Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

22

Muujiza ku Bahari Nyekundu

Muujiza ku Bahari Nyekundu

Wakati Farao alisikia kama Waisraeli wametoka Misri, aliona kama amefanya kosa kuwaacha waende. Aliambia maaskari wake hivi: ‘Mutayarishe magari ya vita na tuwafuate! Hatukupaswa kuwaacha waende.’ Farao na wanaume wake wakaanza kufuata Waisraeli.

Muchana Yehova aliongoza watu wake kupitia wingu na usiku kupitia nguzo la moto. Aliwaongoza mupaka ku Bahari Nyekundu, na kuwaambia watie kambi pale.

Kisha Waisraeli wakaona Farao na maaskari wake wako wanawafuata. Walijikuta katikati. Ngambo moja bahari, na ngambo ingine maaskari wa Misri. Wakaanza kumulilia Musa na kusema, ‘Tutakufa! Ungetuacha Misri.’ Lakini Musa akawaambia: ‘Musiogope. Mungoje mutaona vile Yehova atatuokoa.’ Musa alimutumainia kabisa Yehova, haiko vile?

Yehova akawaambia Waisraeli watoshe kambi na wajitayarishe kuondoka. Ule usiku, Yehova akaleta wingu na kuitia katikati ya Wamisri na Waisraeli. Kukakuwa giza ngambo ya Wamisri, lakini ngambo ya Waisraeli kulikuwa mwangaza.

Yehova akamuambia Musa anyooshe mukono wake juu ya bahari. Kisha Yehova akafanya upepo wenye nguvu upite usiku wote. Bahari ikagawanyika mara mbili na kukakuwa njia katikati. Waisraeli wakapita katikati ya bahari juu ya udongo wenye kukauka, maji ilikuwa kama ukuta hii ngambo, na ile ngambo ingine.

Maaskari wa Farao wakafuata Waisraeli mu ile njia katikati ya bahari. Kisha Yehova akavuruga wale maaskari. Magurudumu ya magari yao ya vita ikaanza kutoka. Wale maaskari wakalalamika na kusema: ‘Tutoke hapa, kwa sababu Yehova anapigania Waisraeli!’

Yehova akaambia Musa: ‘Nyoosha mukono wako juu ya bahari.’ Palepale kuta za maji zikaangukia maaskari wa Misri. Farao na wanaume wake wote wakakufa. Hakuna mwenye alipona.

Ile ngambo ingine ya bahari, watu mingi walikuwa wanamusifu Mungu na kuimba hivi: ‘Tumuimbie Yehova, kwa maana ametukuzwa sana. Farasi na mupandaji wake amewatupa katika bahari.’ Wakati watu walikuwa wanaimba, wanamuke walikuwa wanacheza dansi, na walikuwa wanapiga ngoma. Kila mutu alifurahi sana kwa sababu sasa walikuwa huru kabisa.

“Ili tukuwe hodari na kusema: ‘Yehova ni musaidizi wangu; sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunifanya nini?’”​—Waebrania 13:6