Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

38

Yehova Alipatia Samsoni Nguvu

Yehova Alipatia Samsoni Nguvu

Waisraeli mingi walianza tena kuabudu miungu ya uongo. Kwa hiyo, Yehova aliacha Wafilisti wawatawale. Lakini, kulikuwa Waisraeli fulani wenye walimupenda Yehova. Mumoja wao aliitwa Manoa. Yeye na bibi yake hawakukuwa na watoto. Siku moja, Yehova alituma malaika kwa bibi ya Manoa. Malaika alimuambia: ‘Utazaa mutoto mwanaume. Atakomboa Waisraeli katika mikono ya Wafilisti. Na atakuwa Munaziri.’ Unajua Wanaziri walikuwa nani? Walikuwa watumishi wa pekee wa Yehova. Wanaziri hawakupaswa kukata nywele.

Kisha wakati fulani, bibi ya Manoa alizaa mutoto mwanaume na wakamupatia jina Samsoni. Wakati alikomaa, Yehova alimupatia nguvu mingi sana. Samsoni angeweza kuua simba kwa mikono yake tu. Wakati fulani, Samsoni aliua Wafilisti 30 yeye peke yake. Wafilisti walimuchukia na walitafuta namna ya kumuua. Siku moja, wakati Samsoni alikuwa amelala kule Gaza, Wafilisti walimungoja ku mulango mukubwa wa muji juu asubui wamukamate na kumuua. Lakini, katikati ya usiku, Samsoni aliamuka, akaenda ku mulango mukubwa wa muji, na kuungoa. Kisha, akaubeba ku mabega yake mupaka juu ya mulima wenye ulikuwa karibu na Hebroni!

Kisha, Wafilisti walienda kuonana na Delila, muchumba wa Samsoni. Walimuambia: ‘Tutakupatia feza mingi ukivumbua juu ya nini Samsoni iko na nguvu mingi sana. Tunapenda kumukamata na kumufunga mu gereza.’ Delila aliitika juu alipenda sana feza. Ku mwanzo, Samsoni alikataa kumuambia juu ya nini iko na nguvu mingi sana. Lakini, Delila aliendelea kumubembeleza mupaka Samsoni akamuambia juu ya nini iko na nguvu mingi sana. Alimuambia: ‘Nywele zangu hazijakatiwaka, juu niko Munaziri. Kama tu nywele zangu zinakatwa, sitakuwa na nguvu tena.’ Hauone kama Samsoni alifanya makosa kumuambia vile?

Mara moja, Delila akaambia Wafilisti: ‘Ninajua siri yake!’ Akamufanya alale ku magoti yake. Kisha akaita mutu amukate nywele. Kisha, Delila akasema kwa sauti kubwa: ‘Samsoni, Wafilisti wamekuja!’ Samsoni akaamuka, lakini hakukuwa tena na nguvu. Wafilisti wakamukamata, wakamutoboa macho na kumufunga mu gereza.

Siku moja, Wafilisti mingi walikusanyika mu hekalu la mungu wao Dagoni. Walikuwa wanalalamika na kusema: ‘Mungu wetu ametia Samsoni katika mikono yetu! Mulete Samsoni ili atufurahishe.’ Wakamusimamisha katikati ya nguzo mbili na kuanza kumucheka. Samsoni akasali: ‘Ee Yehova, tafazali unipatie tena nguvu, mara hii moja tu.’ Ile wakati, nywele za Samsoni zilikuwa zimekomaa tena. Samsoni akasukuma nguzo za hekalu na nguvu yake yote. Jengo lote likaanguka na kuua watu wote wenye walikuwa mu hekalu, na Samsoni naye akakufa.

“Kwa mambo yote niko na nguvu kupitia ule mwenye ananipatia nguvu.” ​—Wafilipi 4:13