Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

41

Daudi na Sauli

Daudi na Sauli

Kisha Daudi kuua Goliati, Mufalme Sauli alimuweka kuwa mukubwa wa maaskari wake. Daudi alishinda vita mingi na akajulikana sana. Wakati Daudi alikuwa anatoka ku vita, wanamuke walikuwa wanatoka inje na walikuwa wanacheza dansi na kuimba: ‘Sauli ameua maelfu ya watu, lakini Daudi ameua makumi ya maelfu ya watu!’ Sauli akaanza kusikilia Daudi wivu na akataka kumuua.

Daudi alijua kupiga kinubi muzuri sana. Siku moja wakati Daudi alikuwa anapigia Mufalme Sauli kinubi, Sauli alimutupia mukuki. Mara moja Daudi akakwepa, na ile mukuki ikaingia mu ukuta. Kisha pale, Sauli alijaribu mara mingi kuua Daudi. Ku mwisho, Daudi akakimbia na kujificha mu jangwa.

Sauli akakamata maaskari 3000 na akaenda kuwinda Daudi. Sauli akaingia ndani ya pango kwenye Daudi na wanaume wake walikuwa wanajificha. Wale wanaume wakaambia Daudi kwa sauti ya chini: ‘Hii njo nafasi yako ya kumuua.’ Daudi akaenda polepole karibu na Sauli na akakata sehemu fulani ya koti yake. Sauli hakusikia. Kisha kufanya vile, Daudi akajisikia mubaya juu alikuwa amekosea heshima mufalme, mutiwa-mafuta wa Yehova. Hakuitika wanaume wake waue Sauli. Aliambia hata Sauli kama alipata nafasi ya kumuua lakini hakufanya vile. Unawaza Sauli alibadilisha mawazo yake juu ya Daudi?

Hapana. Sauli aliendelea kuwinda Daudi. Usiku moja Daudi na Abishai, mutoto wa dada yake, waliingia kimya-kimya mu kambi ya Sauli. Hata Abneri, mulinzi wa Sauli, alikuwa amelala. Abishai akasema: ‘Hii njo nafasi ya kumuua! Uniache nimuue.’ Daudi akajibu: ‘Yehova njo atapatia Sauli malipizi. Tukamate tu mukuki wake na mutungi wake wa maji na tuende.’

Daudi akapanda juu ya mulima kwenye angeweza kuona muzuri kambi ya Sauli. Akasema hivi kwa sauti kubwa: ‘Abneri, juu ya nini haukulinda mufalme? Mukuki wa Sauli na mutungi wake wa maji, viko wapi?’ Sauli akatambua kama ilikuwa sauti ya Daudi. Akasema: ‘Ungeniua, lakini haukufanya vile. Ninajua kama wewe njo utakuwa mufalme wa Israeli kisha mimi.’ Sauli akarudia ku nyumba yake ya kifalme. Lakini haiko wote mu familia ya Sauli njo walimuchukia Daudi.

“Kama inawezekana, kwa kadiri inawategemea ninyi, mukuwe wenye kufanya amani na watu wote. Wapendwa, musijilipizie kisasi, lakini muachie kasirani kali nafasi.”—Waroma 12:18, 19