Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

25

Wanajenga Tabenakulo

Wanajenga Tabenakulo

Wakati Musa alikuwa ku Mulima Sinai, Yehova alimuambia ajenge hema ya pekee yenye inaitwa tabenakulo. Pale njo Waisraeli wangekuwa wanamuabudu Mungu. Na wangekuwa wanabeba ile hema fasi yote kwenye walienda.

Yehova alisema: ‘Uambie watu watoe michango ya kujenga tabenakulo.’ Waisraeli wakatoa zahabu, feza, shaba, majiwe ya bei, na vitu vingine vya bei vya kujipamba. Tena walitoa manyoya ya kondoo, vitambaa vya rangi nyekundu, ngozi za wanyama, na vitu vingine vya mingi. Waliendelea kutoa vitu mingi sana mupaka Musa akasema: ‘Michango inaenea! Musitoe tena.’

Wanaume na wanamuke mingi wenye ufundi walisaidia kujenga tabenakulo. Yehova aliwapatia akili ya kufanya ile kazi. Wamoja walitengeneza nyuzi na vitambaa, ao kupamba vitambaa. Wengine walitayarisha majiwe, zahabu, na mbao.

Watu walijenga tabenakulo sawa vile Yehova aliwaambia. Waliweka pazia (rideau) ya muzuri juu ya kugawanya tabenakulo mu sehemu mbili: Patakatifu na Patakatifu Zaidi. Mu Patakatifu Zaidi mulikuwa sanduku la agano lenye lilitengenezwa na mbao za muti wa mugunga na zahabu. Mu Patakatifu mulikuwa kitu cha kuwekea taa ya zahabu, mulikuwa meza, na mazabahu ya kuchomea uvumba. Mu kiwanja mulikuwa beseni ya shaba na mazabahu kubwa. Sanduku la agano lilikumbusha Waisraeli ahadi yenye walifanyaka ya kusema kama watamutii Yehova. Unajua agano ni nini? Ni ahadi fulani ya pekee.

Yehova alichagua Haruni na watoto wake wakuwe makuhani ku tabenakulo. Walipaswa kuichunga muzuri na kumutolea Yehova zabihu. Ni Haruni tu njo alikuwa na ruhusa ya kuingia Patakatifu Zaidi juu yeye njo alikuwa kuhani mukubwa. Aliingia Patakatifu Zaidi mara moja kila mwaka juu atoe zabihu kwa ajili ya zambi zake, zambi za familia yake, na zambi za taifa lote la Israeli.

Waisraeli walimaliza kujenga tabenakulo mwaka moja kisha kutoka Misri. Sasa walipata fasi kwenye wangemuabudu Yehova.

Yehova alionyesha kama anakubali tabenakulo. Kwa hiyo alifanya wingu likuwe juu ya ile tabenakulo. Wakati wingu liliendelea kuwa juu ya tabenakulo, Waisraeli hawakutoka kwenye walikuwa wametia kambi. Lakini wakati wingu lilitoka juu ya tabenakulo, Waisraeli walijua kama ilikuwa wakati wa kuenda. Walibomoa tabenakulo na kufuata lile wingu.

“Halafu nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha ufalme ikisema: ‘Angalia! Hema ya Mungu iko pamoja na wanadamu, na atakaa pamoja nao, na watakuwa watu wake. Na Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao.’”​—Ufunuo 21:3