Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

3

Adamu na Eva Wanakataa Kumutii Mungu

Adamu na Eva Wanakataa Kumutii Mungu

Siku moja wakati Eva alikuwa peke yake, nyoka alisema naye. Alimuuliza hivi: ‘Kweli kabisa Mungu aliwakataza kula matunda ya miti yote?’ Eva alijibia hivi: ‘Tunaweza kula matunda ya miti yote, alitukataza tu matunda ya muti moja. Tukikula matunda ya ile muti, tutakufa.’ Nyoka akamuambia: ‘Hamutakufa. Kwa kweli, mukikula matunda ya ile muti, mutakuwa sawa Mungu.’ Nyoka alisema kweli? Hapana, alisema uongo. Lakini Eva aliamini ile maneno. Eva alianza kuangalia matunda ya ile muti, mupaka akaitamani. Alikula ile tunda na kisha akapatia Adamu. Adamu alijua kama wakikataa kumutii Mungu watakufa. Lakini, aliikula tu.

Kisha wakati fulani, ileile siku, Yehova alisema na Adamu na Eva. Aliwauliza juu ya nini walikataa kumutii. Eva alisema ni kosa la nyoka, na Adamu akasema ni kosa la Eva. Juu Adamu na Eva hawakumutii Yehova, aliwafukuza mu bustani. Ili wasirudie tena mu bustani, Mungu alitia malaika na upanga murefu wenye kuwaka moto mu njia ya kuingia mu bustani.

Yehova alisema atapatia malipizi ule mwenye alidanganya Eva. Haiko kabisa nyoka njo alisemaka na Eva. Yehova hakuumba nyoka na uwezo wa kusema. Ni malaika mubaya njo alifanya nyoka aseme. Alifanya vile juu amudanganye Eva. Ule malaika anaitwa Shetani Ibilisi. Wakati wenye kuja, Yehova atamuharibu Shetani ili asiendelee kudanganya watu wafanye mambo ya mubaya.

“Ibilisi . . . alikuwa muuaji tangu mwanzo, na hakusimama imara katika kweli, kwa sababu kweli haiko ndani yake.”​—Yohana 8:44, maelezo ya chini