Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

29

Yehova Alichagua Yoshua

Yehova Alichagua Yoshua

Kisha kuongoza taifa la Israeli kwa miaka mingi, Musa alikuwa karibu kufa. Yehova akamuambia: ‘Haiko wewe njo utaingiza Waisraeli katika Inchi ya Ahadi. Lakini nitakuonyesha ile inchi.’ Kisha Musa akamuomba Yehova achague kiongozi mupya juu aongoze watu. Yehova akamuambia: ‘Uende kwa Yoshua umuambie yeye njo atakuwa kiongozi.’

Musa akaambia taifa lote kama iko karibu kufa na kama Yehova amechagua Yoshua ili akuwe kiongozi mwenye atawaingiza mu Inchi ya Ahadi. Kisha Musa akaambia Yoshua: ‘Usiogope. Yehova atakusaidia.’ Wakati kidogo kisha pale, Musa akapanda juu ya Mulima Nebo, na kule Yehova akamuonyesha inchi yenye alikuwa ametoa ahadi kama ataipatia Abrahamu, Isaka, na Yakobo. Musa alikuwa na miaka 120 wakati alikufa.

Yehova akaambia Yoshua: ‘Vuka Muto Yordani, na uingie Kanaani. Nitakusaidia sawa vile nilisaidia Musa. Usome Sheria yangu kila siku. Usiogope. Ukuwe hodari. Uende, na ufanye mambo yote yenye nimekuambia.’

Yoshua akatuma wapelelezi wawili waende katika muji wa Yeriko. Mu hadisi ya kufuata, tutaona jambo lenye lilitokea kule. Wakati walirudia, walisema kama ilikuwa wakati wa muzuri wa kuingia Kanaani. Siku yenye ilifuata, Yoshua akaambia taifa lote lijitayarishe kuenda. Kisha akaambia makuhani wenye walikuwa wanabeba sanduku la agano wapite mbele ya taifa na waingie katika Muto Yordani. Muto ulikuwa umejaa maji. Lakini wakati tu miguu ya makuhani ilikanyanga mu maji, muto ikaacha kuteremuka, na maji ikaanza kukauka! Wakati makuhani walifika katikati ya muto wakasimama wakati taifa lote la Israeli lilikuwa linavuka ngambo ingine. Unawaza kama ule muujiza uliwakumbusha jambo lenye Yehova aliwafanyiaka ku Bahari Nyekundu?

Kisha ile miaka yote, Waisraeli waliingia sasa mu Inchi ya Ahadi. Sasa wangeweza kujenga nyumba na miji, kulima mashamba ya chakula, ya mizabibu, na ya matunda. Ile inchi ilikuwa na maziwa na asali mingi.

“Yehova atakuongoza sikuzote na kukushibisha hata katika inchi yenye kukauka.”​—Isaya 58:11