Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

34

Gideoni Alishinda Wamidiani

Gideoni Alishinda Wamidiani

Kisha wakati fulani, Waisraeli walimuacha tena Yehova na kuanza kuabudu miungu ya uongo. Kwa miaka saba, Wamidiani waliiba wanyama wa Waisraeli na kuharibisha mimea yao. Kwa hiyo, juu ya kujilinda, Waisraeli walijificha mu mapango na milima. Walimulilia Yehova awasaidie. Kwa hiyo, Yehova akatuma malaika kwa mwanaume mwenye kuitwa Gideoni. Ule malaika akamuambia: ‘Yehova amekuchagua juu ukuwe mupiganaji-vita mwenye nguvu.’ Gideoni akamuuliza: ‘Namna gani nitaweza kuokoa Waisraeli? Mimi siko kitu.’

Nini njo ingesadikisha Gideoni kama kweli Yehova alikuwa amemuhagua? Gideoni alikamata manyoya ya kondoo na kuitia chini. Kisha, alimuambia Yehova: ‘Kama kesho asubui ninakuta umande ku manyoya lakini chini kunakauka, nitajua kama umenichagua juu niokoe Waisraeli.’ Siku yenye ilifuata, manyoya ilikuwa imeloana lakini chini kulikuwa kunakauka! Kisha, Gideoni akaomba kama, asubui ya kufuata manyoya njo ikuwe ya kukauka lakini chini kukuwe umande. Wakati ilifanyika vile, Gideoni akaamini kabisa kama Yehova alikuwa amemuchagua. Basi, akakusanya maaskari wake na kuenda kupigana na Wamidiani.

Yehova akaambia Gideoni: ‘Nitapatia Waisraeli ushindi. Lakini kwa sababu uko na maaskari wengi, unaweza kuwaza kama ni kwa nguvu yenu njo mulipata ushindi. Uambie kila mutu mwenye kuwa na woga arudie ku nyumba.’ Kwa hiyo, maaskari 22000 wakarudia ku nyumba, na kukabakia maaskari 10000. Kisha, Yehova akasema: ‘Ungali na maaskari wengi sana. Uwapeleke ku muto ya kidogo na uwaambie wakunywe maji. Ubakie tu na wale wenye watakunywa maji na wako wanaangalia kama hakuna adui pembeni.’ Ni wanaume 300 tu njo walifanya vile wakati walikuwa wanakunywa. Yehova alitoa ahadi kama wale wanaume kidogo watashinda jeshi la Midiani lenye kuwa na maaskari 135000.

Usiku, Yehova aliambia Gideoni: ‘Huu njo wakati wa kushambulia Wamidiani!’ Gideoni alipatia watu wake baragumu na mitungi kubwa na alikuwa ameficha mienge (torches) ndani ya ile mitungi. Kisha, akawaambia: ‘Muniangalie na mufanye vile ninafanya.’ Kisha, Gideoni akapiga baragumu, akavunja mutungi, akanyoosha mwenge wake, na kusema: ‘Upanga wa Yehova na wa Gideoni!’ Wanaume wake 300 wakafanya vilevile. Wamidiani wakaogopa na kukimbia ovyo-ovyo kila mutu mu njia yake. Kukakuwa muvurugo, na wakaanza kuuana. Tena, Yehova alisaidia Waisraeli washinde maadui wao.

“Ili nguvu zenye kupita zile za kawaida zikuwe za Mungu, hapana zenye kutoka kwetu.”​—2 Wakorinto 4:7