Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

16

Yobu Alikuwa Nani?

Yobu Alikuwa Nani?

Mu inchi ya Usi, mulikuwa mutu mwenye alimuabudu Yehova. Aliitwa Yobu. Alikuwa na vitu mingi sana na alikuwa na familia kubwa. Alikuwa mutu muzuri, alisaidia maskini, alisaidia bibi wenye bwana zao walikuwa wamekufa, na watoto wenye hawakukuwa na wazazi. Lakini, ni kusema kama hangepataka magumu juu alikuwaka anafanya mambo ya muzuri?

Yobu hakujua kama Shetani Ibilisi alikuwa anamuangalia. Yehova alimuuliza Shetani hivi: ‘Umeona mutumishi wangu Yobu? Hakuna mutu mwenye iko sawa yeye mu dunia. Ananisikilizaka na anafanyaka mambo ya muzuri.’ Shetani akamujibu: ‘Ni kweli Yobu anakutii. Unamulinda na kumubariki. Umemupatia vitu mingi na wanyama. Umunyanganye vile vitu vyote, na ataacha kukuabudu.’ Yehova akamuambia: ‘Unaweza kujaribu Yobu. Lakini usimuue.’ Juu ya nini Yehova aliacha Shetani ajaribu Yobu? Alikuwa hakika kama Yobu angeendelea kuwa muaminifu.

Shetani alianza kuletea Yobu majaribu mbalimbali. Kwanza, alituma watu fulani wenye kuitwa Wasabea ili waibe ngombe na punda za Yobu. Kisha, moto ukaua kondoo zote za Yobu. Watu wengine wenye kuitwa Wakaldayo, waliiba ngamia zake. Wakaua watumishi wenye walikuwa wanachunga wale wanyama. Kisha jaribu ya mubaya sana mu zote ikatokea. Watoto wote wa Yobu walikuwa wanajifurahisha mu nyumba. Kisha ile nyumba ikawaangukia, na wakakufa. Yobu alihuzunika sana, lakini hakuacha kumuabudu Yehova.

Shetani alitaka Yobu ateseke tena sana, kwa hiyo, akamuletea Yobu majipu ku mwili wote. Yobu alisikia maumivu sana. Hakujua juu ya nini ile mambo yote ilikuwa inamupata. Lakini, Yobu aliendelea kumuabudu Yehova. Mungu aliona ile mambo yote, na akamupenda Yobu sana.

Kisha Shetani akatuma watu tatu waende kumujaribu Yobu. Walimuambia: ‘Ulifanya zambi lakini unapenda kuificha. Njo maana Mungu anakupatia malipizi.’ Yobu alisema: ‘Sijafanya kosa hata moja.’ Lakini akaanza kuwaza kama Yehova njo alimuletea ile majaribu, na akasema kama Mungu hakumutendea kwa haki.

Kijana mumoja mwenye aliitwa Elihu alikuwa anasikiliza ile mazungumuzo bila kusema kitu. Kisha akasema: ‘Mambo yote yenye mumesema haiko ya kweli. Yehova ni mukubwa sana kupita vile tunaweza kuelewa. Hawezi kufanya mambo ya mubaya hata kidogo. Anaonaka mambo yote na anasaidiaka watu wakati wa majaribu.’

Kisha Yehova akamuuliza Yobu: ‘Ulikuwa wapi wakati niliumba mbingu na dunia? Juu ya nini unasema kama sikutendee kwa haki? Uko unasema tu, lakini haujue juu ya nini mambo ilitokea vile.’ Yobu aliitika makosa yake na kusema: ‘Nilijidanganya. Nilisikia habari zako, lakini sasa nimekujua. Unaweza kufanya mambo yote. Unihurumie juu ya maneno yote yenye nilisema.’

Wakati majaribu yake iliisha, Yehova alimuponyesha Yobu na kumupatia vitu mingi kuliko vyenye alikuwaka navyo. Yobu aliishi maisha ya murefu na ya furaha. Yehova alibariki Yobu kwa sababu alimutii hata wakati ilikuwa nguvu kufanya vile. Utafuata mufano wa Yobu kwa kuendelea kumuabudu Yehova hata kutokee nini?

“Mumesikia juu ya uvumilivu wa Yobu na mumeona matokeo yenye Yehova alileta.”​—Yakobo 5:11