Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

48

Mutoto wa Mujane Anafufuliwa

Mutoto wa Mujane Anafufuliwa

Wakati mvua haikukuwa inanyesha, Yehova aliambia Eliya: ‘Uende Sarefati. Kule, mujane fulani atakupatia chakula.’ Wakati alifika kwenye milango mikubwa ya muji, Eliya alikutana na mujane maskini mwenye alikuwa anakusanya kuni. Akamuomba maji ya kunywa. Wakati alienda kuleta maji, Eliya akamuita na kumuambia: ‘Tafazali, uniletee kipande cha mukate.’ Lakini ule mujane akamuambia: ‘Sina mukate wa kukupatia. Niko tu na unga na mafuta kidogo ya kupika nayo chakula yangu na ya mutoto wangu.’ Eliya akamuambia: ‘Yehova amesema kama ukinitayarishia mukate, unga wako na mafuta yako havitaisha mupaka wakati mvua itaanza tena kunyesha.’

Basi, ule mujane akaenda kwake na kupikia nabii wa Yehova mukate. Sawa vile tu Yehova alisema, ule mujane na mutoto wake walikuwa na chakula wakati wote wenye mvua haikunyesha. Mitungi yake ya unga na mafuta haikupunguka.

Kisha jambo fulani la mubaya likatokea. Mutoto wa ule mujane akagonjwa sana na akakufa. Ule mujane akamulilia Eliya amusaidie. Eliya akakamata ule mutoto mwanaume na kumupeleka mu chumba cha juu cha ile nyumba ya ule mujane. Akamulalisha ku kitanda na kusali hivi: ‘Yehova, tafazali fufua huyu mutoto.’ Aliomba Yehova afanye jambo la kushangaza sana. Unajua juu ya nini? Ni juu, kama vile tunajua, mbele ya pale hakuna mutu mwenye alikufaka kisha akafufuka. Na ule mujane na mutoto wake hawakukuwa hata Waisraeli.

Lakini ule mutoto akaanza kupumua, na akakuwa tena muzima! Eliya akaambia ule mujane: ‘Ona! Mutoto wako iko muzima.’ Ule mujane akafurahi sana na kuambia Eliya: ‘Uko mutu wa Mungu kabisa. Ninajua vile juu unasemaka tu mambo yenye Yehova anakuambia useme.’

“Muangalie kunguru: Hawapande mbegu wala hawavune; hawana chumba cha kuwekea chakula wala depo; lakini Mungu anawalisha. Je, ninyi hamuko wa maana kuliko ndege?”—Luka 12:24