Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

44

Sulemani Anajengea Yehova Hekalu

Sulemani Anajengea Yehova Hekalu

Kisha Sulemani kuwa mufalme wa Israeli, Yehova alimuuliza: ‘Unapenda nikupatie nini?’ Sulemani akasema: ‘Ningali kijana, na sijue kile niko ninafanya. Tafazali unipatie hekima juu nijue kuongoza watu wako.’ Yehova akasema: ‘Juu umeomba hekima, nitakufanya ukuwe na hekima kupita watu wote ku dunia. Tena nitakufanya ukuwe tajiri sana. Na kama utanitii, utaishi miaka mingi.’

Sulemani akaanza kujenga hekalu. Alitumia zahabu, feza, mbao, na majiwe ya muzuri sana. Wanaume na wanamuke mingi wenye ufundi walifanya kazi ya kujenga hekalu. Kisha miaka saba, hekalu ilikuwa tayari kutolewa kwa Yehova. Ilikuwa na mazabahu. Na juu ya ile mazabahu kulikuwa zabihu. Sulemani akapiga magoti mbele ya ile mazabahu na kusali: ‘Ee Yehova, hii hekalu haiko kubwa wala haiko ya muzuri kabisa kwako, lakini tafazali ukubali ibada yetu na usikilize sala zetu.’ Unawaza Yehova aliona namna gani hekalu na sala ya Sulemani? Kisha tu Sulemani kumaliza kusali, moto ilishuka kutoka mbinguni na kuchoma zabihu zenye zilikuwa ku mazabahu. Ile ilionyesha kama Yehova alikubali ile hekalu. Wakati Waisraeli waliona vile, wakafurahi sana.

Watu mu Israeli na mu inchi za mbali walimujua Mufalme Sulemani kwa sababu ya hekima yake. Watu wenye walikuwa na magumu walikuwa wanakuja kumuomba Sulemani awasaidie. Hata malkia wa Sheba alikuja kumujaribu Sulemani kwa kumuuliza maulizo ya nguvu. Wakati alisikia majibu ya Sulemani, ule malkia alisema: ‘Sikuamini mambo yenye watu waliniambia juu yako, lakini sasa ninaona kama uko na hekima zaidi kuliko vile walisema. Mungu wako, Yehova, amekubariki.’ Maisha mu taifa la Israeli ilikuwa muzuri, na watu walikuwa na furaha. Lakini mambo ilikuwa karibu kubadilika.

“Muangalie! hapa kuko kitu kikubwa kuliko Sulemani.”—Matayo 12:42