Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

12

Yakobo Alipata Uriti

Yakobo Alipata Uriti

Isaka alikuwa na miaka 40 wakati alimuoa Rebeka. Alimupenda sana. Kisha wakati fulani, wakazaa watoto wawili, mapasa wanaume.

Jina la mukubwa lilikuwa Esau, na jina la mudogo lilikuwa Yakobo. Esau alipenda kutembea-tembea, na alijua sana kuwinda wanyama. Lakini, Yakobo alipenda kubakia ku nyumba.

Ile wakati, watu walizoea kupatia mutoto wa kwanza mashamba mingi na feza mingi kisha baba yake kufa. Ile njo waliita uriti. Mu familia ya Isaka, uriti haikukuwa tu mashamba na feza. Mwenye angepewa uriti njo mwenye Yehova angetumia ili kutimiza ahadi zenye alikuwa amefanyia Abrahamu. Esau hakuona zile ahadi kuwa za maana, lakini Yakobo alijua kama zilikuwa za maana sana.

Siku moja, Esau alitoka kuwinda, na alikuwa amechoka sana. Esau alisikia harufu ya chakula tamu yenye Yakobo alikuwa anapika, kisha akamuambia: ‘Ninasikia njaa sana! Unipatie kwa ile chakula ya mwekundu!’ Yakobo akamuambia: ‘Nitakupatia, lakini uitike kwanza kama utanipatia uriti wako!’ Esau akamuambia: ‘Sina lazima ya ule uriti! Ninakupatia. Nipatie tu chakula nikule.’ Unawaza kama Esau alifanya muzuri? Hapana. Esau alipatia Yakobo kitu cha maana sana juu tu ya chakula.

Wakati Isaka alikuwa muzee sana, alipenda kumubariki mutoto wake mukubwa. Lakini, Rebeka alisaidia mutoto wao mudogo Yakobo, ili apate ile baraka. Wakati Esau alijua vile, alikasirika sana na akapanga kuua ndugu yake Yakobo. Isaka na Rebeka walitaka kulinda Yakobo, basi wakamuambia: ‘Uende uishi na Labani, mujomba wako, mupaka kasirani ya Esau itulie.’ Yakobo alisikiliza shauri la wazazi wake, na akakimbia ili Esau asimuue.

“Mutu atapata faida gani kama anapata ulimwengu muzima lakini anapoteza uzima wake? Kwa kweli, mutu anaweza kutoa nini ili apate uzima wake?”​—Marko 8:36, 37