Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

31

Yoshua na Wagibeoni

Yoshua na Wagibeoni

Habari juu ya kuanguka kwa Yeriko ilienea sana mu mataifa ingine ya Kanaani. Wafalme wa ile mataifa wakasikilizana juu wapigane na Waisraeli. Lakini Wagibeoni wakachagua kufanya jambo lingine. Wakavaa manguo ya kupasuka-pasuka na wakaenda kuonana na Yoshua, wakamuambia: ‘Tumetoka katika inchi ya mbali sana. Tumesikia habari juu ya Yehova na mambo yote yenye aliwafanyia wakati mulikuwa Misri na Moabu. Kama munatutolea ahadi kuwa hamutapigana na sisi, tutakuwa watumishi wenu.’

Yoshua aliamini mambo yenye walisema na akawaambia kama hatapigana nao. Kisha siku tatu, akavumbua kama hawakutoka mu inchi ya mbali, walitoka Kanaani. Yoshua akauliza Wagibeoni: ‘Juu ya nini mulitudanganya?’ Wakamujibu: ‘Tuliogopa! Tunajua kama Yehova Mungu wenu iko anawapigania. Tafazali, musituue.’ Yoshua akatimiza mambo yenye aliwaambia, akawaacha waendelee kuishi.

Kisha wakati kidogo, wafalme tano Wakanaani na maaskari wao wakatuma habari za kuogopesha za kusema kama watapigana na Wagibeoni. Yoshua na maaskari wake walitembea usiku muzima juu waende kuokoa Wagibeoni. Vita ikaanza asubui sana siku ya kufuata. Wakanaani walianza kukimbia ngambo zote. Kila fasi kwenye walikimbilia Yehova aliangusha majiwe ya mukubwa-mukubwa sana juu yao. Kisha Yoshua akamuomba Yehova afanye jua isimame. Mbele ya pale, hakuna siku yenye jua ilisimamaka. Sasa, juu ya nini Yoshua aliomba Yehova afanye jua isimame? Ni juu Yoshua alikuwa anamutumainia kabisa Yehova. Jua ikasimama siku muzima mupaka wakati Waisraeli walipata ushindi juu ya wafalme Wakanaani na maaskari wao.

“Neno lenu ‘Ndiyo’ limaanishe ndiyo, na ‘Hapana’ yenu imaanishe hapana, kwa maana lenye kupita hayo linatoka kwa ule muovu.”​—Matayo 5:37