Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

32

Kiongozi Mupya na Wanamuke Mbili Wenye Uhodari

Kiongozi Mupya na Wanamuke Mbili Wenye Uhodari

Kisha kuongoza watu wa Yehova kwa miaka mingi, Yoshua alikufa na miaka 110. Wakati Yoshua alikuwa muzima, Waisraeli walimuabudu Yehova. Lakini kisha Yoshua kufa, walianza kuabudu sanamu, sawa vile Wakanaani. Kwa sababu Waisraeli hawakuendelea kumutii, Yehova aliacha mufalme Yabini wa Kanaani awatese. Watu walimulilia Yehova awasaidie. Kwa hiyo, Yehova akachagua kiongozi mupya mwenye kuitwa Baraka. Ule kiongozi angewasaidia watu wamurudilie Yehova.

Debora, nabii mwanamuke, alimuita Baraka. Wakati alifika, akamuambia kama Yehova anasema hivi: ‘Ukamate wanaume 10000, na uende kupigana na maaskari wa Yabini mu bonde la muto Kishoni. Kule utashinda Sisera, mukubwa wa maaskari wa Yabini.’ Baraka akaambia Debora: ‘Nitaenda kama tu utaenda pamoja na mimi.’ Debora akamujibu: ‘Nitaenda na wewe. Lakini ujue kama, haiko wewe njo utaua Sisera. Yehova amesema kama mwanamuke njo atamuua.’

Debora alienda pamoja na Baraka na maaskari wake ku Mulima Tabori juu wajitayarishe kupigana vita. Wakati tu Sisera alisikia vile, akakusanya magari ya vita na maaskari wake mu bonde. Debora akaambia Baraka: ‘Leo ni siku yenye Yehova atakupatia ushindi.’ Baraka na wanaume wake 10000 walitoka ku mulima na kushuka ili wapigane na maaskari wa Sisera wenye nguvu sana.

Kisha, Yehova akafanya maji ijae mu bonde la Kishoni. Magari ya vita ya Sisera ikakwama mu matope. Sisera akatoka mu gari lake na kuanza kukimbia. Baraka na maaskari wake walishinda maaskari wa Sisera, lakini Sisera alikimbia! Akaenda kujificha mu hema ya mwanamuke mwenye kuitwa Yaeli. Ule mwanamuke akamupatia maziwa akunywe, kisha akamufunika blanketi. Ule mwanaume mwenye nguvu akalala usingizi; alikuwa amechoka. Kisha, Yaeli akaingia kwenye alikuwa analala na kumupigilia musumari ya hema mu kichwa na akakufa.

Baraka alikuja kutafuta Sisera. Yaeli akatoka inje ya hema na kumuambia: ‘Ingia nikuonyeshe mwanaume mwenye uko unatafuta.’ Baraka akaingia na kukuta Sisera amekufa. Baraka na Debora wakaimbia Yehova wimbo wa kumusifu kwa sababu alikuwa amepatia Waisraeli ushindi juu ya maadui wao. Mu miaka 40 yenye ilifuata, Waisraeli waliishi mu amani.

“Wanamuke wenye kutangaza habari njema ni jeshi kubwa.”​—Zaburi 68:11