Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

15

Yehova Hakumusahau Yosefu Hata Kidogo

Yehova Hakumusahau Yosefu Hata Kidogo

Wakati Yosefu alikuwa mu gereza, Farao mufalme wa Misri alilota ndoto. Hakuna mutu mwenye aliweza kufasiria maana ya zile ndoto. Mutumishi wake mumoja aliambia Farao kama Yosefu angeweza kumuelezea maana ya zile ndoto. Palepale, Farao akasema waite Yosefu.

Farao akamuuliza: ‘Unaweza kunielezea maana ya ndoto zangu?’ Yosefu akamuambia Farao hivi: ‘Inchi ya Misri itakuwa na chakula ya mingi kwa miaka saba, lakini miaka saba yenye itafuata kutakuwa njaa. Chagua mutu mwenye hekima aweke chakula ili watu wako wasikufe na njaa.’ Farao akasema: ‘Wewe njo ninachagua! Utakuwa mutu wa pili mwenye cheo kisha mimi katika inchi ya Misri!’ Nani njo alisaidia Yosefu afasirie maana ya ndoto za Farao? Yehova njo alimusaidia.

Kwa miaka saba yenye ilifuata, Yosefu alikusanya na kuweka chakula. Na kama vile Yosefu alikuwa amesema, njaa ikakuwa mu dunia yote. Watu walitoka fasi mbalimbali na kuja kuuza chakula kwa Yosefu. Yakobo, baba ya Yosefu, alisikia kama kule Misri kulikuwa chakula, kwa hiyo akatuma watoto wake kumi waende kule kuuza chakula.

Watoto wa Yakobo walienda kwa Yosefu, na palepale akawatambua. Lakini wao hawakujua kama ni Yosefu. Wakamuinamia sawa vile alilotaka wakati alikuwa mudogo. Yosefu alipenda kujua kama ndugu zake walikuwa wangali na chuki. Kwa hiyo, akawaambia: ‘Muko wapelelezi. Munapenda kujua uzaifu wa inchi yetu.’ Wakasema, ‘Hapana! Tulizaliwa watoto wanaume 12 katika inchi ya Kanaani. Ndugu yetu mumoja alishakakufa, na ndugu yetu wa mwisho alibakia na baba yetu.’ Kisha Yosefu akawaambia: ‘Muniletee ule ndugu yenu mudogo, njo nitawaamini.’ Kwa hiyo wakarudia kwa baba yao.

Wakati chakula iliisha tena, Yakobo alituma watoto wake waende tena Misri. Mara hiyo, walienda na Benyamini, ndugu yao wa mwisho. Ili kujaribu ndugu zake wakubwa, Yosefu alificha kikombe cha feza mu mufuko wa Benyamini na akasema kama walikuwa wamekiiba. Wakati watumishi wa Yosefu walipata kile kikombe mu mufuko wa Benyamini, ndugu zake walishituka. Wakamulilia Yosefu awapatie malipizi pa nafasi ya Benyamini.

Yosefu akajua sasa kama ndugu zake walikuwa wamebadilika. Yosefu hakuweza tena kujizuia. Akaanza kulia sana na kusema: ‘Mimi njo ndugu yenu, Yosefu. Baba yangu angali muzima?’ Ndugu zake walishangaa sana. Akawaambia: ‘Musijisikie mubaya juu ya mambo yenye mulinifanyiaka. Mungu alinituma huku juu niwaokoe. Sasa mufanye mbio, muende mulete baba yangu hapa.’

Wakarudia ku nyumba kumuambia baba yao ile habari ya muzuri, kisha wakamuleta Misri. Yosefu na baba yake wakakutana tena kisha miaka mingi.

“Kama hamusamehe watu makosa yao, Baba yenu pia hatawasamehe ninyi makosa yenu.”​—Matayo 6:15