Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

9

Wanapata Sasa Mutoto!

Wanapata Sasa Mutoto!

Abrahamu na Sara walikuwa wamefanya miaka mingi sana tangu waoane. Waliacha nyumba yao ya muzuri kule Uru na walianza kuishi mu mahema. Lakini Sara hakukataa sababu alimutegemea Yehova.

Sara alipenda sana kupata mutoto. Aliambia Abrahamu: ‘Kama mutumishi wangu Hagari anazaa mutoto, ule mutoto atakuwa sawa mutoto wangu.’ Kisha wakati fulani, Hagari alizaa mutoto mwanaume; aliitwa Ishmaeli.

Kisha miaka mingi kupita, wakati Abrahamu alikuwa na miaka 99 na Sara miaka 89, wageni watatu waliwatembelea. Abrahamu aliwakaribisha ili wapumuzike chini ya muti na wakule chakula. Unajua wale wageni walikuwa nani? Walikuwa malaika! Waliambia Abrahamu: ‘Mwaka wenye kuja, wakati kama huu, wewe na bibi yako mutapata mutoto.’ Sara alikuwa mu hema yake na alikuwa anasikiliza. Alicheka mu moyo na kuwaza: ‘Ninaweza kweli kuzaa mutoto, hata kama niko muzee?’

Mwaka wenye ulifuata, Sara alizaa mutoto mwanaume, sawa vile malaika wa Yehova alimuambiaka. Abrahamu alipatia ule mutoto jina Isaka. Isaka maana yake “Kucheka.”

Wakati Isaka alikuwa na miaka karibu tano, Sara aliona Ishmaeli iko anamucheka Isaka. Kwa sababu alipenda kulinda mutoto wake, aliambia Abrahamu afukuze Hagari na Ishmaeli. Abrahamu alikataa kwanza. Lakini Yehova aliambia Abrahamu: ‘Usikilize Sara. Nitamulinda Ishmaeli. Lakini ni kupitia Isaka njo nitatimiza ahadi zangu.’

“Kwa imani Sara pia alipokea nguvu za kupata uzao, . . . kwa kuwa alimuona Ule mwenye alikuwa ameahidi kuwa ni muaminifu.”​—Waebrania 11:11