Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

28

Punda ya Balaamu Inasema

Punda ya Balaamu Inasema

Waisraeli walikuwa wamefanya karibu miaka 40 mu jangwa. Walikuwa wamepata ushindi juu ya miji ya mingi. Sasa, walikuwa wametia kambi yao mu maeneo ya Moabu yenye haina milima, upande wa mashariki wa Muto Yordani. Wakati wa kuingia mu Inchi ya Ahadi ulifika. Balaki, mufalme wa Moabu, aliogopa. Aliwaza kama watamunyanganya inchi yake. Njo maana aliomba mwanaume mwenye kuitwa Balaamu akuje Moabu ili alaani Waisraeli.

Lakini Yehova akaambia Balaamu: ‘Usilaani Waisraeli.’ Kwa hiyo, Balaamu akakataa kuenda. Mufalme Balaki akamuita mara ya pili na akasema kama atamupatia kila kitu chenye anataka. Lakini Balaamu akakataa tena. Kisha Mungu akamuambia: ‘Unaweza kuenda, lakini utasema tu maneno yenye nitakuambia useme.’

Balaamu akapanda juu ya punda yake na akaanza safari ya kuenda Moabu. Alikuwa amepanga kulaani Waisraeli, hata kama Yehova alimuambia asifanye vile. Malaika wa Yehova akamutokea mu njia mara tatu. Balaamu hakuona ule malaika, lakini punda wake ilimuona. Mara ya kwanza, punda akatoka mu njia na akaingia mu shamba. Mara ya pili, punda akajifinya ku ukuta wa majiwe na kufinya muguu wa Balaamu ku ule ukuta. Mara ya mwisho, punda akalala katikati ya njia. Mara yote tatu, Balaamu alikuwa anapiga punda wake fimbo.

Kisha kumupiga mara ya tatu, Yehova akafanya punda aseme. Punda akauliza Balaamu: ‘Juu ya nini unaendelea kunipiga?’ Balaamu akasema: ‘Umenifanya nionekane sawa pumbafu. Kama nilikuwa na mupanga ningekuua.’ Punda akasema: ‘Nimekubeba miaka mingi. Kuko siku nilishaka kukutendea hivi?’

Kisha Yehova akawezesha Balaamu aone malaika. Malaika akasema: ‘Yehova alikuambia usiende kulaani Waisraeli.’ Balaamu akasema: ‘Nimefanya makosa. Nitarudia kwenye nyumba.’ Lakini malaika akasema: ‘Unaweza kuenda Moabu, lakini useme tu mambo yenye Yehova atakuambia.’

Balaamu alijifunza jambo fulani? Hapana. Kisha pale, Balaamu alijaribu tena kulaani Waisraeli mara tatu, lakini mara yote tatu Yehova akamulazimisha awabariki. Ku mwisho, Waisraeli walipigana na Moabu, na wakaua Balaamu. Hauone kama ingekuwa muzuri Balaamu amusikilize Yehova tangu mwanzo?

“Mujilinde na kila namna ya pupa, kwa sababu hata wakati mutu iko na vitu vingi, uzima wake hautokane na vitu vyenye iko navyo.”​—Luka 12:15