Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

21

Pigo ya Kumi

Pigo ya Kumi

Musa aliambia Farao kama hangeonana naye tena. Lakini mbele atoke kwa Farao alimuambia: ‘Katikati ya usiku, kila mutoto wa kwanza katika inchi ya Misri, kuanzia mutoto wa kwanza wa Farao mupaka mutoto wa kwanza wa watumwa, atakufa.’

Yehova aliambia Waisraeli watayarishe chakula cha pekee. Alisema: ‘Muchinje kondoo dume ao mbuzi wa mwaka moja, kisha mupakae damu yake ku miimo (encadrement) ya milango ya nyumba zenu. Muchome ile nyama na kuikula na mukate yenye haina chachu. Muvae nguo na viatu na mukuwe tayari kuenda. Usiku wa leo nitawakomboa.’ Hauone kama Waisraeli walipaswa kufurahi kabisa?

Katikati ya usiku, malaika wa Yehova alipita ku kila nyumba mu inchi ya Misri. Mutoto wa kwanza wa kila nyumba yenye haikupakaliwa damu ku miimo ya mulango, alikufa. Lakini ule malaika aliacha nyumba zenye zilikuwa zimepakaliwa damu. Kila mutoto wa kwanza alikufa mu kila familia ya Wamisri, za matajiri na maskini. Lakini hakuna mutoto Mwisraeli mwenye alikufa.

Hata mutoto wa Farao alikufa. Farao hakuweza kuvumilia tena. Palepale akaambia Musa na Haruni: ‘Musimame. Mutoke hapa. Muende muabudu Mungu wenu. Mukamate wanyama wenu na muende!’

Ule usiku wenye Waisraeli walitoka Misri, mwezi ilikuwa yote muviringo. Walikuwa wamepangwa kulingana na familia na makabila yao. Kulikuwa wanaume Waisraeli 600000, na wanamuke na watoto wengi. Na watu wengine wengi walienda pamoja nao ili wamuabudu Yehova. Sasa Waisraeli walikuwa huru kabisa!

Ili kukumbuka vile Yehova aliwakomboa, kila mwaka walikuwa wanatayarisha ile chakula ya pekee, yenye inaitwa Pasaka.

“Kwa sababu hii nimekuacha ubakie: ili nionyeshe nguvu zangu kuhusiana na wewe na ili jina langu litangazwe katika dunia yote.”​—Waroma 9:17