Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

30

Rahabu Alificha Wapelelezi

Rahabu Alificha Wapelelezi

Wakati wapelelezi Waisraeli walienda Yeriko, waliingia mu nyumba ya mwanamuke mwenye kuitwa Rahabu. Wakati mufalme wa Yeriko alijua, alituma maaskari ku nyumba ya Rahabu. Lakini Rahabu alificha wale wapelelezi wawili ku sehemu ya juu ya nyumba yake na akatuma wale maaskari mu njia ingine. Kisha Rahabu akaambia wale wapelelezi: ‘Nitawasaidia juu ninajua kama Yehova iko pamoja na ninyi na mutakamata hii inchi. Tafazali, munitolee ahadi kama mutaokoa familia yangu.’

Wapelelezi wakaambia Rahabu: ‘Tunakutolea ahadi kama hakuna mutu ndani ya nyumba yako mwenye ataumia. Funga kamba nyekundu kwenye dirisha, na watu wa familia yako wataokolewa.’

Rahabu akashusha wale wapelelezi kupitia dirisha kwa kutumia kamba. Wakaenda kujificha ku milima siku tatu mbele ya kurudia kwa Yoshua. Kisha Waisraeli wakavuka Muto Yordani na kujitayarisha kukamata inchi. Yeriko ilikuwa muji wa kwanza wenye walikamata. Yehova aliwaambia wazunguke muji mara moja kila siku kwa siku sita. Siku ya saba, walizunguka muji mara saba. Kisha makuhani wakapiga tarumbeta, na maaskari wakalalamika kwa nguvu yao yote. Kuta za ule muji zikaanguka! Lakini nyumba ya Rahabu, yenye ilikuwa ku ukuta haikuanguka. Rahabu na familia yake waliokolewa kwa sababu alimutegemea Yehova.

“Vilevile, je, Rahabu . . . hakutangazwa pia kuwa mwenye haki kupitia matendo, kisha kukaribisha muzuri wale wajumbe na kuwatosha inje kupitia njia ingine?”​—Yakobo 2:25