Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

27

Walimuasi Yehova

Walimuasi Yehova

Kisha muda fulani, wakati Waisraeli walikuwa wangali mu jangwa, Kora, Datani, Abiramu, na watu wengine 250 walimuasi Musa. Walimuambia: ‘Umetuchokesha! Juu ya nini tuendelee kuongozwa na wewe tu? Na juu ya nini Haruni tu njo kuhani mukubwa? Yehova iko katikati yetu sisi wote, haiko tu wewe na Haruni.’ Ile maneno haikumufurahisha Yehova. Aliona kama walimuasi yeye!

Musa akaambia Kora na watu wenye walikuwa wanamuunga mukono: ‘Kesho mukuje kwenye tabenakulo, na mukuje na vyombo vyenye vinajaa uvumba. Yehova atatuonyesha kama amechagua nani.’

Siku yenye ilifuata, Kora na wale wanaume 250 wakaenda kukutana na Musa ku tabenakulo. Hawakukuwa makuhani, lakini wakachoma uvumba. Yehova akaambia Musa na Haruni: ‘Mujitenge na Kora na wale wenye kumuunga mukono.’

Datani, Abiramu, na familia zao walikataa kufuata Kora ku tabenakulo. Yehova akaambia Waisraeli wasikaribie mahema ya Kora, Datani, na Abiramu. Bila kukawia, Waisraeli wakaenda mbali nao. Datani, Abiramu, na familia zao wakasimama inje ya mahema yao. Palepale, inchi ikapasuka na kuwameza! Ku tabenakulo, moto ukashuka na kuunguza Kora na wale wanaume 250 wenye walikuwa pamoja naye.

Kisha Yehova akaambia Musa: ‘Ambia kiongozi wa kila kabila akupatie fimbo moja. Kisha uandike jina la kila kiongozi kwenye fimbo yake. Lakini uandike jina la Haruni kwenye fimbo ya kabila la Lawi. Uweke zile fimbo katika tabenakulo, na fimbo ya mutu mwenye nitachagua itaota maua.’

Siku yenye ilifuata, Musa akatosha fimbo zote na akazionyesha viongozi. Fimbo ya Haruni ilikuwa na maua ya kukomaa na matunda ya kuivya. Ni vile Yehova alionyesha kama alikuwa amechagua Haruni akuwe kuhani mukubwa.

“Mutii wale wenye wanaongoza kati yenu na munyenyekee.”​—Waebrania 13:17