Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

19

Mapigo Tatu ya Kwanza

Mapigo Tatu ya Kwanza

Waisraeli walikuwa watumwa. Wamisri waliwakaza wafanye kazi ya nguvu. Yehova alituma Musa na Haruni waambie Farao: ‘Acha watu wangu waende ili waniabudu katika jangwa.’ Kwa kiburi, Farao akasema hivi: ‘Sihangaikie ile mambo yenye Yehova anasema, na sitaacha Waisraeli waende.’ Kisha Farao akawaongezea kazi ya nguvu sana. Lakini Yehova alimufundisha Farao jambo fulani. Unajua alifanya nini? Alileta Mapigo Kumi juu ya Misri. Yehova alimuambia Musa: ‘Farao amekataa kunisikiliza. Kesho asubui atakuwa ku Muto Nile. Uende umuambie, juu amekataa kuacha watu wangu waende, maji yote ya Muto Nile itageuka damu.’ Musa alitii na akaenda kumuona Farao. Farao aliona vile Haruni alipiga maji ya Muto Nile kwa fimbo yake, na maji ikageuka damu. Samaki zikakufa, muto ukaanza kunuka, na watu hawakuweza tena kunywa maji ya Muto Nile. Lakini Farao alikataa kuacha Waisraeli waende.

Kisha siku saba, Yehova alimutuma tena Musa kwa Farao ili amuambie: ‘Kama hauache watu wangu waende, chura watajaa katika inchi yote ya Misri.’ Haruni akakamata fimbo na kunyoosha mukono wake juu kisha chura wakaanza kujaa mu inchi. Chura walijaa fasi yote mu nyumba za watu, ku vitanda, na mu masahani yao. Chura walikuwa kila fasi! Farao alimuambia Musa amuombe Yehova amalize ile pigo. Farao akasema kama ataacha Waisraeli waende. Kisha Yehova akasimamisha ile pigo, na Wamisri wakakusanya wale chura mu mafungu makubwa-makubwa. Na inchi ikaanza kunuka. Lakini kwa mara ingine tena Farao hakuacha Waisraeli waende.

Kisha pale, Yehova akamuambia Musa: ‘Uambie Haruni apige fimbo yake ku udongo, kisha mavumbi itageuka imbu.’ Palepale, imbu wakajaa kila fasi. Watu fulani wa Farao walimuambia: ‘Hii pigo inatoka kwa Mungu.’ Lakini Farao hakuacha Waisraeli waende.

“Nitawafanya wajue nguvu zangu na uwezo wangu, na watajua kwamba jina langu ni Yehova.” ​—Yeremia 16:21