Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

43

Zambi ya Mufalme Daudi

Zambi ya Mufalme Daudi

Wakati Sauli alikufa, Daudi akakuwa mufalme. Alikuwa na miaka 30. Kisha kutawala kwa miaka fulani, usiku moja alikuwa anatembea juu ya nyumba yake na akaona mwanamuke wa sura ya muzuri. Wakaambia Daudi kama ule mwanamuke aliitwa Bat-sheba na kama alikuwa bibi ya askari mwenye aliitwa Uria. Daudi akasema walete Bat-sheba mu nyumba yake ya kifalme. Akalala naye, na Bat-sheba akakuwa na mimba. Daudi alipenda mambo yenye alifanya isijulikane. Akaambia mukubwa wa jeshi lake atie Uria ku mustari wa kwanza wa vita, kisha warudie nyuma na kumuacha yeye peke yake. Kisha Uria kufa ku vita, Daudi akaoa Bat-sheba.

Lakini Yehova aliona mambo yote ya mubaya yenye ilitokea. Angefanya nini? Yehova alituma nabii Natani kwa Daudi. Natani akamuambia: ‘Mwanaume fulani tajiri alikuwa na kondoo mingi, na mwanaume maskini alikuwa na mwana-kondoo moja mudogo mwenye alipenda sana. Ule tajiri akakamata mwana-kondoo wa ule mwanaume maskini.’ Daudi akakasirika na kusema: ‘Ule mwanaume tajiri anastahili kufa!’ Kisha Natani akaambia Daudi: ‘Ule tajiri ni wewe!’ Daudi akahuzunika sana, na akaambia Natani waziwazi: ‘Nimetendea Yehova zambi.’ Ile zambi ililetea Daudi na familia yake magumu mingi. Yehova alipatia Daudi malipizi, lakini alimuacha aendelee kuishi juu aliitika makosa yake na alikuwa munyenyekevu.

Daudi alipenda kumujengea Yehova hekalu, lakini Yehova akasema kama Sulemani, mutoto wake, njo ataijenga. Daudi alianza kutayarishia Sulemani vitu vya kujenga navyo na kusema: ‘Hekalu la Yehova linapaswa kuwa la muzuri sana. Sulemani angali mutoto; lakini nitamusaidia kwa kumutayarishia vitu vya kujenga navyo.’ Daudi alitoa feza mingi juu ya ile kazi ya kujenga hekalu. Alitafuta watu wenye kuwa na ufundi wa kufanya kazi mbalimbali. Alikusanya zahabu na feza, na alileta miti ya mierezi kutoka Tiro na Sidoni. Wakati alikaribia kufa, Daudi alipatia Sulemani plani ya kujenga hekalu. Alimuambia: ‘Yehova aliniambia niandike hii mambo yote kwa ajili yako. Yehova atakusaidia. Usiogope. Ukuwe nguvu na uanze kazi.’

“Mwenye anafunika makosa yake hatafanikiwa, lakini kila mutu mwenye anayaungama na kuyaacha ataonyeshwa rehema.”—Mezali 28:13