Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

39

Mufalme wa Kwanza wa Israeli

Mufalme wa Kwanza wa Israeli

Yehova alikuwa amepatia Waisraeli waamuzi ili wawaongoze, lakini wao walipenda tu wakuwe na mufalme. Waliambia Samweli: ‘Mataifa yote yenye inatuzunguka iko na wafalme. Na sisi tunapenda tukuwe na mufalme.’ Samweli hakufurahia jambo hilo, basi alisali kwa Yehova. Yehova alimujibia: ‘Wale watu hawakukatae wewe. Mimi njo wanakataa. Uwaambie kama wanaweza kuwa na mufalme, lakini ule mufalme atawaomba mambo mingi.’ Hata hivyo, watu wakamujibia na kusema: ‘Tunapenda tu tukuwe na mufalme!’

Yehova aliambia Samweli kama Sauli njo atakuwa mufalme wa kwanza wa Waisraeli. Wakati Sauli alienda kuona Samweli kule Rama, Samweli alimutia mafuta, ni kusema, alimwanga mafuta ku kichwa yake juu ya kuonyesha kama Yehova amemuchagua akuwe mufalme.

Kisha, Samweli akaita Waisraeli wote juu waone mufalme wao wa mupya. Lakini, walitafuta Sauli fasi yote, lakini hawakumuona. Unajua ni juu ya nini? Ni juu alikuwa amejificha mu mizigo. Wakati walimupata, walimuleta na kumusimamisha katikati ya watu. Sauli alikuwa murefu kupita wengine wote, na alikuwa na sura ya muzuri sana. Samweli akasema: ‘Muone mwenye Yehova amechagua.’ Watu wakalalamika na kusema: ‘Mufalme aishi milele!’

Ku mwanzo, Mufalme Sauli alisikiliza Samweli na kumutii Yehova. Lakini, kisha wakati fulani, alibadilika. Kwa mufano, mufalme hakupaswa kutoa zabihu. Wakati fulani, Samweli aliambia Sauli amungojee, lakini Samweli akachelewa kufika. Basi, Sauli akaamua kutoa zabihu yeye mwenyewe. Samweli alifanya nini? Alimuambia: ‘Ulipaswa kumutii Yehova.’ Kosa la Sauli, lilimufundisha jambo fulani?

Kisha, wakati Sauli alienda kupigana na Waamaleki, Samweli alimuambia aue Waamaleki wote. Lakini, Sauli hakuua Mufalme Agagi. Yehova aliambia Samweli: ‘Sauli ameniacha, na haiko ananisikiliza tena.’ Samweli alihuzunika sana na kuambia Sauli: ‘Juu haukumutii Yehova, atachagua mufalme mwingine.’ Wakati Samweli alianza kuenda, Sauli alikamata upindo wa koti ya Samweli mupaka ikapasuka. Kisha, Samweli akaambia Sauli: ‘Yehova ametosha ufalme katika mikono yako.’ Yehova angepatia ufalme mutu mwingine mwenye angemupenda na kumutii.

“Kutii ni muzuri kuliko zabihu.”​—1 Samweli 15:22