7
Munara wa Babeli
Kisha Garika, wana wa Noa na bibi zao walizaa watoto mingi. Watu waliongezeka na kuenea mu dunia, kama vile Yehova alikuwa amewaambia wafanye.
Lakini watu fulani hawakumutii Yehova. Walisema: ‘Tujenge muji na sisi wote tubakie hapa. Tutajenga munara murefu sana wenye utafika mbinguni. Kisha, tutajulikana sana.’
Yehova hakufurahia mambo yenye wale watu walikuwa wanafanya, kwa hiyo aliamua kusimamisha sura ya kufuata.
kazi yao. Unajua alifanya vile namna gani? Palepale Yehova alifanya waanze kusema luga tofauti-tofauti. Juu hawangeweza kuelewana tena, kazi ilisimama. Muji wenye walikuwa wanajenga uliitwa Babeli, maana yake “Muvurugo.” Watu walianza kuenda mu maeneo mbalimbali ya dunia. Lakini, waliendelea kufanya mambo ya mubaya kule kwenye walienda kuishi. Kulikuwa watu wenye waliendelea kumupenda Yehova? Tutapata jibu mu“Kila mutu mwenye kujiinua atapatishwa haya, lakini kila mutu mwenye kujinyenyekeza atainuliwa.”—Luka 18:14