Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

2

Mungu Aliumba Mwanaume na Mwanamuke wa Kwanza

Mungu Aliumba Mwanaume na Mwanamuke wa Kwanza

Yehova alifanya bustani fasi kwenye kuliitwa Edeni. Mu ile bustani mulikuwa maua, wanyama, na miti ya mingi. Kisha, Mungu aliumba mwanaume wa kwanza Adamu, kwa kutumia mavumbi na alipuliza katika matundu ya pua yake pumuzi. Unajua nini ilitokea? Ule mutu akakuwa muzima! Yehova alipatia Adamu kazi ya kuchunga ile bustani, na kazi ya kupatia wanyama wote majina.

Yehova alimupatia Adamu sheria ya lazima sana. Alimuambia: ‘Unaweza kula matunda ya miti yote, lakini usikule matunda ya muti moja. Ukikula matunda ya ule muti utakufa.’

Kisha, Yehova akasema: ‘Nitafanyia Adamu musaidizi.’ Mungu akamulalisha Adamu usingizi muzito, kisha akakamata mbavu moja ya Adamu na akamuumbia bibi. Jina la ule mwanamuke lilikuwa Eva. Adamu na Eva wakakuwa familia ya kwanza. Adamu alijisikia namna gani wakati aliona bibi yake? Alifurahi sana na kusema: ‘Yehova ameumba mwanamuke kutoka katika mbavu yangu! Huyu ni wa kunifanana kabisa.’

Yehova akaambia Adamu na Eva wazae watoto na wajaze dunia. Alitaka wafurahie kufanya kazi pamoja, na kufanya dunia yote ikuwe paradiso, ao shamba la muzuri, sawa vile bustani ya Edeni. Lakini hawakuweza kufanya dunia ikuwe paradiso. Unajua ni juu ya nini? Tutapata jibu mu sura ya kufuata.

“Ule mwenye aliwaumba tangu mwanzo aliwafanya mwanaume na mwanamuke.”​—Matayo 19:4