaza kama ni kosa lao na wako na mawazo mengine yenye hayafae. Lakini, kama unakataa kusema, ni nani anapata faida? Wewe ao mutu mwenye alikutendea mubaya? Ni muzuri ufikirie jambo lingine.

SEMA MAMBO YENYE YALIKUFIKIA

Biblia inatuambia kama wakati mwanaume mwaminifu Ayubu alikuwa na uchungu, alisema hivi: “Nitasema kwa uchungu wa nafsi yangu!” (Ayubu 10:1) Unaweza kupata faida kwa kufanya hivyo pia. Kumuambia mutu mwenye unatumania mambo yenye kukuhangaisha kunaweza kukusaidia ukubali hali yako na kukutuliza.

Mahangaiko yako yanaweza kuwa mazito sana ili kuyabeba peke yako. Sababu gani usimuambie mutu fulani mahangaiko yako ili akusaidie?

Annette aliona kwamba ni muzuri kusema. Anasema hivi: “Nilimuambia rafiki yangu wa sana, na rafiki huyo alinishauri nizungumuze na wazee fulani Wakristo wa kutaniko letu. Niko na furaha kwa sababu nilifanya hivyo. Tulizungumuza nao mara nyingi na waliniambia mambo yenye nilikuwa nayo lazima kusikia. Waliniambia kwamba mambo yenye yalitokea haikuwa kosa langu. Sikufanya hata kosa moja.”

Natalie aliambia wazazi wake jambo lenye lilimufikia. Anasema hivi: “Walinisaidia sana. Walinitia moyo kuzungumuzia jambo hilo, na hilo lilinisaidia nisikuwe na huzuni wala hasira.”

Natalie alipata musaada pia kupitia sala. Anasema hivi: “Kuzungumuza na Mungu kulinisaidia, zaidi sana wakati singeweza kuambia mutu mwengine. Kupitia sala, ninaweza kusema bila kuogopa. Sala inanisaidia kuwa na amani ya kweli na utulivu.”

Na wewe pia unaweza kutambua kama kuna “wakati wa kuponya.” (Mhubiri 3:3) Hangaikia afya yako na namna unajisikia. Pumuzika muzuri. Na zaidi ya yote, umutumainie Yehova, Mungu wa faraja yote.—2 Wakorintho 1:3, 4.

WAKATI UKO NA MIAKA YA KUANZA URAFIKI WA KIMAPENZI

Kama uko kijana mwanamuke na kuna mutu mwenye anataka kukuingiza katika mwenendo muchafu, sema bila muzaha, “Usifanye hivyo!” ao, “Uniache!” Usiogope kwamba utapoteza rafiki yako mwanaume. Kama yeye anapenda tu mufanye mambo ya mubaya, ujue kama hakustahili! Uko na lazima ya mwanaume mwenye anaheshimu mwili wako na kanuni zenye kukuongoza.

MAULIZO KUHUSU KUSUMBULIWA ILI UFANYE UASHERATI

“Wakati nilikuwa kwenye masomo ya musingi, vijana wanaume walikuwa wanakokota soutien yangu na kutumia maneno ya kunishushia heshima, kama vile kuniambia nitajisikia muzuri sana wakati nitalala nao.”—Coretta.

Unawaza vijana hao walikuwa:

  1. Wanafanya naye muzaha?

  2. Wanamuchezea kimapenzi?

  3. Wanamusumbua ili afanye nao uasherati?

“Wakati nilikuwa ndani ya motokari, kijana mumoja mwanaume alianza kuniambia mambo machafu na kunikamata-kamata. Nilisukuma kwa nguvu mukono wake na kumuambia aniache. Aliniona kama mutu mwenye hana akili.”—Candice.

Unawaza kijana huyo alikuwa anamufanyia nini Candice?

  1. Alikuwa anafanya naye muzaha?

  2. Alikuwa anamuchezea kimapenzi?

  3. Alikuwa anamusumbua ili afanye naye uasherati?

“Mwaka jana, kijana mumoja mwanaume aliendelea kuniambia kama ananipenda na kama alitaka tutoke pamoja naye, hata kama niliendelea kumuambia hapana. Wakati fulani, aligusa-gusa mukono wangu. Nilimuambia aache, lakini aliendelea. Kisha, wakati nilikuwa ninafunga kamba ya viatu, alinipiga kwenye makalio (fesses).”—Bethany.

Unawaza kijana huyo alikuwa:

  1. Anafanya naye muzaha?

  2. Anamuchezea kimapenzi?

  3. Anamusumbua ili afanye naye uasherati?

Jibu la muzuri kwa maulizo hayo yote tatu ni C.

Kuko tofauti gani kati ya kusumbua mutu fulani ili afanye uasherati na kumuchezea kimapenzi ao kufanya naye muzaha?

Ni mutu mumoja tu ndiye anasumbua mwengine ili afanye naye

uasherati. Anaendelea kufanya hivyo hata kama mutu mwenye

kusumbuliwa anamuambia aache.

Kusumbuliwa ili kufanya uasherati haliko jambo la muchezo.

Jambo hilo linaweza kufanya mutu afikie kulalwa kinguvu.