Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

40

Daudi na Goliati

Daudi na Goliati

Yehova aliambia Samweli: ‘Uende ku nyumba ya Yese. Mumoja kati ya watoto wake atakuwa mufalme wa pili wa Israeli.’ Kwa hiyo, Samweli akaenda ku nyumba ya Yese. Wakati aliona mutoto mukubwa wa Yese, akawaza: ‘Huyu kijana njo anapaswa kuwa mufalme.’ Lakini Yehova akaambia Samweli kama hakuchagua ule kijana. Yehova akasema: ‘Mimi ninaonaka mambo yenye iko mu moyo wa mutu, hapana namna anaonekana kwa inje.’

Yese akaleta watoto wake wengine sita mbele ya Samweli. Lakini Samweli akasema: ‘Kati ya wale wote, hakuna mwenye Yehova amechagua. Uko na watoto wengine wanaume?’ Yese akasema: ‘Kungali mutoto mwingine wa mwisho, Daudi. Alienda kuchunga kondoo zangu.’ Wakati Daudi aliingia, Yehova akaambia Samweli: ‘Ule njo nimechagua!’ Samweli alimwanga mafuta ku kichwa cha Daudi juu ya kuonyesha kama atakuwa mufalme wa Israeli.

Kisha wakati fulani, Waisraeli walienda kupigana na Wafilisti. Wafilisti walikuwa na mupiganaji-vita murefu na munene mwenye alikuwa anawapigania, mwenye aliitwa Goliati. Kila siku, Goliati alikuwa anacheka Waisraeli. Alisema hivi kwa sauti kubwa: ‘Muchague mwanaume mumoja akuje tupigane naye. Kama anashinda, tutakuwa watumwa wenu. Lakini kama ninamushinda, mutakuwa watumwa wetu.’

Daudi alienda ku kambi ya Maaskari wa Israeli juu apelekee ndugu zake chakula. Ndugu zake walikuwa maaskari. Wakati alisikia maneno ya Goliati, Daudi akasema: ‘Mimi nitapigana naye!’ Mufalme Sauli akamuambia: ‘Lakini uko tu kijana.’ Daudi akamujibu: ‘Yehova atanisaidia.’

Sauli alivalisha Daudi silaha zake za vita, lakini Daudi akasema: ‘Sitaweza kupigana na hizi silaha.’ Daudi akakamata kombeo yake na kuenda ku muto. Akachagua majiwe tano yenye iko laini na kuitia mu mufuko. Kisha Daudi akakimbia juu akutane na Goliati. Ule mupiganaji-vita murefu na munene akasema hivi kwa sauti: ‘Kuja hapa, wewe kijana. Nyama yako, nitaipatia ndege wa mbinguni na wanyama wa pori.’ Daudi hakuogopa. Akajibu kwa sauti kubwa: ‘Unakuja na upanga na mukuki, lakini mimi ninakuja katika jina la Yehova. Usiwaze uko unapigana na sisi, uko unapigana na Mungu. Kila mutu mwenye iko hapa atajua kama Yehova iko na nguvu kupita upanga na mukuki. Atawatia ninyi wote katika mikono yetu.’

Daudi akatia jiwe moja mu kombeo yake na kuitupa na nguvu yake yote. Yehova akamusaidia. Ile jiwe ikapiga Goliati na kuingia ndani ya paji la uso wake. Goliati akaanguka chini na akakufa. Mara moja Wafilisti wakakimbia. Na wewe, unatumainiaka Yehova, sawa vile Daudi?

“Kwa wanadamu haiwezekane, lakini kwa Mungu inawezekana, kwa maana mambo yote yanawezekana kwa Mungu.”—Marko 10:27