Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

13

Yakobo na Esau Wanasikilizana

Yakobo na Esau Wanasikilizana

Yehova aliambia Yakobo kama atamulinda sawa vile alilindaka Abrahamu na Isaka. Yakobo alienda kuishi Harani. Alioa wakati alikuwa kule, akakuwa na familia kubwa, na vitu mingi.

Kisha, Yehova aliambia Yakobo hivi: ‘Rudia katika inchi yenu.’ Basi, Yakobo na familia yake wakaanza safari ya murefu ya kurudia. Wakati walikuwa mu njia, watu fulani walikuja kumuambia Yakobo hivi: ‘Ndugu yako Esau iko anakuja, na iko na wanaume 400!’ Yakobo aliogopa, aliwaza kama Esau atamutendea mubaya yeye na familia yake. Alisali hivi kwa Yehova: ‘Tafazali uniokoe ili ndugu yangu asinitendee mubaya.’ Siku yenye ilifuata, Yakobo alitumia Esau zawadi mingi. Alimutumia kondoo, mbuzi, ngombe, ngamia, na punda za mingi.

Ule usiku, wakati Yakobo alikuwa peke yake, aliona malaika! Malaika alianza kupigana naye. Walipigana mupaka asubui. Hata kama Yakobo aliumia, hakuacha kupigana. Kisha malaika akamuambia: ‘Niache niende.’ Lakini Yakobo akamujibu: ‘Sitakuacha kama haujanibariki.’

Ku mwisho malaika akamubariki Yakobo. Na Yakobo akajua kama Yehova atamulinda juu Esau asimutendee mubaya.

Asubui, Yakobo aliona kwa mbali Esau iko anakuja na wanaume 400. Yakobo aliacha familia yake nyuma, akapita mbele na kuinama mupaka chini mara saba mbele ya ndugu yake Esau. Esau alienda mbio na kumukumbatia. Wote wawili wakaanza kulia na kisha wakasikilizana. Unawaza Yehova alijisikia namna gani wakati aliona namna Yakobo alijikaza kusikilizana na ndugu yake?

Kisha, Esau alirudia kwake, na Yakobo akaendelea na safari yake. Yakobo alikuwa na watoto wanaume 12. Majina yao ni Rubeni, Simeoni, Lawi, Yuda, Dani, Naftali, Gadi, Asheri, Isakari, Zabuloni, Yosefu, na Benyamini. Mungu alitumia mumoja kati ya wale watoto, ni kusema, Yosefu, juu akomboe watu wake. Unajua alifanya vile namna gani? Acha tuone.

“Muendelee kupenda maadui wenu na kusali kwa ajili ya wale wenye kuwatesa ninyi, ili muonyeshe kuwa ninyi ni wana wa Baba yenu mwenye kuwa mbinguni.”​—Matayo 5:44, 45