Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

6

Watu Munane Waliokoka Garika

Watu Munane Waliokoka Garika

Noa, familia yake, na wanyama waliingia mu safina. Kisha, Yehova alifunga mulango na mvua ikaanza kunyesha. Ile mvua ilikuwa ya mingi sana na safina ilianza kuenda juu ya maji. Kisha, dunia yote ikajaa maji. Watu wote wabaya wenye walikuwa inje ya safina walikufa. Lakini Noa na familia yake walikuwa salama mu safina. Hauone kama walifurahi kwa sababu walimutii Yehova?

Mvua ilinyesha kwa siku 40 muchana na usiku, kisha ikaisha. Maji ikaanza kupunguka polepole. Ku mwisho, safina ikasimama ku mulima. Lakini, kulikuwa kungali maji ya mingi fasi yote, kwa hiyo Noa na familia yake hawakuweza kutoka mu safina palepale.

Maji iliendelea kukauka polepole. Noa na familia yake walibakia ndani ya safina zaidi ya mwaka moja. Kisha, Yehova aliwaambia watoke mu safina. Walifurahi sana kwa sababu Yehova aliwaokoa. Na ili kumushukuru, walimutolea zabihu.

Yehova alifurahia ile zabihu. Na alisema kama hataharibishaka tena vitu vyote mu dunia kupitia garika ao mvua kubwa. Ili kuonyesha kama hataharibishaka tena dunia kupitia garika, alifanya upinde wa mvua (arc-en-ciel) uonekane mu mawingu kwa mara ya kwanza. Ulishakaona upinde wa mvua?

Kisha pale, Yehova aliambia Noa na familia yake wazae watoto na kujaza dunia.

“Noa aliingia ndani ya safina; na [watu] hawakuhangaika mupaka Garika ikakuja na kuwaharibu wote.”​—Matayo 24:38, 39