Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

33

Rutu na Naomi

Rutu na Naomi

Wakati kulikuwa njaa mu inchi ya Israeli, mwanamuke Mwisraeli mwenye kuitwa Naomi alihamia Moabu na bwana yake na watoto wake wanaume wawili. Kisha, bwana ya Naomi akakufa. Mutoto wake mumoja alioa Rutu, na mwingine alioa Orpa, wanamuke Wamoabu. Lakini, kisha wakati fulani watoto wa Naomi walikufa.

Wakati Naomi alipata habari kama njaa ilikuwa imeisha mu inchi ya Israeli, aliamua kurudia. Rutu na Orpa walienda pamoja naye, lakini, wakati walikuwa mu njia, Naomi aliwaambia hivi: ‘Mulikuwa bibi wazuri kwa watoto wangu na mulikuwa wakwe wazuri kwangu. Ninapenda muolewe tena. Murudie Moabu.’ Wakamuambia: ‘Tunakupenda sana! Hatupendi kukuacha.’ Naomi akaendelea kuwabembeleza warudie. Kisha, Orpa akarudia, lakini Rutu akabakia. Naomi akamuambia: ‘Orpa anarudia kwa watu wake na kwa miungu yake. Rudia naye, na uende ku nyumba ya mama yako.’ Lakini, Rutu akamuambia: ‘Sitakuacha. Watu wako watakuwa watu wangu, na Mungu wako Mungu wangu.’ Unawaza Naomi alijisikia namna gani wakati Rutu alimuambia vile?

Rutu na Naomi walifika Israeli mwanzo wa mavuno ya mbegu ya shayiri (orge). Siku moja, Rutu alienda kuokota mbegu ya shayiri mu shamba la mwanaume mwenye kuitwa Boazi, mwenye alikuwa mutoto wa Rahabu. Boazi alipata habari kama Rutu alikuwa Mumoabu mwenye alikataa kabisa kuachana na Naomi. Aliambia wafanyakazi wake waache mbegu fulani mu shamba juu Rutu aziokote.

Mangaribi, Naomi aliuliza Rutu: ‘Leo ulifanya kazi mu shamba la nani?’ Rutu akamujibia: ‘Mu shambala Boazi.’ Naomi akamuambia: ‘Boazi ni mutu wa jamaa ya bwana yangu. Uendelee kufanya kazi mu shamba lake pamoja na wanamuke wengine. Pale hakuna mutu mwenye atakusumbua.’

Rutu aliendelea kufanya kazi mu shamba la Boazi mupaka wakati kazi ya kuvuna iliisha. Boazi alitambua kama Rutu ni mwanamuke muzuri na mwenye bidii. Ile wakati, kama mwanaume anakufa bila kuzaa watoto, mutu wa jamaa yake alipaswa kuoa bibi yake. Basi, Boazi alioa Rutu. Wakazaa mutoto mwenye aliitwa Obedi, mwenye alifikia kuwa tate (nkambo) wa Mufalme Daudi. Marafiki wa Naomi walifurahi sana. Walimuambia: ‘Kwanza, Yehova alikupatia Rutu mwenye anakupenda sana, na sasa uko na mujukuu. Yehova asifiwe.’

“Kuko rafiki mwenye anashikamana sana na mutu kuliko ndugu.”​—Mezali 18:24