Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

1

Mungu Aliumba Mbingu na Dunia

Mungu Aliumba Mbingu na Dunia

Yehova Mungu njo Muumbaji wetu. Aliumba vitu vyote, vyenye tunaweza kuona na vyenye hatuwezi kuona. Mbele ya kuumba vitu vyenye tunaona, aliumba malaika wengi sana. Malaika ni nani? Malaika ni watu wenye Yehova aliumba wenye kumufanana. Hatuwezi kuwaona sawa vile tu hatuwezi kumuona Mungu. Malaika wa kwanza mwenye Yehova aliumba alimusaidia kuumba nyota, sayari (planètes), na vitu vingine vyote. Dunia, fasi yetu ya muzuri sana ya kuishi, iko kati ya zile sayari.

Kisha, Yehova alitayarisha dunia juu watu na wanyama waishi ndani. Alifanya mwangaza wa jua uangazie dunia. Aliumba milima, bahari, na mitoni.

Kisha alifanya nini tena? Yehova alisema: ‘Nitaotesha majani, mimea, na miti.’ Miti ya matunda ya namna mbalimbali, mboga za majani, na maua vikaanza kuota. Kisha, Yehova akaumba wanyama wote: wenye kuruka, wenye kuogelea, wenye kutembea, na wenye kujikokota. Aliumba wanyama wa kidogo-kidogo sawa vile sungura (lapin), na wanyama wakubwa-wakubwa sawa vile tembo. Unapendaka munyama gani?

Kisha, Yehova akamuambia ule malaika wa kwanza: “Tufanye mutu.” Watu wangekuwa tofauti na wanyama. Wangeweza kufanya vitu, kuzungumuza, kucheka, na kusali. Wangechunga dunia na wanyama. Unajua mutu wa kwanza alikuwa nani? Tutaona mu hadisi ya kufuata.

“Katika mwanzo Mungu aliumba mbingu na dunia.”​—Mwanzo 1:1