Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

36

Ahadi ya Yefta

Ahadi ya Yefta

Waisraeli walimuacha tena Yehova na kuanza kuabudu miungu ya uongo. Lakini, ile miungu haikuwasaidia hata kidogo wakati Waamoni walipigana nao. Waisraeli waliteseka kwa miaka mingi. Ku mwisho, wakamuambia Yehova: ‘Tumefanya zambi. Tafazali utuokoe katika mikono ya maadui wetu.’ Kisha, wakavunja-vunja sanamu zao na wakaanza tena kumuabudu Yehova. Yehova hakupenda waendelee kuteseka.

Mupiganaji-vita mwenye kuitwa Yefta alichaguliwa juu aongoze Waisraeli. Aliambia Yehova hivi: ‘Ukitusaidia kushinda hii vita, ninakutolea ahadi kama, wakati nitarudia ku nyumba, nitakupatia mutu wa kwanza mwenye atatoka mu nyumba yangu ili kunipokea.’ Yehova alisikiliza sala ya Yefta na akamusaidia apate ushindi.

Wakati Yefta alirudia kwake, mutoto wake mwanamuke, mutoto mumoja tu mwenye alikuwa naye, njo alikuwa mutu wa kwanza mwenye alikuja kumupokea. Alikuwa anacheza dansi na kupiga ngoma. Yefta angefanya nini? Alikumbuka ahadi yake na akasema: ‘Aah, mutoto wangu! Umenivunja moyo. Nilitoa ahadi kwa Yehova. Juu niitimize, ninapaswa kukutuma mu muji wa Shilo ili utumikie ku tabenakulo.’ Binti yake akamuambia: ‘Baba, kama umetoa ahadi kwa Yehova, unapaswa kuitimiza. Ninaomba tu uniache niende ku milima na marafiki wangu wanamuke kwa miezi mbili. Kisha, nitaenda Shilo.’ Binti ya Yefta alitumikia kwa uaminifu ku tabenakulo maisha yake yote. Kila mwaka marafiki wake walikuwa wanaenda kumuona.

“Mutu mwenye anamupenda baba ao mama kuliko mimi hanistahili.”​—Matayo 10:37