Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

26

Wapelelezi 12

Wapelelezi 12

Waisraeli walitoka ku Mulima Sinai na kusafiri mu jangwa la Parani mupaka wakafika fasi yenye kuitwa Kadeshi. Wakati walifika kule, Yehova akaambia Musa: ‘Chagua watu 12, mutu mumoja mu kila kabila. Uwatume wapeleleze katika inchi ya Kanaani, yenye nitapatia Waisraeli.’ Kwa hiyo, Musa akachagua wanaume 12 na kuwaambia: ‘Muende katika inchi ya Kanaani muchunguze kama udongo wake unakomalishaka chakula. Muangalie kama watu wa ile inchi ni wazaifu ao kama wako na nguvu na kama wanaishi mu mahema ao mu miji.’ Wale wapelelezi 12 wakaenda Kanaani. Kati yao kulikuwa Yoshua na Kalebu.

Kisha siku 40, wale wapelelezi wakarudia na matunda ya tini, makomamanga, na zabibu. Wale wapelelezi wakasema: ‘Ni inchi ya muzuri, lakini watu wenye wanakaa ndani wako na nguvu na miji yake iko na kuta za murefu sana.’ Kisha Kalebu akasema: ‘Tunaweza kupata ushindi. Tuende mara moja!’ Unajua ni juu ya nini Kalebu alisema vile? Ni juu yeye na Yoshua walimutegemea Yehova. Lakini wale wapelelezi wengine kumi wakasema: ‘Hapana! Wale watu ni warefu na wanene! Tulikuwa kama panzi mbele yao.’

Waisraeli walivunjika moyo. Wakaanza kulalamika na kuambiana: ‘Tuchague kiongozi mwengine aturudishe Misri. Juu ya nini tujipeleke katika hatari ili tukufe?’ Yoshua na Kalebu wakasema: ‘Mumutii Yehova, na musiogope. Yehova atatulinda.’ Lakini Waisraeli hawakusikiliza. Walianza hata kutafuta kuua Yoshua na Kalebu!

Yehova alifanya nini? Aliambia Musa: ‘Nimefanyia Waisraeli mambo ya mingi, lakini hawanitii. Njo maana watafanya miaka 40 mu hii jangwa na watakufia humu. Watoto wao, na Yoshua, na Kalebu njo tu wataishi katika inchi yenye nilisema nitawapatia.’

“Sababu gani munaogopa sana, ninyi wenye imani kidogo?”​—Matayo 8:26