Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

4

Aliua Mudogo Wake Juu ya Kasirani

Aliua Mudogo Wake Juu ya Kasirani

Kisha kutoka mu bustani, Adamu na Eva walizaa watoto wengi. Mutoto wao wa kwanza aliitwa Kaini, alikuwa mulimaji, na mutoto wao wa pili aliitwa Abeli, alikuwa muchungaji.

Siku moja Kaini na Abeli walimutolea Yehova zabihu. Unajua zabihu ni nini? Ni zawadi ya pekee yenye mutu anatolea Mungu. Yehova alifurahia zabihu ya Abeli, lakini hakufurahia zabihu ya Kaini. Kaini alikasirika sana. Yehova alimuambia Kaini kama, kasirani ingemusukuma afanye jambo la mubaya. Lakini, Kaini hakusikiliza.

Kuliko kusikiliza, Kaini alimuambia Abeli hivi: ‘Tuende kwenye shamba.’ Wakati walikuwa wao wawili tu mu shamba, Kaini alipiga ndugu yake na kumuua. Yehova alifanya nini? Yehova alipatia Kaini malipizi kwa kumufukuza aende mbali na familia yake. Yehova hakukubali Kaini arudie kwao.

Ile inatufundisha nini? Tunaweza kukasirika kwa sababu mambo haikuwe vile tulipenda. Tukiona kama tunaanza kukasirika ao mutu mwingine anatushauria juu ya tabia yetu ya kukasirika, tunapaswa kubadilika bila kukawia na kujikaza kutulia.

Kwa sababu Abeli alimupenda Yehova na alifanya mambo ya muzuri, Yehova angali anamukumbuka. Mungu atafufua Abeli wakati atafanya hii dunia ikuwe paradiso.

“Fanya kwanza amani na ndugu yako, na kisha urudie na utoe zawadi yako.”​—Matayo 5:24